Banner 468

1234453_10201664080105694_1716282793_n
Facebook

TANZANIA YAWEKA HISTORIA UMOJA WA MATAIFA


DKT. SERVACIUS LIKWELILE, NAIBU KATIBU MKUU WIZARA YA FEDHA NA UCHUMI AKIWASILISHA MPANGO WA PAMOJA WA MAENDELEA KATI YA SERIKALI YA JAMHURI YA MUUNGAO WA TANZANIA NA MASHIRIKA MANNE YA UMOJA WA MATAIFA KATIKA MOJA YA VIKAO VYA BODI TENDAJI ZA MASHIRIKA YA UMOJA WA MATAIFA. VIKAO VYA BODI TENDAJI ZA UNDP, UNICEF, WFP NA UNFPA VINAFANYIKA MAKAO MAKUU YA UMOJA WA MATAIFA, JIJINI NEW YORK, MAREKANI.
---
NA MWANDISHI MAALUM
NEW YORK
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeweka historia ya kuwa nchi ya kwanza duniani kuandaa Mpango wa Pamoja wa Maendeleo kwa kushirikiana na Mashirika Manne yaliyo chini ya Umoja wa Mataifa (UM).
Mashirika hayo ni Mpango wa Maendeleo wa Umoja wa Mataifa (UNDP), Shirika la kuhudumia watoto (UNICEF), Mpango wa Chakula Duniani(WFP) na Shirika linalohusika na Idadi ya watu (UNFPA). 
Kufuatia kukamilishwa kwa mchakato huo wa aina yake, Jumuia ya Kimataifa imeipongeza na kuisifu Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuonyesha njia na kuwa mfano wa kuigwa na mataifa mengine.
Mpango huo ambao unajulikana kama Common Country Programme Document (CCPD), Umewasilishwa mbele ya Bodi tendaji za UNDP na UNFPA na Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha na Uchumi, Dkt. Servacius Likwelile. Ukiwa ni sehemu ya Mpango Mkubwa wa Umoja wa Mataifa ( UNDAP).
Bodi Tendaji za Mashirika hayo manne zinafanya mikutano yao ya kikazi katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa, New York.Ambapo Tanzania ilipatiwa fursa ya kuwasilisha Mpango huo.
Utekelezaji wa CCPD utafanyika kwa miaka minne kuanzia Julai 2011 hadi June 2015. Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia mpango huo itapata Dola za Kimarekani 773 milioni zitakazotolewa na Umoja wa Mataifa.

Akiuwasilisha CCPD Naibu Katibu Mkuu anasema, maandalizi na utekelezaji wake umezingatia vipaumbele na mipango ya maendeleo ambayo Serikali zimeainisha kupitia MKUKUTA kwa Tanzania Bara na MKUZA kwa Tanzania Visiwani.

“ Ingawa tumeshirikiana na mashirika hayo tangu hatua zote za maandalizi hadi utekelezaji wake, huu ni mpango wetu, tunaumiliki wenyewe na tumehakikisha unakidhi vipaumbele ambavyo Serikali zimejiwekea katika kuharakisha maendeleo ya wananchi wake” anasema Dkt. Likwelile.
Anaongeza kuwa maandalizi hayo pia yamewashirikisha wadau wengine zikiwamo asasi zisizo za kiserikali.
Dkt. Likwelile anasema kwa Tanzania kuwasilisha mpango huo katika Bodi tendaji za Mashirika hayo, kumeipa fursa nchi ya kutoa uzoefu wake kwa nchi nyingine wa namna ya mchakato mzima ulivyofanyika. 
“ Lakini hii pia ni changamoto kwa UM, kwa sababu kwanza, hawakutegemea kwamba tungefikia hatua hii, tumewaonyesha njia, na tunawapa changamoto ya kuwa sasa wana mahali pa kuanzia katika kuboresha mfumo wa utendaji katika ngazi ya nchi”, anasisitiza Naibu Katibu Mkuu. 
Akasema kuwa Mpango unaweza kutumika kama mwongozo kwa UM kama ulivyo au kwa kuuboresha kwa kuzingatia mahitaji na malengo ya nchi husika.
Akielezea manufaa ya kuwa na CCPD,Dkt Likwelike anayataja manufaa yake kuwa ni pamoja na kuboresha utendaji kazi, utekelezaji, ufuatiliaji, ufanisi katika matumizi ya raslimali fedha.
Manufaa mengine ni kujenga uwezo wa raslimali watu ndani ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa ili kwa pamoja waweze kukabiliana na changamoto za kuleta maendeleo.

