Banner 468

1234453_10201664080105694_1716282793_n
Facebook

HOTTEST HEADS OF STATE..


  1. Yulia Tymoshenko Prime Minister of Ukraine
    -
  2. Stoltenberg
    Jens Stoltenberg Prime Minister of Norway
    -
  3. Wangchuck
    Jigme Khesar Namgyel Wangchuck King of Bhutan
    -
  4. Kabila
    Joseph Kabila President of the Democratic Republic of the Congo
    -
  5. Kirchner
    Cristina Fernández de Kirchner President of Argentina
    -
  6. Correa
    Rafael Correa President of Ecuador
    -
  7. Henri
    Henri Grand Duke of Luxembourg
    -
  8. Skerrit
    Roosevelt Skerrit Prime Minister of Dominica
    -
  9. Macapagal-Arroyo
    Gloria Macapagal-Arroyo President of the Philippines
    -
  10. Topi
    Bamir Topi President of Albania
    -
  11. Bachelet
    Michelle Bachelet President of Chile
    -
  12. Lukashenko
    Alexander Lukashenko President of Belarus
    -
  13. Gusmão
    Xanana Gusmão Prime Minister of East Timor
    -
  14. Nasheed
    Mohamed Nasheed President of the Maldives
    -
  15. Obama
    Barack Obama President of the United States of America
    -
  16. Loong
    Lee Hsien Loong Prime Minister of Singapore
    -
  17. Funes
    Mauricio Funes President of El Salvador
    -
  18. Putin
    Vladimir Putin Prime Minister of Russia
    -
  19. Nkurunziza
    Pierre Nkurunziza President of Burundi
    -
  20. Kikwete
    Jakaya Kikwete President of Tanzania
    ree-
[ Read More ]

Child actor of Slumdog Millionaire loses his father


Mohmmed Azharuddin played the role of elder brother of the protagonist in the first half of the Oscar winning film Slumdog Millionaire. He lost his father on Friday.

The child actor was away at school at the time of his father’s death. According to family members the child was not aware of the declining health of his father.

Ismail Shaikh, 46, died due to tuberculosis. He was suffering from advanced tuberculosis for past two years. Apart from Azharuddin, Shaikh is survived by his wife Shamim, an older son and two daughters.

Shamim said that Shaikh had neglected his health and was totally immersed in making a bright future for Azharuddin, especially after the Slumdog Millionaire became an international box-office hit.

The child actor recently shifted to his new Santacruz home. Director Danny Boyle of the film has sent his condolences to the family. He will be visiting the family next month to express his support to the family.

[ Read More ]

Wachomana Sindano Zenye Damu Yenye Ukimwi China

Mashambulizi ya watu kuchomwa sindano zinazohofiwa kuwa na damu yenye virusi vya ukimwi, yamezidi kuongezeka katika jimbo lililokumbwa na vurugu za kikabila la Xinjiang lililopo magharibi mwa China. Kumekuwa na kuongezeka kwa idadi ya watu wanaoshambuliwa kwa kuchomwa sindano zinazohofiwa kuwa zina damu yenye virusi vya ukimwi au kemikali zenye sumu katika mji wa Urumqi uliopo kwenye jimbo la Xinjiang magharibi mwa China pamoja na kwamba serikali ya China imeweka ulinzi mkali kwenye jimbo hilo kuzuia mashambulizi hayo.

Mashambulizi hayo yanatokana na vurugu za kikabila kati ya kabila dogo la Uygur ambalo wengi wao ni waislamu na kabila kubwa la Han.

Wakazi wa mji huo wa kabila la Han wamekuwa wakiwalaumu watu wa kabila la Uygur kufanya mashambulizi hayo ya kuwachoma watu sindano.

Jumla ya watu 45 kutoka makabila yote mawili wameishakamatwa katika mji huo wakituhumiwa kuhusika na mashambulizi hayo ya kutumia sindano.

Polisi katika jimbo la Xinjiang walitangaza kupokea ripoti ya watu 77 kushambuliwa na kuchomwa sindano hizo katika kipindi cha kuanzia jumapili mchana mpaka jumatatu mchana.

