Banner 468

1234453_10201664080105694_1716282793_n
Facebook

MAKAMU WA RAIS MGENI RASMI SALA YA EID EL FITRI KITAIFA MSIKITI WA AL-FAROUK JIJINI DAR



Makamu wa rais wa jamhuri ya muungano akisoma hotuba baada ya sala ya eid fitri

 Kaimu Mufti mkuu wa Tanzania Sheikh Ally Muhidin Mkoyogore. akiwasalisha waumuni wa dini ya kiisalamu sala ya eid-el-fitri













[ Read More ]

Masheikh: Bora tukose misaada kuliko ushoga


Makamu wa Rais Dk. Gharib Bilali (wapili kulia) akifuatgilia hotuba ya sala ya Eid El-haji iliyosaliwa kwenye msikiti wa Alfaruq Bakwata Kinondoni jijini Dar es Salaam jana.kulia ni Ahmed Abdallah Sambi aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Komoro. Kushoto ni Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Alhadi Musa Salim na Kaimu Mufti wa Tanzania Sheikh Ally Muhidin Mkoyogore.

MASHEIKH nchini wamesema ni bora Watanzania wakakosa misaada yote kutoka Serikali ya Uingereza kuliko kusujudia shinikizo lilitolewa na kiongozi wake kutaka kuruhusu sheria inayotambua mashoga na kuhalalisha ndoa za jinsi moja.


Msimamo huo wa masheikh umekuja siku chache baada ya Waziri Mkuu wa Uingereza, David Cameron kutamka kwamba nchi yake ina mpango wa kusitisha misaada yake kwa nchi ambazo sheria na katiba zao, hazitambui mashoga na ndoa za jinsi moja.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti kwenye ibada ya Eid El Hajj masheikh hao waliwataka Waislamu kuungana na kupinga kwa nguvu zote udhalimu huo ili dunia ifahamu kwamba Waislamu na Watanzania hawako tayari kuona Mungu akichezewa.


Akitoa hotuba ya Idd katika swala iliyofanyika kitaifa kwenye Msikiti wa Al-Farouk yalipo Makao Makuu ya Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata), Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Musa Salum alisema haiwezekani dini ya Mwenyezi Mungu ikachezewa kwa maslahi ya watu wachache.




Alizipongeza serikali zote mbili, ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kwa kutoa msimamo thabiti dhidi ya matamko yaliyotolewa na Cameron aliyenukuliwa na vyombo vya habari akisisitiza kwamba nchi zitakazoshindwa kufuata agizo hilo zitanyimwa misaada.
“Bila shaka mmesikia vyombo vya habari vikimnukuu Cameron  akiweka shinikizo kwa nchi zitakazowanyima uhuru mashoga na ndoa za jinsi moja atasitisha misaada, huku ni kuupinga Uislamu na hili hatuwezi kukubali,” alisema Sheikh Salum.


Alisema ni heri Watanzania wafe kuliko kuridhia masharti ya mabwana wakubwa wanaotaka kuangamiza ulimwengu kwa ajili ya matakwa yao binafsi yasiyoendana na maadili ya dini ya Mwenyezi Mungu.


Kwa upande wake, Kaimu Mufti wa Tanzania, Sheikh Ali Muhidin Mpoyogole alisema kama hakuna uadilifu kutoka kwa viongozi, amani ya nchi haiwezi kuwa ya kudumu. Aliwataka Waislamu kudumisha amani kwa kuzingatia maadili ya dini.


“Bila ya kuwa na haki na uadilifu hakutakuwa na amani nchini kwani mambo haya mawili yanafungamana na bila shaka ndiyo yaliyokuwa yametufungamanisha nchini, lakini katika siku za hivi karibuni bahati mbaya mambo haya yanaanza kuwa adimu nawaombeni tuyadumishe,” alisema.
Akizizungumza katika ibada hiyo, Makamu wa Rais, Dk Mohammed Gharib Bilal aliwapongeza Waislamu kwa kudumisha udugu na umoja na akawapongeza kwa kuratibu vyema safari za Hijja tofauti na ilivyokuwa siku za nyuma.


“Mwaka huu naona safari za Hijja hazikuwa na matatizo makubwa na niwapongezeni kwa hatua hiyo... lakini pia niwatie shime tujitahidi kuongeza elimu yetu kwa kujenga shule zaidi na kuwapeleka watoto wetu shule ili kusudi waje kuwa jamii bora baadaye,” alisema.


