Banner 468

1234453_10201664080105694_1716282793_n
Facebook

Michael Jackson: Mazishi yake dili

-
Rehema Mwinyi.



Mazishi ya Mfalme wa Pop Duniani Michael Jackson yamegeuka kuwa 'dili' la aina yake baada ya watu kibao kugombea nafasi ya kuhudhuria shughuli hiyo.

Taarifa zinaeleza kuwa hadi sasa, zaidi ya watu 500,000 wamejisajili kwa ajili ya kucheza bahati nasibu ya kuwania tiketi kiduchu, zinazotajwa kuwa ni 17,500 pekee ili kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa Michael Jackson.

Uwanja wa mpira wa kikapu wa Staples Center Jijini Los Angeles ndio utakaotumika Jumanne ijayo kwa shughuli za kumuaga mwanamuziki huyo aliyefariki ghafla Alhamisi iliyopita.

Hata hivyo, wakati watu kibao wakiwania kushiriki mazishi ya mfalme huyo wa pop duniani, familia yake bado haijaeleza ni siku gani hasa atazikwa.

Leave a Reply