Taarifa za awali zilisema kwamba kulikuwa na jumla ya watu 531 waliokumbwa na mashambulizi hayo ya kuchomwa sindano katika wiki chache zilizopita.

Baada ya wiki iliyopita maelfu ya watu kuandamana kwenye mji huo kutaka serikali iongeze ulinzi kukomesha mashambulizi hayo, serikali ya China iliamua kupeleka majeshi yake na polisi wengi sana katika mji huo kulinda amani.

Mashambulizi hayo yamesababisha hali tata kwenye mji huo na kutishia kutokea tena kwa vurugu kubwa za kikabila kama zilizotokea julai 5 mwaka huu ambazo zilisababisha vifo vya takribani watu 200 wengi wao wakiwa ni watu wa kabila la Han.

Taarifa iliyotolewa na serikali ya China ilisema kuwa watu watakaopatikana na hatia ya kuwadhuru watu kwa kutumia sindano, watahukumiwa adhabu ya kifo.

Hofu ya sindano hizo kuwa na damu yenye virusi vya ukimwi imetokana na kwamba jimbo la Xinjiang ndilo jimbo linaloongoza kwa waathirika wa ukimwi nchini China kukiwa na jumla ya waathirika 25,000 katika jimbo hilo kwa mujibu wa takwimu za mwaka jana. Idadi hiyo kubwa inasababishwa na watumiaji wengi wa madawa ya kulevya katika jimbo hilo kutumia sindano zilizotumiwa na wenzao.

source:nifahamishe
[ Read More ]

Urembo wamtumbukia nyongo.


Jitihada za kutafuta urembo wa ziada za mwanamke mmoja wa nchini Marekani zilimtokea puani baada ya sura yake kuharibika vibaya kiasi cha kuwa vigumu kutambulika alipoamua kujidunga sindano za urembo za silikoni.Mary Johnson mwenye umri wa miaka 54 mkazi wa California nchini Marekani katika jitihada zake za kutafuta urembo wa ziada aliamua kufanya upasuaji wa kurekebisha sura yake aonekane kijana na mrembo. Lakini Mary ambaye ni mama wa watoto watatu alipoambiwa kuwa upasuaji wa kurekebisha sura yake utamgharimu maelfu ya dola za Marekani, aliamua kughairi kufanya upasuaji huo hospitalini na kuamua kutumia njia za kujidunga sindano za silikoni. Baada ya kufanya utafiti kwenye Internet Mary alinunua sindano za kimiminika cha silikoni kwa dola 10 tu na kujidunga mwenyewe kwenye mdomo wake na kwenye mashavu yake. Badala ya sindano hizo kumfanya aonekane mrembo kama alivyotarajia, ziliiharibu kabisa sura yake na kuifanya iwe vigumu kwa mtu kumtambua. Baada ya muda mfupi sura yake ilianza kubadilika rangi na kuvimba na kwenye kona za mdomo wake kulitokea vidonda vikubwa visivyoeleweka. Hali ilikuwa mbaya kiasi cha kusababisha Mary awahishwe hospitali na kufanyiwa upasuaji wa kuifanya sura yake irudie hali yake ya zamani. Hivi sasa ingawa sura ya Mary imerudia hali yake ya zamani, Mary anakiri kujutia uamuzi wake wa kutafuta urembo wa ziada.

source:nifahamishe.com
[ Read More ]

Mama Awauwa Watoto Wake Wanne Akidai Wana Mashetani Wabaya


Mama mmoja nchini Marekani amepandishwa kizimbani kwa tuhuma za kuwaua watoto wake wanne akidai walikuwa wame wameingilwa namashetani wabaya.
Banita Jacks, 33, wa Washington nchini Marekani amefunguliwa mashtaka manne ya mauaji ya watoto wake wanne wa kike wenye umri kati ya miaka mitano na 17.

Banita alikamatwa nyumbani kwake akiishi na mabaki ya miili ya watoto wake ambao maiti zao zilikuwa zikiozea ndani ya nyumba hiyo.

Banita alidai kuwa watoto hao walikuwa na mashetani wabaya na walikufa mmoja mmoja wakiwa usingizini.

Ndugu wapatao 30 wa familia ya Banita waliohudhuria kesi hiyo mahakamani waliondoka mahakamani kimya kimya bila kutaka kusema chochote.