Alisisitiza umuhimu wa wananchi kushirikiana na kuondokana na udini na ukabila ambao umeanza kuchipuka kwa kasi nchini.“Tuzidi kuliombea taifa letu libakie na mshikamano tuliokuwa nao kwani mataifa mengi duniani yanalilia amani na yanatuchukulia sisi kama mfano. Tusije tukabweteka, amani yetu tukaiweka rehani,” alisema Dk Bilal.


Akizungumza katika ibada ya Idd El Hajj iliyofanyika katika Viwanja vya Tangamano jijini Tanga, Naibu Mudir wa Taasisi ya Ansar Sunna, Sheikh Salimu Bafadhil aliwaonya Waislamu kutowategemea wanasiasa akisema watapambana kupinga udhalili unaotaka kufanywa na wafadhili wanaotaka kuhalalisha ndoa za jinsi moja.


Sheikh huyo alisema shinikizo hilo la Cameron ni matokeo ya watawala wa nchi maskini kama Tanzania kushindwa kutumia kikamilifu rasilimali zilizopo na kuziacha zikitoroshwa nje nazo kubaki kuwa tegemezi kwa kila kitu kutoka nchi zinazojiita wafadhili.
Alisema ikiwa Waislamu watakaa kimya na kutegemea kuwa wanasiasa watawapigania katika hili, watambue kuwa watakuwa na la kujibu kwa Mwenyezi Mungu.


“Ufisadi na ubinafsi wa baadhi ya wanasiasa umetufikisha hapa, Tanzania si maskini kiasi cha kutegemea kila kitu kwa wafadhili ambao wanatuletea sasa mashinikizo ambayo ni kinyume cha ubinadamu,” alisema Sheikh Bafadhil.


Alieleza kushangazwa kwake na haki za binadamu zinazoelezwa na kutolea mfano wa aliyekuwa Kiongozi wa Libya, Muammar Gaddafi ambaye aliuawa na mwili wake kuwekwa hadharani kwa siku tano bila yeyote kukemea.
“Haki za binadamu ni kuruhusu ushoga, lakini Gaddafi aliuawa kinyama na madhalimu wa nchi za Magharibi na kuwekwa kwenye bucha kwa siku tano hilo halikuonekana,” alisema Bafadhil.


Sheikh atoa wito
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Alhaj Dk Ali Mohamed Shein ametoa wito kwa kila kiongozi kuheshimu dhamana yake kwa kuwajali walio chini yake pamoja na wale wote anaowahudumia.
Aisha, amewaonya wafanyakazi ambao huwatolea maneno yasioridhisha watu wanaowahudumia jambo ambalo alisema linawavunja moyo wananchi na kuilaumu Serikali yao.


Alhaj Dk Shein aliyasema hayo jana katika hotuba aliyoitoa kwenye Baraza la Idd, katika Ukumbi wa Baraza la Wawakilishi, Wete Kisiwani Pemba na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa vyama na serikali akiwamo Makamu wa Kwanza wa Rais, Maalim Seif Sharif Hamad, Jaji Mkuu wa Zanzibar, Omar Makungu, Kadhi Mkuu, Sheikh Khamis Haji Khamis, Mama Mwanamwema Shein na Mama Fatma Karume.


Dk Shein alisema nidhamu ina umuhimu mkubwa katika maisha ya kila mwanadamu na hayo ni miongoni mwa mafunzo ya Ibada ya Hijja na kusisitiza kuwa ufanisi na utoaji wa huduma katika taasisi za hapa nchini hutegemea hilo.


“Watoa huduma za aina zote lazima waongozwe na nidhamu katika kuwahudumia watu..... tukumbuke kwamba kila binadamu anastahiki heshima. Nidhamu katika sehemu ya kazi itafanikisha  lengo la Serikali la kuwa na utumishi bora ambao utaongeza ufanisi,” alisema.


Alhaj Dk Shein alieleza kuwa  maendeleo ya nchi hayawezi  kupatikana bila ya wananchi wake kuwa na umoja na mshikamano akisisitiza kuwa ni wajibu wa kila mwananchi kujua kuwa analo jukumu la kuchangia maendeleo ya nchi katika nafasi yake.


Akizungumzia Ibada ya Hijja, Dk Shein alisema ni jambo la kutia moyo kuona idadi ya mahujaji wa Tanzania inaongezeka kila mwaka sambamba na taasisi zinazoshughulikia kuwasafirisha. Hata hivyo, alisema inasikitisha kusikia kuwa baadhi ya mahujaji hupata usumbufu wa kutekeleza ibada hiyo kutokana na huduma zisizoridhisha za baadhi ya taasisi.


