Banner 468

1234453_10201664080105694_1716282793_n
Facebook

OPRAH REVEALS HER FAMILY SECRET ON HER SHOW.


Meet Oprah Winfrey's Half-Sister Patricia
Oprah Winfrey and sister Patricia
Reunion: Winfrey sits down and chats to her half-sister in front of fans on her TV talk show
She was the family secret that Oprah Winfrey called "one of the greatest surprises" of her life. 

But on Monday's 
Oprah Winfrey Show, Patricia, the media mogul's half-sister, stepped forward in a very public way. 

During the show, Winfrey revealed that she learned she had a sister last October, saying the discovery "left me speechless." 

She was 9-years-old and living with her father in Tennessee when her mother, Vernita Lee, became pregnant with a daughter, Patricia, who was given up for adoption. Born in 1963 in Milwaukee, Patricia would later live in a series of foster homes until the age of 7. She was then adopted, but said her childhood was "difficult." 

Tracing her roots took years of perseverance but Patricia finally discovered her mother – and her half-sister. 

"I received this big old package of information in the mail," Patricia said during Monday's interview. "And it has all of my birth information in it. I was like, 'Oh my God. I have a family.' " 
**************************************



OPRAH'S FAMILY HISTORY

Oprah
Oprah was born to unmarried teenagers, Vernita Lee, a housemaid, Vernon Winfrey, who was in the Armed Forces.
During her childhood was raised at various times by her grandmother Hattie Mae Lee in Mississippi, her mother in Milwaukee, and her father in Nashville.
She was raped and abused by family friends, who have not been publicly  identified, while in Milwaukee.
She moved to Nashville permanently in 1968 to live with her father while she was secretly pregnant at 14. She gave birth to a son, who died when he was just a week old.
Oprah had two half-siblings on her mother's side - Jeffrey, who died in 1989, and Patricia, who passed away in 2003.
She met her secret half-sister - who, by coincidence, is also named Patricia - in November last year.
[ Read More ]

KESI YA JERRY MURO YAZIDI ILIVYOUNGURAMA LEO

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu leo imepokea risiti ya pingu kama kielezo cha ushahidi katika kesi ya kuomba rushwa ya sh. milioni 10 inayomkabili aliyekuwa mtangazaji wa TBC 1 Jerry Muro na wenzake Edmund Kapama na Deogratius Mgasa.

Risiti ya Pingu hiyo iliwasilishwa na shahidi wa tano katika kesi hiyo ofisa mpelelezi Anthony Mwita (45), ambaye aliieleza Mahakama kuwa risiti hiyo yenye namba 341573B, aliipata katika duka la silaha la Mzinga lililoko Upanga jeshini jijini Dar es Salaam.

Alisema alifika katika duka hilo kupata uthibitisho kama pingu aliyokutwa nayo Jerry ilinunuliwa kwao ambapo nao walithibitisha kumuuzia pingu hiyo yenye thamani ya sh.25000 Mei 26, mwaka 2009 .

Mbali na kuwasilisha risiti hiyo pia shahidi huyo alidai katika upelelezi wake alienda katika Hoteli ya Seacliff ili kuthibitisha kama Jerry alifika hotelini hapo Januari 29, mwaka 2010.

Alidai alifika hotelini hapo Januari 31, mwaka jana na kumuona mlinzi wa KK Security aliyemtaja kwa jina la Brightone Babamika na kumuomba daftari la kuandikisha magari yaliyoingia hotelini hapo Januari 29 ambapo aliwapatia na kuona gari ya Jerry yenye namba za usajili T 545
TEH aina ya Cresta ambayo iliingia saa 7:33 mchana na kukabidhiwa kadi namba 673 na kuondoka saa 8:44 mchana.

Mwita alidai aliingia hotelini na kuuomba uongozi kuwaonyesha picha katika kamera ya CCTV ya matukio ya Januari 29 ambayo walionyeshwa na kupatiwa nakala ya picha hizo, lengo likiwa ni kuthibitisha kama kweli Jerry alifika hapo siku hiyo.

