Banner 468

1234453_10201664080105694_1716282793_n
Facebook

DAME ELIZABETH TAYLOR (MJ'S BEST FRIEND) DIES @ 79 FROM HEART FAILURE IN HOSPITAL


Last of the Hollywood greats: Dame Elizabeth Taylor has died in hospital aged 79 of congestive heart failure
Her last show: Elizabeth was snapped celebrating her 79th birthday a month early in January before she was admitted to hospital a few days after


Dame Elizabeth Taylor, one of the 20th Century's biggest movie stars, has died in Los Angeles at the age of 79.

The double Oscar-winning actress had a long history of ill health and was being treated for symptoms of congestive heart failure.
Her four children were with her when she died at Cedars-Sinai Medical Center, her publicist said.
In a statement, her son Michael Wilding called her "an extraordinary woman who lived life to the fullest".
"We know, quite simply, that the world is a better place for Mom having lived in it," he continued.
"Her legacy will never fade, her spirit will always be with us, and her love will live forever in our hearts."


Dame Elizabeth's most famous films included National Velvet, Cleopatra and Who's Afraid of Virginia Woolf?
She was equally well-known for her glamour and film partnership with Richard Burton, one of seven husbands.
In her prime, she was arguably one of the world's greatest actresses and most beautiful women.
Her colourful private life, screen success and Aids charity work ensured she was never far from the spotlight since finding fame at the age of 12.
The peak of her film career came in the 1950s and 1960s, with four Oscar nominations in a row from 1958 to 1961.
She lost out in her first three attempts - for Raintree County, Cat on a Hot Tin Roof and Suddenly, Last Summer - but triumphed at her fourth attempt with Butterfield 8.



She met the actor while filming 1963's Cleopatra - which became notorious as one of the most expensive films of all time, but which also sparked one of Hollywood's greatest romances. 
Her second Oscar came in 1967 for Who's Afraid of Virginia Woolf?, one of 12 films with Burton.

Taylor had already been married four times - to Conrad Hilton Jr, Michael Wilding, Michael Todd and Eddie Fisher - before she wed Burton in 1964.
Their tempestuous relationship saw them divorce and remarry in 1975 before she moved on to further marriages with John W Warner and Larry Fortensky.
Her health problems began with a fall while filming her first hit film, National Velvet, which led to a lifetime of back problems.
A rare strain of pneumonia almost killed her in 1961 and she also battled addictions to alcohol and painkillers.
In the 1990s, she endured two hip replacement operations and another near-fatal bout of pneumonia and survived surgery for a benign brain tumour in 1997.
In 2004, it was revealed that she was suffering from congestive heart failure, with symptoms including fatigue and shortness of breath, and scoliosis, which twisted her spine.
But she continued to campaign for her Aids charity, which she set up in 1991 after the death of her friend and co-star Rock Hudson.
In addition to her four children - Michael Wilding, Christopher Wilding, Maria Burton-Carson and Liza Todd-Tivey - Dame Elizabeth is survived by 10 grandchildren and four great-grandchildren.
A private family funeral will be held later this week. Instead of flowers, the family has requested that contributions be made to the Elizabeth Taylor Aids Foundation.
[ Read More ]

Kasheshe kwa wanaotaka kusoma Uingereza



Maandamano ya wanafunzi Uingereza
Sheria za kupata viza za wanafunzi nchini Uingereza zinatarajiwa kuwa ngumu zaidi- baada ya kuibuka wasiwasi kuwa mbinu za kuingia nchini humo kwa minajil hiyo hutumiwa kiudanganyifu
Waziri wa mambo ya ndani Theresa May alisema viza za wanafunzi hazitumiwi inavyotakiwa na "wengi wamekuja hapa kufanya kazi na si kusoma".
Alitangaza mpango wa kupunguza idadi ya viza za wanafunzi kufikia 80,000- takriban robo ya idadi iliyopo sasa.
Waziri kivuli wa wizara ya mambo ya ndani Yvette Cooper alionya sheria hazitakiwi kuharibu idara zenye thamani ya dola za kimarekani bilioni tano kwa mwaka.
Bi May aliliambia bunge kuwa matumizi mabaya ya viza za wanafunzi yamekuwa "ishara ya mfumo wa uhamiaji uliotumiwa vibaya".