Dk Shein alisema Ibada ya Hijja ambayo hufanywa mara moja kwa mwaka ni Nguzo ya Tano ya Uislamu ambayo kuitekeleza, siyo tu kutii amri ya Allah, bali pia ni kusimamisha Uislamu.


Alisema kitendo cha Mwislamu kukubali kutumia sehemu ya mali yake, kuacha familia yake, ndugu na marafiki, akafunga safari hadi Nyumba Tukufu ya Makka kuitikia wito wa Mola wake ni kitendo cha utii.


Mapema asubuhi, Dk Shein aliungana na wananchi, viongozi na waumini mbalimbali wa dini ya Kiislamu katika swala ya Idd El Hajj, kwenye Uwanja vya Gombani, ChakeChake.
[ Read More ]

REAL VIDEO of Muammar Qaddafi/Gaddafi Captured and Alive Before Death

[ Read More ]

KIFO CHA ALIEKUA KIONGOZI WA LIBYA.KANAL MUAMMAR GADDAFI





ALIYEKUWA kiongozi wa Libya, Kanali Muammar Gaddafi ameripotiwa kuuawa na wapiganaji wanaoongozwa na Baraza la Mpito nchini humo (NTC), baada ya mji wa nyumbani kwake, Sirte kunyakuliwa na vikosi hivyo jana.

Kifo cha Kanali Gaddafi (69) kilitangazwa rasmi na Waziri Mkuu wa Serikali ya mpito nchini humo, Mahmoud Jibril, muda mfupi baada kiongozi huyo aliyeitawala Libya kwa miaka 42 kuuawa.

Awali, msemaji wa NTC nchini Libya, Kanali Ahmed Bani alisema Kanali Gaddafi aliuawa na mwili wake ulipelekwa katika mji wa Misratah, bila kutoa ufafanuzi kamili kuhusu mazingira ya kifo hicho.

Taarifa za kuuawa kwake zilitolewa huku zikiambatanishwa na picha zinazoonyesha sura inayoonekana kuwa ni ya kiongozi huyo, katika muonekano wa nywele zake laini na ndefu wastani na uso uliotapakaa damu na majeraha.

Kanali Gaddafi anakuwa kiongozi wa kwanza kuuawa tangu kuanza vuguvugu la mageuzi katika mataifa ya kiarabu mwanzoni mwa mwaka huu, yaliyowaondoa madarakani Rais Ben Ali wa Tunisia na Hosni Mubarak wa Misri.

Kifo hicho kimetangazwa ikiwa ni miezi tisa tangu kuanza kwa upinzani mkali dhidi ya Serikali yake Februari mwaka huu, ambapo aliapa kwamba asingeondoka nchini Libya na kwamba yeye na wafuasi wake wangepambana hadi tone la mwisho la damu.

Kanali Gaddafi ambaye wakati wa utawala wake aliwahi kujipa wadhifa wa “mfalme wa wafalme wa Afrika” alikuwa akisifika kwa ukali wa sauti yake na maneno makali ya kuhamasisha na kueleza misimamo yake katika hotuba zake.

Mapambano hayo yameishia katika mji wa nyumbani kwake, Sirte ambao umekuwa na upinzani mkali kwa vikosi vya wapiganaji wa NTC ambavyo vililazimika kupambana kwa miezi kadhaa hadi waasi walipofanikiwa kuuteka jana.

Kanali Bani alisema mtoto wa Kanali Gaddafi, Mutassim ambaye walikuwa pamoja katika mji wa Sirte aliuawa na wapiganaji hao wa NTC.

Msemaji huyo aliwaambia waandishi wa habari kuwa kiongozi huyo alifariki dunia baada ya kujeruhiwa vibaya katika miguu yake yote na kichwani.

“Aliuawa katika mapambano na wapiganaji wetu. Kuna picha zinazoonyesha hayo,”alisema.

Alijificha kwenye karavati

Kwa mujibu wa taarifa za vyombo mbalimbali vya habari vya kimataifa, Kanali Gaddafi alidhibitiwa baada ya kukutwa  amejificha katika karavati la barabarani, yeye pamoja na baadhi ya walinzi wake.

Kwa upande wake, kamanda wa wapiganaji wa baraza hilo, Abdul Hakim Belhaj pia alithibitisha kuwa Kanali Gaddafi alifariki dunia kutokana na majeraha aliyoyapata baada ya kukamatwa.

