Majenereta ya Shirika la Umeme Zanzibar
Shirika la umeme Zanzibar ZECO limesema linashindwa kuzitumia Genereta zake 32 za akiba kwa kuzalisha nishati ya umeme kila unapokatika umeme kutoka gridi ya taifa kutoakana na gharama kubwa za mafuta ya kuendesha genereta hizo.
Akizungumza na zenji fm radio afisa uhusiano wa ZECO Salum Abdalla Hassan amesema Shirika hilo  limekuwa likiwasha Genereta hizo kila siku kuanzia saa 12 jioni hadi saa nne za usiku ambapo huzalisha Megawati 10 ili kusaidia Megawati 40 kutoka Gredi ya taifa kutokana na ongezeko la mahitaji kwa wateja hasa katika nyakati hizo.
Amesema kwa sasa shirika hilo linatumia  wastani wa shilling Milioni 400 kila mwezi kuzalisha Megawati 10 kwa masaa matano kila siku…
Hata hivyo amesema kukosekana kwa huduma ya umeme leo hii kunatokana na Shirika la umeme Tanzania TANESCO Kufanya kazi zake za kawaida za usafishaji mitambo yake katika kituo cha Ras Kiromoni kabla ya umeme huo kupokelewa katika kituo cha Fumba.