Sheria za lugha

Sheria ngumu zilizowekwa ni pamoja na mwanafunzi kutakiwa kuzungumza lugha ya Kiingereza.
Bi May alisema alitaka kumaliza tatizo ambapo wale wanaojifanya wanafunzi hufika kwenye uwanja wa ndege wa Uingereza na kushindwa hata kutaja masomo wanayotarajia kufanya.
Pia utaratibu utazidi kubanwa kwenye kuwaruhusu wanaolelewa na mwanafunzi huyo kujiunga naye Uingereza- na idadi ya miaka ya wanafunzi kutoka nje kukaa Uingereza baada ya kumaliza masomo yao itapunguzwa.
Katika kukabiliana na wasiwasi wa viza za wanafunzi kutumiwa vibaya na wahamiaji wa kiuchumi, kutakuwa na kiwango maalum cha saa za kufanya kazi kwa wanafunzi kutoka nje.
Awali vyuo vikuu vilionyesha wasiwasi wa kupoteza wanafunzi kutoka nchi za nje kutokana na sheria kali za kuomba viza.
Vikwazo vingi vinawalenga wanafunzi walio katika vyuo vya watu binafsi badala ya vyuo vikuu.
Hata hivyo Bi May aliwaambia wabunge kwamba "njia kama hiyo" ya kusoma kupitia vyuo vikuu vitalindwa, iwapo tu vyuo vikuu vitawadhamini wanafunzi.
[ Read More ]

WASANII 13 WA FIVE STARS MODERN TAARAB WAFARIKI KATIKA AJALI

WATU wapatao 13 wamefariki dunia na wengine kujeruhiwa vibaya katika ajali ya basi aina ya Coaster lenye namba za usajili T 361 BGE lililokuwa limebeba wanamuziki wa kundi la Five Stars Modern Taarab waliokuwa wakitokea Kyela-Mbeya kueleka jijini Dar.

Ajali hiyo ilitokea jana majira ya saa mbili usiku ndani ya hifadhi za wanyama za Mikumi mkoani hapa, baada ya gari hilo kuligonga kwa nyuma roli aina ya Scania lenye namba za usajili T 848 APE lililokuwa linavuta tela lenye namba za usajili T 559 BDL liliokuwa na mzigo wa mbao.


ZIFUATAZO NI PICHA ZAIDI ZA TUKIO HILO:





Waliofariki katika ajali ya Bendi ya Five Star ni pamoja na 
Issa Kijoti, Omar Tolu, Haji Babu, Sheba Juma, Omar Hashim, Tizo Mgunga, Hamisa Mipango, Husna Mapande, Samir Maulid, hasan Ngereza, Rama Kinyoya, Nasoro Madenge na mcheza shoo wakitu tigo mmoja.


Hawa ni marehemu waliokufa kwenye ajali hiyo na mwili wa tatu ndio Issa Kijoti aliyekuwa mwimbaji mzuri kabisa katika bendi hiyo ya Five Star Mordem Taarabu





































Yafutayo ni majina ya wana Five Stars waliothibitishwa kufa hadi sasa:

Issa kijoti - mwimbaji
Husna mapande-mwimbaji
nasoro madenge - mkurugenzi 
Sheba juma - mpiga solo
Omari hashimu- mpiga bass
Omari tall- fundi mitambo
Hamisa mussa - mwimbaji
Rama kinyoya - mwimbaji
Tizo mgunda - mcheza shoo
Haji mzaniwa - fundi mitambo

source;global publisher.
[ Read More ]

MAJONZI MAKUBWA TANZANIA!!!!!!! KUNDI LA TAARABU LA FIVE STARS LAPATA AJALI USIKU HUU, ZAIDI YA WATU 10 WAHOFIWA KUFA!!!