Makamu Mwenyekiti wa NTC, Abdul Hafiz Ghoga alithibitisha mbele ya waandishi wa habari kuwa Gaddafi aliuawa katika mji wa Sirte.

“Tunatangaza kwa dunia kuwa Muammar Gaddafi aliuawa katika mikono ya wanamapinduzi,” alisema Ghoga.

Katika mtiririko wa matukio yaliyokuwa yakirushwa katika vituo mbalimbali vya televisheni, kituo cha televisheni cha al-Jazeera kilionyesha picha za mwili wa Kanali Gaddafi ukiburuzwa katika eneo alilouawa.

Filamu za video zilizochukuliwa kwa simu za mkono zilionyesha kile kilichoonekana kuwa maiti ya Gaddafi iliyolowa damu. Mwili wake baadaye uliburuzwa na wapiganaji na kupakiwa nyuma ya gari aina ya pick-up.

Nato na Marekani zilieleza kuwa haziwezi kuthibitisha taarifa za kuuwawa kwa kiongozi huyo ambaye hajaonekana tangu NTC ilipoikamata Tripoli.

Watu washangilia mitaani

Wakati huohuo, katika mji wa  Benghazi na miji mingine nchini humo, watu walionekana kukusanyika mitaani na kushangilia taarifa hizo za kuuawa kwa Gaddafi.

Viongozi mbalimbali duniani pia wamezungumzia kuhusu taarifa hizo za kuuawa kwa Kanali Gaddafi ambaye amewahi kuwa mpinzani mkubwa wa mataifa ya Ulaya na Marekani kutokana na misimamo yake dhidi ya mataifa hayo.

Miongoni mwa viongozi hao ni Waziri Mkuu wa Uingereza, David Cameroon ambaye alisema ni siku maalum ya kukumbuka maovu yote yaliyofanywa na Gaddafi.

Alisema watu wa Libya wako katika nafasi nzuri ya kujenga nchi imara na yenye demokrasia.

“Ninafurahi kazi ambayo Uingereza imesaidia katika kuuondoa utawala wa Gaddafi,”alisema.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Ufaransa, Alain Juppe amepongeza kufikiwa mwisho kwa utawala wa miaka 42 ya Gaddafi.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-Moon pia alisema kwamba kifo cha Kanali Gaddafi kinatoa mwanya wa “historia mpya kwa Libya”.

“Watu wanatakiwa watambue kuwa huu ni mwisho wa mwanzo. Sasa ni wakati wa Walibya wote kushikamana na kuwa kitu kimoja. Ni wakati wa kuponya majeraha na kujenga upya taifa. Si wakati wa visasi,” alisema Ki-Moon.

Balozi wa Libya nchini Uingereza, Mahmud Nacua alisema kuwa kuawa kwa Gaddafi kunamaanisha Libya inaelekea kwenye mustakhabali bora wa baadaye.

Wasifu wa Kanali Muammar Gaddafi

Alikuwa mtoto wa wafugaji wa Kibedui, mwenye maisha ya utata, lakini ambaye alitukuzwa sana, huku mataifa ya Magharibi yakimuona mtu wa hatari wakati wote.

Muammar Muhammad Gaddafi aliitawala Libya kwa zaidi ya miaka 40. Hadi mwanzoni mwa Machi 2011, alikuwa akiamini ndani ya moyo wake kwamba watu wake walikuwa wakimpenda na kwamba walikuwa tayari kumlinda hadi kufa kwa ajili yake.

Lakini wakati huo, tayari Gaddafi alikuwa ameshatumia njia za kikatili kuyazima maandamano dhidi yake, maandamano ambayo baadaye yaligeuka vita vya wenyewe kwa wenyewe.

Kwa mujibu wa taarifa, watu zaidi ya 30,000 waliuawa kwenye vita hivyo. Mara nyingi sana, Gaddafi alitoa matamko makali wakati wa vita hivyo, ila linalojuilikana zaidi ni lile la kuwaita wapinzani wake kuwa ni panya.

Kwa kila hali, yaliyotokea ni mambo ambayo Gaddafi hakuyatarajia asilani. Mtoto huyu wa wafugaji wa Kibedui aliyezaliwa mwaka 1942, alikuja kuibuka kama mkombozi wa Walibya, alipompindua Mfalme Idriss hapo mwaka 1969.