Naye shahidi wa nne alidai mahakamani hapo kuwa malalamikaji Michael Wage alikuja na fedha kiasi cha Sh milioni 10 kwenye ‘briefcase’ lakini hakuzihesabu.

Kesi hiyo itaendelea tena kesho mbele ya Hakimu mkazi wa Mahakama hiyo Gabriel Mirumbe.
[ Read More ]

KESI YA JERRY MURO ILIVYOUNGURAMA LEO

MHASIBU wa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo aliyesimamishwa kazi na Waziri Mkuu Mizengo Pinda kwa ubadhirifu wa fedha za Umma Michael Wage, ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa alikubali kutoa Sh milioni 10 alizoombwa na aliyekuwa mtangazaji wa shirika la Habari Tanzania (TBC1) Jerry Muro kwa kuogopa kubambikiziwa kesi kama Liyumba.

Wage, ni shahidi wa tatu katika kesi ya kuomba rushwa ya Sh milioni 10, inayomkabili Muro na wenzake Edmund Kapama na Deogratius Mgassa, walidai mahakamani hapo kuwa alitishiwa maisha na washitakiwa hao na alikiri kutoa Sh milioni moja kwa ahadi ya kumalizia nyingine tisa
kesho yake.

Akitoa ushahidi wake mbele ya Hakimu mkazi wa Mahakama hiyo Gabriel Mirumbe, alidai kuwa mfululizo wa matukio hayo ulianza Januari 28, mwaka 2010 jioni, akiwa nyumbani kwake Bagamoyo ambapo alipokea simu kutoka kwa mtu aliyejitambulisha kuwa jina la Jerry Muro na mtangazaji
wa TBC1.

Alidai Muro alimtaka kufika Dar es Salaam kwa ajili ya kufanya naye mahojiano kwamba kuna taarifa za tuhuma zinazomkabili zilizoanza kusambaa ambazo alitaka kuweka sawa ambapo alikuja na kukutana na Muro katika mgahawa wa Carlifonia kama walivyoahidiana ambapo baada ya kukutana Muro alimwambia alikua akiandaa kipindi kuhusiana na tuhuma zake ambapo alimtaka waende katika Hoteli ya Seacliff ambako mahojiano hayo yangefanyika.

Alidai wakiwa njiani kwenye gari ya Muro kuelekea Seacliff Muro alimpigia mtu simu na katika maongezi yake alimtaja yeye (Wage) na alipokata simu alimuuliza alikuwa akiongea na nani, Muro akamjibu kuwa huyo ni Kaimu Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) ambaye pia alikuwa na maongezi na yeye.

Wakiwa bado njiani Wage alidai kuwa Muro alimwambia kuwa yeye ni Ofisa wa jeshi, ana nyota tatu na amesomea Marekani, ambapo alifungua ‘dashboard’ ya gari akatoa pingu na kumwambia kama akifanya vurugu au fujo ya aina yoyote angemfunga pingu na kisha alitoa bastola yenye
kitako cha rangi ya damu ya mzee na kumwambia kama yote yangeshindikana basi angempiga risasi na kumuua.

Alidai walipofika Seacliff walipokelewa na mtu mmoja mrefu, mweupe na mnene aliyejitambulisha kuwa yeye ni Kaimu mkurugenzi wa TAKUKURU anaitwa Mussa na baada ya muda akaja mwingine aliyejitambulisha kuwa ni msaidizi wa Kaimu Mkurugenzi wa TAKUKURU.

Wakiwa wamekaa meza moja Kaimu Mkurugenzi akamwambia kuwa ana tuhuma za ufisadi na kwamba hajafikishwa mahakamani aseme kama atahitaji msaada wao ambapo aliwajibu kuwa yeye sio fisadi.

Wage alidai Kaimu Mkurugenzi alimwambia kuwa hata Liyumba hakufanya kosa bali alimuambukiza Ukimwi bibi wa jamaa yake ambaye wanafanya naye kazi.