Hawa ndo baadhi ya wanamziki wa Five Star Modern Taarab
WANAMUZIKI WA BENDI YA FIVE STAR MODERN TAARABU ZAID YA 10, WAMEPOTEZA MAISHA KWA AJALI YA GARI HUKO MOROGORO ENEO LA MIKUMI NA WENGINE KUJERUHIWA VIBAYA SANA NA HALI ZAO NI MBAYA. GARI HILO LILIKUWA NA WATU 22, LAKINI WAMENUSURIKA 5, HUKU WATATU WAKIWA WAMEUMIA KIDOGO. KWA MUJIBU WA VYANZO VYA HABARI INADAIWA GARI HILO LILIKUWA KWENYE MWENDO MKALI NA KUPELEKEA KUGONGA LORI LILILOKUWA LIMEPAKIA MBAO PEMBENI YA BARABARA, KUGONGA HUKO ILIPELEKEA VIFO VYA WATU 8, HAPO HAPO NA KISH AKAENDA UPANDE WA PILI AMBAPO LORI LINGINE LILIKUWA LINATEMBEA NDIPO ILIPOISHIA NA KUSABABISHA VIFO HIVYO ZAIDI YA 10, NA MAJERUHI WENGI.MAITI ZIMEHAARIBIKA VIBAYA SANA HALI AMBAYO HAZITAMBULIKI KUTOKANA KUWA VIWILI WILI. 

Habari kwa hisani ya Andrew Chale (Tanzania Daima)
[ Read More ]

Makaazi ya Kanali Gaddafi yashambuliwa

Ndege zake za kijeshi, zimeshambulia makaazi ya Kanali Gaddafi mjini Tripoli na kusababisha uharibifu mkubwa kwenye jengo moja.
Viongozi wa muugano wa majeshi hayo wanasema jengo lililoharibiwa lilikuwa linatumika kuamrisha majeshi ya Libya yanayopigana na waasi.
Waandishi wa habari wametembezwa kwenye eneo hilo lakini hakuna taarifa ikiwa maafa yalitokea baada ya shambulizi hilo.
Naibu mkuu wa jeshi la wanamaji wa marekani Bill Gortney anasema mashubulizi hayo hayaja mlenga kanali Gaddafi.
vifaru vya serikali vinateketea
Televisheni ya Libya imeonesha maiti na magari ya kijeshi yaliyoteketea kwenye barabara ya kuelekea mji wa Benghazi, shina la wapinzani wa serikali
Msemaji wa serikali ameeleza kuwa watu 64 wameuwawa katika mashambulio yaliyofanywa na mataifa ya magharibi, lakini hakuna njia ya kuthibitisha taarifa hiyo.
Awali afisa mkuu wa jeshi la Marekani, , Mike Mullen, alisema ndege kutoka Qatar zinapelekwa huko, kuwa tayari kushiriki katika operesheni dhidi ya Libya, na nchi nyengine piya zimetoa ahadi kusaidia.
Adimeri Mullen alieleza kuwa agizo la Umoja wa Mataifa, la kuzuwia ndege za serikali kuruka katika anga ya Libya, sasa limetekelezwa, na majeshi ya Kanali Gaddafi, katika mji wa Benghazi, unaodhibitiwa na wapinzani, sasa hayawezi kusonga mbele.
Alisema hakuona taarifa, kuwa raia wameuwawa.
mpinzani na bunduki yake karibu na Benghazi
mpinzani na bunduki yake karibu na Benghazi
Urusi imetoa wito kwa Uingereza, Ufaransa na Marekani, ziache kushambulia maeneo yasiyokuwa ya kijeshi, na kwamba raia wameshambuliwa.
Mkuu wa Jumuiya ya Kiarabu, Amr Moussa, amesema mashambulio yamekwenda mbali, kushinda lile lengo la kulinda tu anga ya Libya, ambavyo ndivo jumuiya yake ilivotaka.
[ Read More ]

Uzinduzi Rasmi wa Flaviana Matata Foundation ni May 21st, 2011

 May 21st is always a special and very difficult day for me, my family and the families of thousands who lost their loved ones on that fateful day in 1996, when MV Bukoba sank in Lake Victoria. On that day I lost my mother, but never lost hope. I knew a day would come and will be able to cherish her memory and do something special to honor her life and the life she game me.