Kuanzia hapo akaanza kujenga kile alichokiona mwenyewe kuwa ni mfumo wa kidemokrasia wa moja kwa moja. Alianzisha kamati za umma zilizoamua juu ya mustakabali wa umma na wa Serikali. Aliuita mfumo wake wa kisiasa na kiuchumi kuwa ni wa kisoshalisti, alioufafanua kwenye kijitabu chake cha Kijani.

Historia yake kiufupi

Alizaliwa mwaka 1942 katika eneo la Jangwa, kwenye mji wa Sirte, katika familia ya baba Mohamed Abdulsalama Abuminiar na mama Aisha Ben Niran. Alijiunga na Jeshi la Libya  mwaka 1965.
Alifanya mapinduzi ya Serikali yasiyo ya umwagaji damu na kumuondoa mfalme Idris katika utawala wake mwaka 1969 na kuwa mtawala wa Libya akiwa na umri wa miaka 27.

Alikuwa maarufu kwa nguo anazopenda kuvaa na walinzi wa kike wenye kubeba silaha, kiongozi huyo wa Libya pia anadhaniwa kuwa na mbinu nzuri za kisiasa kwa kuweza kuirejesha Libya kutokana na kutengwa kidiplomasia duniani.

Baada ya miongo miwili ya kutengwa katika jamii ya kimataifa, mwaka 2003, Tripoli ilikiri kuwa walifanya shambulio la Lockerbie kwa kuiangamiza kwa mabomu ndege ya Pam Am. Umoja wa Mataifa (UN) ulikubali kuondoa vikwazo dhidi ya Libya.

Baada ya miezi kadhaa, Serikali ya Kanali Gaddafi ilisitisha mipango yake ya kuunda silaha za maangamizi na hii ikarejesha ushirikiano na nchi za Magharibi.

Gaddafi ni mtu wa kipekee katika kauli zake, mienendo yake, tabia zake na mikakati yake, kwa mujibu wa Saas Djebbar, mtaalam wa siasa za Libya.
Alipokuwa kijana alivutiwa na kiongozi mzalendo wa Misri, Gamal Abdel Nasser, alipokuwa akishiriki katika maandamano dhidi ya Israel wakati wa mtafaruku wa Suez mwaka 1956.

Alipanga njama ya kupindua utawala wa kifalme alipokuwa mwanafunzi wa kijeshi alipokuwa mafunzoni Uingereza kabla ya kurejea nyumbani Libya. Alipanga mapinduzi ya Septemba 1, 1969 akiwa katika mji wa Benghazi.

Alianza kujenga itikadi zake za kisiasa mwaka 1970 na kuziandika katika kitabu chake cha kijani kibichi.
Alikitumia kitabu chake kuanzisha mfumo wa kisiasa uliojumuisha kanuni za Kiislamu na mfumo ulio tofauti na siasa za ujamaa au ubepari.

Mwaka1977 aliasisi mfumo ujulikanao kama 'Jamahiriya' au 'Taifa la Umma' ambapo raia ndio wanaoendesha uongozi wa nchi yao kupitia 'kamati za umma'.

Mfumo huo wa Gaddafi umevuka mipaka na hauhusishi mambo ya siasa tu, bali pia mambo mengine.
Akiwa safarini ng'ambo, alikuwa akitumia makazi maalum kwenye kambi iliyojengwa na hema yake ya kifahari ya Kibeduwi akiwa amefuatana na walinzi wanawake ambao, inasemekana, huwa hawapotezi umakini kazini kama walinzi wanaume.Hema hiyo pia ilitumiwa kuwalaki wageni wa Libya na Kanali Gaddafi huendesha mikutano na mahojiano yake humo humo akipepea usinga au tawi la mitende.

Rais wa zamani wa Marekani Ronald Reagan alimwita Gaddafi 'mad dog' yaani 'mbwa kichaa' na Marekani ililipiza kisasi dhidi ya Libya kwa madai ya kuhusika na mashambulio ya anga barani Ulaya kwa kuvamia miji ya Tripoli na Benghazi mwaka 1986.Aliposhindwa katika jitihada zake za kuzipatanisha nchi za Uarabuni katika miaka ya 90, Kanali Gaddafi alielekeza nguvu zake barani Afrika na kupendekeza 'Muungano wa Nchi' za bara la Afrika.

Alianza kuvaa mavazi yake binafsi, sare za michezo zilizo na ngao za Bara la Afrika au picha za viongozi kutoka bara hilo.Aliwahi kuvunja na kufuta Wizara za nchi hiyo pamoja na bajeti zao, isipokuwa Wizara chache ikiwemo ya Ulinzi, Fedha na Mambo ya Nje.Licha ya uchumi wa Libya kutoa fursa kwa wawekezaji wa nje, mabadiliko bado yanakwenda taratibu.