Kupitia CCPD, sasa inakuwa rahisi kujua nani anafanya nini na katika eneo gani, na itasaidia kupunguza muingiliano wa shughuli kati ya Shirika moja na jingine na kwa upande mwingine Serikali itaondokana na urasimu na ukiritimba wa kufanya kazi na shirika moja moja.
Maeneo yatakayonufaika na mpango huo ni Mazingira, HIV/AIDS,Elimu, Afya, Ukuaji wa Uchumi, Utawala Bora na Masuala ya Wakimbizi.

Bi Anne Webster kutoka Ubalozi wa Ireland, akizungumza kwa niaba ya mataifa 17 anasema.
“ Kama marafiki wa maboresho ya mfumo wa UM, na baada ya kufuatilia kwa makini mchakato wote huu. Tumeridhishwa sana na kazi iliyofanywa.Tunapenda kutambua na kuipongeza Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa hatua hii ya kihistoria” 

Nchi hizo ni Japan, Sweden, Uingereza, Ujerumani, Jumuia ya Ulaya, India, Canada, Finland, Belgium, Denmark,Netherelands, Norway, Ireland, Ufaransa, Spain, Switzerland na Marekani.
Akasema nchi hizo zinaunga mkono kwa dhati Mpango huo kwa sababu unaifanya Tanzania kuwa mshirika mkubwa wa UM katika maeneo muhimu ya Maendeleo.

Watendaji Wakuu wa Mashirika ya UNDP Bi Helen Clark na UNFPA Dkt. Babatunde Osotimehin, nao kwa nafasi zao walitumia fursa hiyo kuutambua, kuupokea na kuipongeza Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuukamilisha, lakini pia kwa hatua mbalimbali za maendeleo ya kiuchumi, kijamii na kisiasa.
[ Read More ]


 
‘’ASalaammu Alaikum’’ 
Jummuah Mubarak 
  

O Allah!
On this blessed day we ask of you... 
Guide us among those, whom you have guided, 
And grant us protection among those whom you have protected. 
  
Befriend us among those whom you have befriended. 
Grant us blessings in that, which you have given us, 
And save us from the evil which you have ordained. 
  
For, surely, your decree matters and no one decrees over you. 
Indeed the one whom you befriend will never be dishonored, 
And the one with whom you have enmity will never be honored. 
  
You are Most blessed our Lord and You are Most Exalted.. 
We seek your forgiveness and turn towards you in repentance. 
  
And may Allah send salutations upon the most Honorable Prophet Muhammad (S.A.W). 
  
O Allah! Grant respect to Islam and the Muslims. 
O Allah! Assist Islam and the Muslims. 
O Allah! Create love among the hearts of the believers, 
O Allah! Destroy the unbelievers, who prevent people 
From the path of your religion, reject your Messengers, 
And who fight against your friends.
O our Beloved Allah! Hear our dua’s..
Aameen .. Ya Rabul-Aalimeen (Oh Creator of Everything)
[ Read More ]

Mashindano ya kusoma Qur'an London.




Hafla ya matokeo ya kusoma Qur'an ya mwaka 2010 (1431 AH) yamefanyika siku ya Alhamisi ya tarehe 03/02/2011 katika ukumbi wa Town Hall, East Ham, jijini London.