I am happy to announce that on May 21st, 2011 I will officially launch the FLAVIANA MATATA FOUNDATION in the honor of my beloved mother. As a former Miss Universe Tanzania, and currently, a model based in New York and Europe, I would like to use my fame to help the most vulnerable in our society… young women and kids.

 FLAVIANA MATATA FOUNDATION, a Tanzanian registered nonprofit organization, will give leaders in health, business, government and communities globally the opportunity to be a part of a movement that relies on participation, collaboration and action to reverse child pregnancy rates, and empowering of young women and kids and the like. I consider this to be my greatest achievement, and gives me joy to see that my mother’s memory has a chance to live forever. I hope this initiative will bring happiness and joy to many that will be touched directly and indirectly by FLAVIANA MATATA FOUNDATION. Please reserve this date (May 21st, 2011) to come and join me in the launch of this very important initiative. Venue, time, and special guests will be announced at a later stage.THANK YOU


Regards


Flaviana Matata(Lavvy)
[ Read More ]

Mama Mwanamwema Shein Akutana na Wake za Mambozi wa Afrika Ikulu Zanzibar

 Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein (Kulia)akizungumza na Mwenyekiti wa jumuiya ya wake za mabalozi wa afrika waliopo Tanzania Bi Aletha Isack Ikulu Mjini Zanzibar Jana

 Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein akizungumza na wake za mabalozi ambao ni wanachama wa chama cha wake za Mabalozi Afrika.

 Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein akonyesha jambo kwa wake za Mabalozi wa afrika ikulu mjini zanzibar jana.
Picha na Yussuf Simai-MAELEZO,Zanzibar
[ Read More ]

ZANZIBAR IMEJIANDAA VIPI NA TSUNAMI?

Hivi karibuni tumeshuhudia katika vyombo vya habari madhara makubwa yaliyotokea Japan kutokana na mtetemeko mkubwa wa Ardhi pamoja na Tsunami. Maelfu ya watu wamefariki na wengine bado hawajulikani hatima yao kutokana na mawimbi makubwa yenye kina cha mita kumi kufika ardhini kwa kasi na kuharibu kila kilichosimama.

Madhara makubwa yametokea katika mji wa Sendai kaskazini mashariki mwa Japan na sehemu nyingi ambazo zipo kando kando na bahari zimeathirika vibaya sana kutokana na Tsunami. Waziri Mkuu wa Japan ameliweka tukio hili sawa na yaliyotokea takriban miaka 60 iliyopita Vita vya pili vya Dunia.

Japan ni nchi iliyoendelea. Iliwahi kukumbwa na Tsunami 1920 ambapo watu 120,000.00 walifariki. Japan ni nchi iliyopo katika mkanda wa ardhi ambao hutokea matetemeko mengi ya Ardhi na imejiandaa kadri ya uwezo wake kukabiliana na majanga ya aina hii.

Licha ya ukubwa wa mtetemeko katika kipimo cha Richter (Richter scale) 8.9, hatukuona nyumba zilizoanguka kutokana na mtetemeko (zilizoanguka zilikumbwa na dhoruba ya tsunami) wakati majuzi tu New Zealand ilipata mtetemeko ambao ni maradufu kulinganisha na Japan lakini nyumba nyingi ziliharibiwa. Japan inajenga nyumba zake quake proof (tayari zina hifadhi na mitetemeko)

Zanzibar si mgeni wa majanga lakini nina imani Mola wetu anatupa yetu kutokana na hali zetu ‘dhooful haal’. Mwaka 2009 tulipata mtihani wa kuzama meli Mv Fatih wakati ikijaribu kutia nanga bandarini. Meli ilichukua muda mrefu kuopolewa tena kwa msaada kutoka Tanganyika. Watu sita walifariki. Tume iliundwa na ikaleta ripoti. Mapendekezo yalifanyiwa kazi Kwani hatukuwa na Tagi lenye winchi nzito ya kuweza kuibeba Meli na Jitihada nyingi za kienyeji zilizokosa utaalamu zilijaribiwa na kufeli.