Vuguvugu la mageuzi dhidi yake lilipoanza mwanzoni mwa mwaka huu, aliapa kuwafuata wanaompinga nyumba hadi nyumba, mlango kwa mlango, hatua iliyoibua hasira na kuchochea harakati za kijeshi dhidi yake.

Baada ya baadhi ya askari kutangaza kujitoa katika jeshi lake na kuanzisha uasi, aliapa kwamba atapambana hadi tone la mwisho la damu litakapomwagika. Alisisitiza kwamba kamwe hatakimbia kutoka katika ardhi ya Libya, atafia katika ardhi ya mababu zake.

Taarifa zilieleza jana kwamba aliuawa baada ya kukutwa akiwa amejificha katika daraja dogo kwa ajili ya kupitisha maji barabarani (karavati).

Mara baada ya kuuawa, wapiganaji wa Baraza la Mpito waliokuwa katika mapambano dhidi yake walibaini kwamba alikuwa na bastola iliyotengenezwa kwa dhahabu tupu.

[ Read More ]

MAULID HAMAD MAULID AFARIKI DUNIA LEO

Hayati Maulid Hamad Maulid enzi za uhai wake

CHAMA Cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (Taswa), kinasikitika kutangaza kifo cha mwandishi mahiri wa habari za michezo Zanzibar, Maulid Hamad Maulid.

Maulid ambaye anafanyia kazi vituo vya Redio One na ITV akiwa Zanzibar, amefariki dunia leo Jumanne Oktoba 18, 2011 asubuhi nyumbani kwake Jang’ombe Zanzibar.

Taswa imepokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya kifo cha Maulid kwani alikuwa kiungo muhimu kwa ushirikiano kati ya Taswa na waandishi wa habari za michezo Zanzibar.

Pia Maulid alikuwa Makamu Mwenyekiti wa Taswa Zanzibar ambayo ilianzishwa hivi karibuni kwa lengo la kuwaweka pamoja waandishi wa habari za michezo Zanzibar.

Tumepoteza mtu muhimu, mpiganaji mahiri katika mambo ya michezo ambaye daima Taswa tutaendelea kumkumbuka.

Tunaipa pole familia yake, Taswa Zanzibar na wanamichezo wengine weote kutokana na msiba huo mkubwa na tupo nao katika kipindi hiki kigumu.

Wakati wa uhai wake Maulid licha ya kuwa kiongozi wa timu mbalimbali ikiwemo kuwa Rais wa timu ya Taifa Jang’ombe iliyopata kushiriki Ligi Kuu Zanzibar, pia amepata kuchezea timu ya Kikwajuni ya Zanzibar.

Pia amepata kuwa msemaji wa Chama cha Soka Zanzibar(ZFA) kabla ya kujiondoa baada ya uchaguzi wa chama hicho mwaka jana.

Kulingana na taarifa ambazo Taswa imezipata kutoka kwa Katibu wa Taswa Zanzibar, Donisya Thomas ni kuwa taratibu za maziko zilikuwa zikiendelea na kuna uwezekano mkubwa akazikwa leo alasiri. Mungu aiweke mahali pema peponi roho ya Maulid Hamad Maulid.Amin

Nawasilisha.

Amir Mhando
Katibu Mkuu Taswa
18/10/2011.
[ Read More ]

MH. KIKWETE AND 50-CENT US


[ Read More ]

JOKE OF THE DAY..



 A tourist asked a boat Guy do u know biology,physiology,geology,psychology and criminology?The boat guy said No........The tourist then said damn, what the hell do u know on the face of this earth you will die illiteracy!!

After a while a boat started sinking' then a boat guy asked the tourist Do you know swimology and escapology from crocodology? The tourist answer No........the boat guy said well you will drownology and crocodilogy will eat your assology and you will dieology because of your badmouthlogy!

                have a nice weekend
[ Read More ]

Fuso laua watu watano Moro

WANUNUZI watano wa mahindi  wamekufa na wengine watatu kujeruhiwa baada ya tairi la gari walilokuwa wakisafiria, kupasuka na kusababisha gari hilo kupinduka,  katika eneo la Magubike katika Barabara ya Dodoma- Morogoro.Kamanda wa Polisi mkoani Morogoro, Adolphina Chialo, aliwataja waliokufa katika ajali hiyo juzi usiku kuwa ni Mwarami Abdallah, mkazi wa Mzense jijini Dar es Salaam, Selemani Ngula (30), Kasimu Mwitago (30).