Miili ya watoto hao iligundulika wakati polisi walipoingia nyumbani kwa mama huyo kusini mashariki mwa Washington mwezi januari mwaka jana.

Banita aliwaambia wapelelezi kuwa watoto wake walikuwa wakimilikiwa na mashetani wabaya na walianza kufariki mmoja mmoja wakiwa usingizini katika muda wa siku saba.

Banita aliwaambia pia wapelelezi hao kuwa aliwanyima chakula watoto wake hao kwa muda mrefu kabla ya vifo vyao.

Mchunguzi wa mambo ya kidaktari, Dr. Marie-Lydie Pierre-Louis alisema kuwa kwa kuangalia vielelezo vya idadi kubwa ya wadudu waliokutwa kwenye maiti hizo, miili ya watoto hao ilikuwa ndani ya nyumba aliyokuwa akikaa mama huyo kwa zaidi ya siku 15 kabla ya kugundulika.

Polisi walisema kuwa Banita alizuga amehama kwenye nyumba aliyokuwa akikaa kwa kufunga mapazia yote ya nyumba yake na kuacha kulipa bili za umeme na kuacha barua zake zirundikane mbele ya nyumba yake huku yeye akitumia mlango wa nyuma kutokea.

Banita huenda akafungwa kifungo cha maisha iwapo atapatikana na hatia.


SOURCE:nifahamishe.com


[ Read More ]

Askari wadaiwa kuua mpita njia Dar

ASKARI wa jeshi la polisi jijini Dar es Salaam amedaiwa kumpiga risasi Hassani Likanoga (24), mwanafunzi mtarajiwa wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam wakati alipokuwa wakipiga risasi gari moja lililodhaniwa kuwa ni la majambazi.

Tukio hilo la kusikitisha lilitokea Julai 10 mwaka huu majira ya saa nane mchana katika eneo la Tandika jijini Dar es Salaam wakati polisi walipokuwa wakifukuza gari hilo aina ya Toyota RAV 4.

Mashuhuda wa tukio hilo waliliambia Mwananchi kuwa, eneo la mtaa wa Mbwela uliopo Tandika uligeuka na kuwa Darfur kwa muda wakati mirindimo ya risasi ilipokuwa ikirushwa kutoka kwenye gari la polisi kuelekea kwenye gari lililokuwa mbele lililodaiwa kuwa ni la majambazi.

Mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo Shabani Ramadhani aliliambia Mwananchi "Nikiwa kibarazani nimekaa niliyaona magari matatu yakifukuzana, gari moja ndogo aina ya Toyota RAV 4 likiwa limetangulia na limefunga vioo vyote na nyuma yake kulikuwa na magari mawili, moja likiwa ni la polisi na jingine lilikuwa Suzuki ambalo baadaye niligundua kuwa lilikuwa likitumiwa na polisi."

Alisema risasi hizo zilianza kurushwa muda mfupi baada ya magari hayo kuacha barabara ya lami inayoelekea Tandika na Mwembe Yanga na kuelekea barabara ya Vumbi inayokatisha mtaa wa Mbwela.

Alisema risasi hizo ambazo zilianza kurushwa mfululizo zililifanya eneo hilo kuwa katika hali ya hatari kwani zingine zilirushwa juu, nyingine chini na nyingine zililenga usawa wa gari walilokuwa wakilifukuza.

"Risasi hizo ambazo muda wote zilipigwa ovyo nyingine zilipigwa juu na nyingine chini huku nyingine zikilenga gari walilokuwa wakilifukuzia zikitokea kwenye gari la polisi ambalo nyuma yake kulikuwa na askari wawili tu,"alisema Ramadhani.

Alisema muda mfupi baadaye aliona mtu akianguka chini baada ya kupigwa risasi iliyotoka kwenye gari la polisi na ulipotoweka msafara huo walikwenda kumwangalia na kukuta marehemu akiwa amejeruhiwa sehemu ya shingoni huku damu ikimtoka kwa wingi.

Alisema baada ya tukio hilo lilijitokeza kundi kubwa la wasamaria wema akiwamo yeye na kwenda kutoa msaada kwa kijana huyo kwa lengo la kumpeleka hospitalini.