Alidai baada ya maelezo hayo alimuomba Muro amsaidie ambapo alimuomba atoe Sh milioni 10, naye akawajibu hakuwa nayo pale alikuwa na Sh. milioni moja tu, na hizo nyingine angekwenda kuwatafutia na kuziwasilisha kesho yake.

Alieleza akiwa na watu hao aliamua kumpigia mke wake aliyekuwa Morogoro simu na kuweka kipaza sauti ambapo alimtaka kumletea Sh. milioni tisa kesho, mkewe huyo alidai asingeweza kupata milioni tisa kwa kesho badala yake angeleta milioni nne tu.

Alidai kutokana na matukio ya siku hiyo aliwapigia simu ndugu zake ambao walimshauri kuripoti polisi ambapo kesho yake alienda kuripoti katika kituo cha polisi kati jijini Dar es Salaam, ambapo walimwambia ampigie simu Muro amwambie wakutane katika mgahawa wa City Garden maeneo ya Posta mpya mkabala na klabu ya Billicanas.

Wage alidai alimpigia simu Muro na kukubaliana kukutana hapo ambapo alifika saa 4:30 asubuhi na kumpigia simu kumfahamisha kama ameshafika na ndipo akajitokeza akiwa na polisi waliovalia kiraia ambapo Muro alipowatambua akataka kukimbia lakini polisi wakalizuia gari lake.

Shahidi huyo aliwatambua washitakiwa hao mahakamani na pingu, bastola na miwani ambavyo viliwasilishwa na upande wa mashitaka kama utambulisho katika kesi hiyo. Shauri litaendelea kusikilizwa tena leo kwa mashahidi upande wa mashitaka kuendelea kutoa ushahidi wao.
[ Read More ]

MFUNGWA KUTOKA URUSI AFARIKI ZANZIBAR CHUO CHA MAFUNZO


RAIA mmoja wa Russia, aliyekuwa akitumikia kifungo cha maisha katika Chuo cha Mafunzo Zanzibar amefariki dunia.

Inarserger Othirov, amefariki dunia Januari 9, mwaka huu katika Hospitali Kuu ya Mnazimmoja ambapo alikuwa amelazwa katika hospitali hiyo akipatiwa matibabu.

Kwa mujibu wa taarifa za Daktari kutoka Hospitali hiyo ya Mnazimmoja, marehemu alikuwa akisumbuliwa na maradhi ya homa, kifua kikuu (TB), pamoja na uvimbe uliojaa maji katika pafu lake la upande wa kulia.

Staff Ofisa wa Vyuo vya Mafunzo, Makao Makuu Kilimani wilaya ya Mjini Unguja, Makame Kombo Ame, alithibitisha kutokea kifo cha mwanafunzi huyo wa Chuo cha Mafunzo.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi huko ofisini kwake, Staff Ofisa huyo, huyo alisema kuwa, marehemu amefariki siku tisa mara baada ya kufikishwa hospitalini hapo kwa matibabu.

Alisema kuwa, kabla ya kifo chake Ivan Ochirov kama jina lake la umaarufu alilokuwa akijulikana nalo Chuoni humo, alikuwa akipatiwa matibabu katika hospitali ya Chuoni humo, lakini baadae alilazimika kupelekwa Hospitali Kuu ya Mnazimmoja baada ya hali yake kuwa mbaya.

Akiwa hospitalini hapo kwa matibabu, Januari 9 mwaka huu majira ya saa 12:15 za asubuhi Ivan alifariki dunia, kwa mujibu wa Staff Ofisa huyo.

Alifahamisha kuwa, mara baada ya kifo hicho mwili wake ulikabidhiwa wazee wake wote wawili waliokuwepo hapa nchini, chini ya usimamizi wa Balozi wa Russia nchini Tanzania kwa taratibu za mazishi.

Kwa mujibu wa Staff Ofisa huyo, mazishi ya marehemu huyo yalifanyika Zanzibar saa nane mchana, katika ufukwe wa pwani ya Migombani ngazi mia, kwa kuuchoma moto mwili wa marehemu huyo.