Kwa mujibu wa kamanda huyo, maiti mwingine ametambuliwa kwa jina moja la Kiejo (30) wakati mwingine hajatambuliwa. Chialo pia aliwataja waliojeruhiwa kuwa ni, Timoth Paul,  Elisafi Mkumbwa na Hamisi Selemani, wote wakazi wa Kibaigwa  na kwamba majeruhi hao wamelazwa katika Hospitali ya Mkoa wa Morogoro kwa matibabu.

Alisema gari hilo lilikuwa linatokea katika Kijiji cha Kibaigwa, wilayani Kilosa kwenda jijini Dar es Salaam na kwamba chanzo cha ajali ni mwendo mkali.Alisema watu hao walikuwa wanasafiri kwa kutumia gari aina ya Mistubish Fuso iliyokuwa ikiendeshwa na Jackson Bezaleli Senyegwa (27) mkazi wa Kibaigwa ambaye alitoroka mara baada ya ajali hiyo.

Akizungumza na Mwandishi wa habari hizi katika wodi namba moja,mmoja wa majeruhi Hamisi Selemani, alisema gari hilo lilikuwa limebeba gunia 100 za mahindi, jambo lililosababisha  moja ya matairi kuelemewa na kupasuka.

Alisema abiria wote waliokuwa nyuma ya gari hilo walifariki papo hapo baada ajali na kwamba walifunikwa na mahindi.Kamanda huyo alisema miili ya watu hao imehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti cha Hospitali ya Mkoa wa Morogoro, na kuomba wananchi kujitokeza ili kutambua miili ambayo haujatambuliwa.
[ Read More ]

Vijana wa Zanzibar kupata mafunzo ya kujiajiri kutoka India





VIJANA wanaomaliza vyuo vikuu vya Zanzibar wataanza kunufaika na utaratibu wa kupatiwa mafunzo maalumu ya biashara pamoja ufundi yatakayowawezesha kufungua miradi kujiajiri na kuwaajiri vijana wengine na kukuza hali zao za maisha.

Utaratibu huo unatarajiwa kutekelezwa kufuatia mazungumzo yaliyofanyika kati ya ujumbe wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar unaoongozwa na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad na Idara ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (IT&C) ya Andhara Pradesh yaliyofanyika Hoteli ya Grand Kakatiya mjini Hyderabad.

Mbali na hatua hiyo Serikali ya Andhra Pradesh imemwomba Balozi wa Tanzania nchini India, John Kijazi kuandaa utaratibu utakaowezesha Zanzibar kunufaika na makubaliano yaliyofikiwa katika ziara ya Makamu wa Kwanza wa Rais kukuza mashirikiano katika nyanja za kiuchumi, biashara, kilimo na elimu kwa faida ya nchi mbili hizo.

Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari na Mawasiliano wa Serikali ya Andhra Pradesh, Pannola Lakshmaiah alisema utaratibu huo unapaswa kuandaliwa mikakati ya ya utekelezaji mapema ili Serikali mbili hizo hasa Zanzibar iweze kunufaika mapema na kuchangia harakati zake za kuinua hali yake ya kiuchumi.

Alisema Jimbo la Andhra Pradesh limepata heshima kubwa duniani kote kwa Teknolojia ya Mawasiliano na Habari (IT), ambapo pia katika eneo hilo kunapatikana mji maalum wa Teknolojia ya Mawasiliano (Hyderabad Technology City) unaotoa mchango mkubwa katika kukuza uchumi wa eneo hilo na India kwa ujumla.

“Jambo muhimu tutiliane saini makubaliano ya mashirikiano leo hii jioni (jana) na kitakachofuata Balozi aandae utaratibu wa utekelezaji kwa vile hakuna muda wa kusubiri, teknolojia ya habari na mawasiliano hivi sasa ni ajira ni uchumi ni kila kitu”, alisema Waziri wa IT& C.

Katika mazungumzo hayo, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, Ramadhan Abdallah Shaaban alisema bado Zanzibar iko nyuma katika elimu ya IT&C, licha ya juhudi kubwa zinazoendelea kuchukulia kuinua elimu hiyo, ukiwamo mpango mahsusi ulioanzishwa na Serikali ya Zanzibar uitwao E -government.