Washiriki wasiopungua 18 walishiriki mashindano hayo ya kusoma Qur'an yaliyoandaliwa na kituo cha kujitolea na kinachosaidia Waislamu waishio nchini Uingereza (Salama Trust).

Mashindano hayo yaligawanyuka katika makundi matatu. Mshindi wa kwanza katika kundi la kwanza alikuwa Khayrat Juma ambaye alipata kura 99%, mshindi wa pili katika kundi la kwanza alikuwa Yaaqub Abeid ambaye alipata kura 98% na mshindi wa tatu alipata kura 85%.

Kundi la pili, mshindi wa kwanza Rashid Mohammed alipata kura 100%, Mujahidi Mujahidi alitokea mshindi wa pili kwa kupata kura 94% na mshindi wa tatu Faisal Issa aliyepata kura 85%.

Ashraf Khalifa ndiye mshindi katika kundi la tatu kwa kupata kura 100%, Mohammed Yusuf alitokea mshindi wa pili kwa kupata kura 87% na Abdulmajid Yusuf alitokea mshindi wa tatu kwa kupata kura 64%.

Mwenyekiti wa Salama Trust Bw. Salehe Jaber aliwapongeza washiriki wote kwa kujitolea kushiriki mashindano hayo ya kusoma Qur'an.

"Umoja na ushirikiano ndiyo chanzo cha maendeleo" alisema Bw. Jaber na kusisitiza mshikamano kwa waislamu dunia kote.

Ally Muhdin - WWW.TZ-ONE.BLOGSPOT.COM
[ Read More ]

Taarifa Ya Habari Yasomwa Gizani Nepal


''Ifuatayo ni taarifa ya habari ikisomewa gizani, kwa kuwa umeme umekatwa.'' Mojawapo wa vituo vikuu vya televisheni nchini Nepal kimeanza kutangaza taarifa zake za habari za usiku katika mazingira ya nusu kiza ili kubainisha athari za ukataji mkubwa wa umeme.

Tangu mwanzoni mwa mwezi wa February, kituo cha televisheni cha Kantipur kimetumia taaa zinazotumia mafuta kutoa mwanga wakati wa taarifa yake ya habari ya dakika 30 saa moja usiku.

Mkuu wa kituo hicho alisema shabaha ni kutia shinikizo kwa serikali ikabiliane na tatizo hili.

Kwa sasa Nepal inakabiliwa na mpango wa kukata umeme kwa saa 12 kila siku.

"tunaitaka serikali izalishe umeme zaidi kwa haraka" mkuu wa Kantipur News Tirtha Koirala aliiambia BBC.

"hadi sasa watazamji wetu wamepokea vizuri hatua hii;lakini serikali bado haijasema chochote."

Licha ya kuwa na uwezo mkubwa wa kuzalisha umeme kutokana na mito, Nepal huzalisha nusu tu ya mahitaji yake ya umeme.

Miaka kumi ya vita vya wenyewe kwa wenyewe kati ya waasi wa Kimao na serikali ya Nepal vilivyomalizika mnamo mwaka 2006, imemaanisha uwekezaji mdogo sana katika sekta ya umeme ya Nepal.

Juu ya yote hayo mtandao wa kusambaza umeme nchini uliathiriwa vibaya sana baada ya kuharibiwa na mafuriko ya mto Kosi mnamo mwaka 2008.

Hii imesababisha kuwepo na mgawo wa umeme kuwa ni jambo la kawaida katika maisha ya kila siku.

Tatizo ni kubwa zaidi katika majira ya baridi ambapo ukosefu wa mvua na kina cha chini cha mito inamaanisha mabwawa yaliyopo hayawezi kuendesha shughuli zao kikamilifu.

Mamlaka ya nguvu za umeme ya Nepal yanayomilikiwa na serikali yamesema kuwa nchi inaweza kutazamia kukatwa umeme kwa kipindi cha saa 14 kila siku katika muda wa wiki chache zijazo.