Ivan alikuwa ni mmoja kati ya wanafunzi wawili wanaotumikia kifungo cha maisha Chuo hicho cha Mafunzo, baada ya kupatikana na hatia ya kumuua kwa makusudi kijana mwenzao raia wa Russia kwa kumchoma moto, tukio ambalo lilitokea Zanzibar mwaka 1998.

Kabla ya adhabu hiyo, Ivan na mwenzake huyo (jina halikupatikana), ambaye naye pia ni raia wa Russia, Mei 31, 2001 walihukumiwa kutumikia Chuo hicho kwa muda wa miaka 15, baada ya kupatikana na hatia ya kuua bila ya kukusudia katika kesi ya jinai namba 14/1998 iliyokuwa ikiwakabili Mahakama Kuu ya Zanzibar.

Lakini hata hivyo, Aprili 23, 2004 jopo la Majaji wa Mahakama ya Rufaa Tanzania, ilitengua adhabu hiyo na kuwahukumu kunyongwa hadi kufa, baada ya kuonekana kuwa wameua kwa makusudi.

Adhabu hiyo imetolewa baada ya kushindwa kwa rufaa yao waliyoiwasilisha mahakamani hapo, kwa kupinga adhabu hiyo ya miaka 15 Chuo cha Mafunzo iliyotolewa na Mahakama Kuu ya Zanzibar.

Hata hivyo, aliyekuwa Rais wa Zanzibar kwa wakati huo Dk. Amani Abeid Karume, Novemba 12, 2002 aliwapatia msamaha kutoka adhabu hiyo ya kunyongwa hadi kifungo cha maisha.

Kwa mujibu wa Staff Ofisa huyo, pamoja na kutumikia kifungo cha maisha Chuoni hapo, hali ya mwanafunzi mwenzake bado inaendelea vizuri.
[ Read More ]

WEWE NI MWANAMKE/MSICHANA NA UNAENDESHA GARI,UNAPASWA KUJUA YAFUATAYO....


Sasa hivi wanawake/wasichana wengi ni madereva...wanaendesha magari sana tu tofauti na ilivyokuwa zamani ambapo wanaume ndio walikuwa wengi wana magari na wanaendesha magari.
Wanawake sisi tumeshajiwekea kichwani kwamba sisi tunaendesha tu gari na kazi yetu ni kuweka mafuta tu kwenye gari(petrol/deasel) basi.Au kuhakikisha gari safi lakini mengine ni kazi ya wanaume...sio kweli kuna vitu ambavyo unapaswa kuvifaham kuhusu magari.
Kubadili Tyre
unaweza kuwa sehemu ambayo hakuna hata mtu wa kuku saidia halafu tyre imepata pancha.Kwenye gari una jeki,spana na spair tyre lakini kubadilisha Tyre huwezi.Jifunze hili wala sio kazi mimi sio dereva lakini nimeshawahi kutoa tyre na kuweka tyre inasaidia sana hata gari ikikuhabibikia mahali unakuwa huna wasiwasi na kuanza kusumbua watu.
Kuweka maji ya wiper
Wakati mwingine vioo vimepata uchafu,vumbi,kioo kimenyewa na ndege,...unataka kusafisha lakini hakuna maji ya kwenye wiper na wala hujui yanawekwaje.Unapaswa kujua hili ni kwa manufaa yako mwenyewe binafsi.
Pia unapaswa kujua kuweka oil kwenye gari lako na hata namna ya kuicheki kabla hujaweka.
Break down
Gari inaweza kupata tatizo ikashindwa kuwaka kabisa,kuwa na namba za watu wa break down kabisaa ili kikinuka basi unapiga simu ili uje kutolewa hapo ulipoharibikiwa na gari.