"Ingawa tulikuwa hatumjui, lakini kwa tukio lile tuliloliona sote tulijua wazi kuwa hakuwa jambazi, hivyo umati mkubwa watu ulilazimika kukimbnilia hapo na kuanza kutoa msaada wa kila namna ikiwa ni pamoja na kufanya juhudi za kumkimbiza hospitalini," alisema Ramadhani.

Kwa upande wake George Kiondo alifafanua kuwa kazi ya kumtafutia usafiri kijana huyo iligeuka kuwa ngumu baada ya magari yaliyokuwa yakipita katika eno hilo kukataa na kukimbia.

"Tulisimamisha gari la kwanza likakimbia, tukasimamisha la pili likakimbia ndipo tulipoamua kwa umoja wetu kutanda barabarani na kuzuia magari yote yaliyokuwa yanapita hapo kisha tukafanikiwa kumnyang'anya ufunguo dereva mmoja na kumlazimisha kumpakia kijana huyo kwa ajili ya kwenda hosptalini," alisema Kiondo.

Kiondo alibainisha adha nyingine waliyokutana nayo kuwa walipokuwa wakijitayarisha kumpakia kijana huyo gari lililodaiwa lilikuwa likitumiwa na Polisi aina ya Suzuki lilifika katika eneo hilo na kushuka askari mmoja kisha kuanza kufyatua risasi hewani huku akiwataka watu wote kutawanyika.

Kiondo alisema tulisikia sauti ikisema "Tawanyikeni sitaki kuona mtu katika eneo hilo ondokeni haraka" akimnukuu askari huyo anayedaiwa alikuwa akifyatua risasi hewani.

Alisema kizaazaa hicho kiliwalazimu umati mkubwa wa watu waliokuwa wakijaribu kutoa msaada kwa kijana huyo kukimbia hivyo kubaki idadi ndogo ya watu waliosimama na kumsisitiza askari huyo kuwa eneo hilo halikuwa na ujambazi bali wao wanashughulikia suala la kumpeleka kijana aliyekuwa amejeruhiwa kwa risasi hospitalini.

Alisema baada ya polisi huyo kuelezwa hivyo alirudi kwenye gari na kuondoka na ndipo wao walipompakia kijana huyo kwenye gari na kumpeleka kituo cha polisi cha Chang'ombe ambako walipewa PF3 na kumpeleka kijana huyo katika hosptali ya Temeke kwa ajili ya matibabu.

Mwananchi alipomtafuta Kamishna msaidizi wa Polisi na kamanda wa Kanda maalumu ya Dar es Salaam Sulemani Kova alisema,"Kwa kuwa tukio hilo limetokea Temeke wasiliana na Kamanda wa huku atakupa maelekezo yote"

Kamanda wa mkoa wa Temeke Liberatus Sabas alipopigiwa simu mara ya kwanza alijibu akisema alikuwa kwenye gari hivyo kumtaka Mwanandishi kumtafuta baadaye.

[ Read More ]

HONGERA IRENE.


muigizaji filam maarufu wa inchini Tanzania irene uwoya hatimae amefunga pingu za maisha na Ndikumana.


more photos:global publisher.com
[ Read More ]

huyu ng'ombe au????????


[ Read More ]

watu wa nne wafariki dunia katika mapigano nchini india.


watu wapatao sita wamefariki dunia katika mapigano kati ya madhehebu maarufu nchini mysore india,mapigano hayo ambayo yalisababisha shunguli nyingi kusitisha kwa muda ikiwemo shule,vyuo vikuu,maofisi na maduka yote kufungwa kwa muda.Kitahanani hicho kilitokea katika maeneo ya udayagiri pale dhehebu la hindu walipomchinja ngurue na kumuingiza msikitini mnyama ambae kwa waislam ni gharamu, watu wapatao wa nne walifariki dunia katika mapigano hayo mali mbali mbali ziliharibia zikiwemo gari na baadhi ya maduka kuchomwa moto.
[ Read More ]

huu ni mfano mzuri wakuigwa tz.


laiti kama tz kungekua na mitaro kama haya kungeondosha usumbufu kipindi cha mvua.
[ Read More ]