Mwaka 2009 huo kuna meli mbili pacha zilikuwa matengezoni Mtoni Mv Aziza 1+2, nazo zilishika moto. Vikosi vya zimamoto viliitwa kudhibiti hali kwa kuwa Meli zilikuwa karibu na ufukwe. Je ikitokea Meli kuwaka na iko nangani tuna kifaa chochote cha kuweza kuzima moto baharini?

Mwaka 2005 kulitokea mvua kubwa za El Nino. Maeneo mengi yalijaa maji na nyumba nyingi kuharibika katika maeneo ya Kwahani, Sebulani, Kwamtipura na kadhalika.

Mawimbi ya Tsunami yanaweza kutembea masafa marefu na kwa kasi na kuweza kuathiri sehemu nyengine ambazo hazipati mtetemeko wa lakini zinaweza kupata athari za Tsunami kama ilivyotokea mwaka 2006 Kusini mashariki mwa Asia ambapo mawimbi yaliweza kufika mpaka fukwe za Somalia, Kenya na kadhalika.

Ulimwengu hutoa tahadhari ‘alert’ ya kujuulisha kuwepo kwa tsunami. Ingawa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imewataka wananchi wanaoishi katika mwambao wa Bahari ya Hindi kuondoa wasiwasi wa kukumbwa na hali hiyo, hivyo wanapaswa kuendelea na shughuli zao ila suala la kimsingi endapo hali hii itatokea wananchi tayari wameshaelimishwa (awareness) nini wanatakiwa kufanya? Je vipi idara yetu ya hali ya hewa ina utaratibu wowote wa kupokea hizi tahadhari na huzifanyia kazi angalau kuwatahadharisha wananchi, wavuvi, wasafiri ambao hutumia bahari?

Kuna mazoezi yoyote yaliyowahi kufanyika kama “drill” ambayo yangelioneshwa kwa televisheni zetu vipi mwananchi akiwa baharini, nchi kavu, kando kando mwa bahari anatakiwa afanye? Japan kukitokea mtetemko, kila mwananchi anajua nini afanye vipi ajipange katika kuikabili hali hii.Kuna matangazo yoyote au vipeperushi vilivyoandaliwa ambavyo vinatoa taarifa na maelekezo likitokea janga la tsunami nini wananchi wafanye?

Na vipi hiyo taarifa ya tahadhari itaweza kutolewa kwa kutumia njia gani, redio, Tv, simu, mdomo kwa mdomo pasipo kuleta kuhamanika (panic) na kitahanani kwa wananchi na kwa muda wa haraka na hapa ndipo panapohitaji maandalizi na mipangilio.

Zanzibar ni nchi masikini. Lakini umasikini wetu usiwe kigezo cha kukosa maandalizi angalau kwa kadri ya uwezo wote na hili tusisubiri wafadhili waje kutusaidia ili kukitokea majanga au maafa tuweze kujipanga.Umasikini wetu usiwe sababu ya kutukwaza katika mambo ambayo yataweza kuokoa maisha ya watu hasa ukizingatia mazingira ya kisiwa chetu jinsi kilivyo takriban sawa na usawa wa bahari kwa maeneo mengi. Wimbi la mita tano tu likija kwa nguvu ya tsunami basi nusu ya mji wa Zanzibar upo majini. Madhara yake ni Allah pekee anayejua.

Tusisubiri yatokee kisha tuanze kuunda tume, tuwe ‘proactive’ wabunifu kabla ya majanga na maafa na huku ndiko kujiandaa tunakoshauri vyombo husika kama Tume ya Maafa na kadhalika hasa kwa majanga ambayo yanaweza kutukabili katika maeneo yetu kutokana na hali halisi ya kiulimwengu na mabadiliko ya hali ya hewa.

Ndiyo tuna matatizo mengi na hili la tsunami si la kutuumiza vichwa kama baadhi yetu wakatakavyotumia hoja ya kudadisi haja ya kujiandaa na tukio hili la ‘kufikirika’ Ila msemo wetu wa Kiswahili unatukumbusha ‘mwenzako akinyolewa...

Tumuombe Mola wetu atuepushe na majanga na maafa kwa rehma na nguvu zake Subhaana.

source;othman  mapara.

[ Read More ]