Hivi ni baadhi na muhimu uavyoweza kujua ili hata jambo likitokea basi huna wasiwasi kivile kisa hujui pa kuanzia.

source dina marios
[ Read More ]

PINDA AKUTANA NA BARAZA LA MAWAZIRI LEO



Waziri Mkuu Mh Mizengo Pinda leo amekuwa na mkutano na Baraza la Mawaziri la Kazi linao jumuisha mawaziriri na manaibu Waziriri ofisini kwake mtaa wa Magogoni Jijini Dar

[ Read More ]

MISS PROGRESS INTERNATIONAL ATEMBELEA WALEMAVU WA NGOZI SHINYANGA LEO


Mkurugenzi wa kampuni ya One Touch Solutions, Peter Mwendapole akiwa na watoto wa wenye ulemavu wa ngozi wanaosoma na kulelewa katika shule ya Buhangija mkoani Shinyanga.
Mkurugenzi wa kampuni ya One Touch Solutions Bw. Peter Mwendapole na Miss Progress International Julieth William Lugemba na wenyeji wao wenye ulemavu wa ngozi wanaosoma na kulelewa katika shule ya Buhangija mkoani Shinyanga.
Miss Progress International, Julieth William Lugembe akiwa na watoto wanaolelewa kwenye kituo cha Buhangija kilichopo mkoani Shinyanga wakati alipofanya ziara mkoani humu kuangalia matatizo mbalimbali yanayowakabili albino.

MSHINDI wa dunia taji la Miss Progress International Julieth William, leo ametembelea watu wenye ulemavu wa ngozi Mkoani Shinyanga.
Julieth alitembelea watu hao na watoto wenye ulemavu huo wa ngozi kwa lengo la kutaka kufahamu mahitaji yao kabla ya kuweza kuwasaidia.
Ziara hiyo iliyoandaliwa na kampuni ya One Touch Solutions inayoandaa shindano la Miss Progress Tanzania ilimedhaminiwa na Precision Air na kampuni ya simu za mkononi ya Airtel
Mlimbwende huyo aliyetwaa taji hilo mwaka jana nchini Italia alianza kwa kutembelea shule ya Buhangija, ambayo inatunza watoto wenye ulemavu huo.
Akiwa katika shule hiyo alipata fursa ya kutanzama mazingira ya shule hiyo pamoja na kuzungumza na watoto hao kwa muda wa dakika 30.
Katika moja ya mahitaji waliyotaka watoto hao ni kumaliziwa kwa moja ya bweni lao ambalo halijamalizika ili kuweza kupata nafasi nzuri ya kulala kutokana na lile wanalotumia kuwa dogo, jambo linalowafanya walale kitanda kimoja watu watatu.
Baadaye alitembelea ofisi za mkoa za Chama cha Maalbino (TAS) na kuweza kuzungumza na watu wazima ili nao kutaja mahitaji yao.
Katika kikao hicho watu hao wenye ulemavu walitaja mahitaji yao ikiwaa ni pamoja na kutaka kupewa elimu ya ujasiliamali ili waweze kuendesha maisha yao na kuondokana na utegemezi.
Pia alikutana na Ofisa Elimu wa mkoa wa Shinyanga, Eva Lopa, Ofisa Ustawi wa Jamii, Jesca Kagunila. Leo Julieth atakuwa mkoani Mwanza kabla kuelekea Arusha.

[ Read More ]

TANZANIA MITINDO HOUSE WANUNUA GARI WALIOCHANGIWA KWENYE RED RIBBON FASHION GALA





 Watoto wa Tanzania Mitindo House wanashukuru wadau wote waliochangia kwa hali na mali kufanikisha usafiri wao.
[ Read More ]

Happy 47th Birthday Michelle Obama


Today our First Lady Michelle Obama celebrates her 47th birthday. We've loved watching this Chicago native ever since she hit the world's stage alongside her husband, President Barack Obama. Since then she has awakened within all of us a sense of pride in being Black women.There's no question that Michelle Obama is a First Lady with style.Ilove her sense of fashion age apropriate.She and her family marked the occasion by paying tribute to MLK with a painting project at a school on Capitol Hill.
[ Read More ]