Banner 468

1234453_10201664080105694_1716282793_n
Facebook

Basi laua watano Dodoma

-
Rehema Mwinyi.

WATU watano wamekufa baada ya basi la abiria kupinduka leo saa tano asubuhi wakati likitoka Dar es Salaam kwenda mkoani Singida.

Basi hilo liitwalo, Hajjiz, aina ya Scania lilipinduka baada ya tairi ya mbele kupasuka.

Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Dodoma, Salum Msangi amesema, basi hilo lenye namba za usajili T 441 AYN lilipinduka saa 5.40 katika kijiji cha Mtumba, takribani kilomita 17 kutoka mjini Dodoma.

Inadaiwa kuwa watu wanne walikufa papo hapo, mwingine alifariki dunia wakati akikimbikizwa hospitali.

Kwa mujibu wa Msangi, walioshuhudia ajali hiyo wamedai kuwa basi hilo lilikuwa kwenye mwendo mkali, na baada ya ajali dereva alikimbia polisi wanamtafuta.

Leave a Reply