Waziri Shaaban alisema kuna haja Serikali ya Andhra Pradesh ambapo inafanana kiutawala na Zanzibar ndani ya Jamhuri ya Muungano kushirikiana kuandaa utaratibu wa masomo kwa vijana wa Zanzibar.

Alisema kazi hiyo inaweza kufanikishwa chini ya utaratibu wa kupeleka wataalamu Zanzibar kutoa mafunzo hayo au vijana wa Zanzibar kwenda India kujifunza na baadaye kurudi nyumbani kutumia ujuzi huo kwa maslahi yao na nchi.    

Waziri wa Biashara, Viwanda na Masoko, Nassor Ahmed  Mazrui alisema Zanzibar kuna vijana wengi wanaomaliza vyuo vikuu na kukaa muda mrefu bila ya kupata ajira na utaratibu huo utawasaidia kupunguza tatizo la uhaba wa ajira na kuwapa mafunzo ya kazi maalumu za amali zitakazosaidia kuimarisha maendeleo.

Waziri Mazrui alisema maeneo mengine ambayo Zanzibar inaweza kunufaika katika mashirikiano na Andhra Pradesh ni usindikaji wa bidhaa kama vile za matunda, viungo pamoja na mazao ya baharini.

Waziri Mazrui alisema Zanzibar imejaaliwa kuna rasilimali za viungo kama vile karafuu zao ambao linasafirishwa kwa wingi kwenda India na kama kutakuwa na utaratibu wa kufanyiwa ‘branding’ na baadaye kusafirishwa litaweza kupata soko kubwa zaidi ya sasa katika soko la dunia.
[ Read More ]

Bomu Lililofichwa Kwenye Kilemba Lamuua Rais Mstaafu wa Afghanistan





Aliyekuwa rais wa Afghanistan Burhanuddin Rabbani ameuliwa baada ya mtu aliyelificha bomu kwenye kilemba chake kulilipua bomu hilo wakati wakisalimiana.
Rais Burhanuddin Rabbani ambaye pia alikuwa ndiye mkuu wa baraza kuu la kutafuta amani nchini Afghanistan, alifariki dunia baada ya mtu aliyekuwa akimuamini kumgeuka na kujilipua kwa bomu alilolificha kwenye kilemba chake.

Wasaidizi wanne wa Rabbani nao walifariki dunia baada ya bomu hilo kulipuka wakati Rabanni aliposimama kumsalimia kwa kumkumbatia mwakilishi wa Talibani baada ya kumalizika kwa mazungumzo marefu baina yao ya kutafuta suluhisho la amani nchini Afghanistan.

Fazel Karim Aymaq ambaye ni mjumbe wa baraza la amani la Afghanistan alisema kuwa watu wawili wanaoaminika sana walifika nyumbani kwa Rabbani mjini Kabul ili kuleta ujumbe wa amani toka kwa Talibani.

"Mmoja wao alisalimiana na Rabbani kwa kuweka kichwa chake kwenye mabega ya Rabbani na kulilipua bomu alilokuwa amelificha kwenye kilemba chake", alisema Aymaq.

Taarifa zaidi zilisema kuwa mjumbe huyo wa Talibani alikuwa akijulikana kama Mohammad Masoom na alikuwa akifahamiana vizuri sana na Rabbani akiaminika kuwa anatafuta suluhisho la amani.

Masoom aliluwa akienda mara kwa mara nyumbani kwa Rabbani na aliwahi kumkaribisha Rabbani nyumbani kwake na alimpa ulinzi wa kutosha hali iliyomjengea uaminifu wa kutosha kwa rais huyo wa zamani.

Masoom aliteuliwa na Talibani kuwa mwakilishi wa Talibani katika mazungumzo ya kutafuta suluhisho la amani kati ya Talibani na serikali ya Afghanistan.

Kuuliwa kwa Rabbani ni pigo kubwa sana kwa rais wa Afghanistan, Hamid Karzai ambaye aliamua kukatisha ziara yake nchini Marekani na kurudi Afghanistan.

Mamia ya watu waliandamana leo kwenye mitaa ya mjini Kage.bul kulaani kuuliwa kwa rais huyo mstaafu aliyekuwa akiheshimika kwa jitihada zake za kuleta amani kwenye nchi hiyo ambayo imeharibiwa kwa vita.

"Alitaka amani nchini Afghanistan na alijitolea maisha yake kupigania njia ya kuleta amani", alisema mmoja wa waandamanaji hao.

source nifahamis
[ Read More ]