"tunasumbuka sana kwa sababu ya mgawo wa umeme ," amesema Bwana Koirala .

"Takriban wanafunzi 400,000 hivi sasa wanajitayarisha kwa mtihani wa shule za sekondari na hawana mwanga wowote wa taa usiku".

"Halikadhalika wafanyibiashara wadogo wadogo ambao hawawezi kumudu jenereta au kifaa cha "inverter"nao pia hawawezi kuendesha shughuli zao."

Bwana Koirala alisema taarifa za habari za kituo chake zitaendelea kutangazwa katika mazingira ya kiza mpaka serikali itakapochukua hatua .
[ Read More ]

Shahidi akitoa ushuhuda kuhusiana na kutupwa kwa vichanga 11

[ Read More ]

UKATILI: MAITI ZA VITOTO 11 ZAFUKULIWA SHIMO MOJA.

KATIKA hali isiyo ya kawaida, wakazi wa Mwananyamala Kwakopa, jijini Dar es Salaam wamepatwa na mshituko mkubwa baada ya kaburi moja kugundulika jana (Jumatatu) likiwa na watoto 11 waliozikwa ndani yake, tukio lililoelezwa kuwa ni ukatili wa kutisha, Uwazi lina habari kamili.

Habari zilizolifikia gazeti hili jana zilieleza kuwa mkazi mmoja wa eneo hilo aliyefahamika kwa jina moja la Thabiti  ndiye aliyeligundua kaburi hilo alipokuwa  akitafuta sehemu ya kuchimba jalala, jirani na Hospitali ya Mwananyamala.
Ilielezwa kuwa mzee huyo alipofika eneo hilo alishtuka baada ya kuona nzi wengi wamezingira huku kukiwa na harufu kali, machale yakamcheza na kuhisi kuwa huenda kuna kitu kibaya kimefukiwa.

“Mzee Thabiti aliamua kuwataarifu polisi ambao walifika eneo la tukio, jirani na makaburi ya Mwananyamala. Baada ya kuona hali ilivyokuwa, polisi waliwapigia simu madaktari waliowasili muda mfupi baadaye,” kilieleza chanzo chetu.

POLISI KUFIKA ENEO LA TUKIO
Habari zinaeleza kuwa mara baada ya polisi kupewa taarifa hizo na kuwasili eneo la tukio wakiwa kwenye gari aina ya Landrover ‘defender’ walianza uchunguzi wao mara moja.
Mwandishi wetu aliyekuwepo eneo la tukio, alishuhudia kazi ya kufukua kaburi hilo ikifanywa kwa uangalifu mkubwa.

Dakika chache baadaye  shimo likiwa na urefu wa futi nne, lilionekana shuka jeupe likiwa limeviringishwa kitu. Lilipotolewa, kwa mshangao mkubwa maiti ya kitoto kichanga ikadondoka.

Polisi aliyekuwa akifanya kazi hiyo alipolichunguza vizuri shuka lile, aligundua kuwa kuna kitu kingine kimebaki. Alipoingiza mkono, alichomoa maiti nyingine ya kitoto kichanga.

KANGA KIBAO ZILITUMIKA
Askari huyo aliendelea na zoezi hilo na baadaye akalifunua kabisa shuka hilo, ndipo alipokuta maiti nyingine za watoto wachanga zikiwa zimevingirishwa kwenye kanga tofauti. 
Zilipohesabiwa ilibainika kuwa jumla ya maiti 11 zilikuwa zimefukiwa kwenye kaburi hilo.

Uchunguzi zaidi ulibaini kuwa moja ya kanga iliyokutwa kwenye kaburi hilo ilikuwa imebandikwa plasta yenye maneno yaliyosomeka: ‘Ruth Mtanga, Male Pre-mature (yakimaanisha kuwa mwanamke mwenye jina hilo alikuwa amejifungua ‘njiti’ wa kiume).

Haikufahamika maandishi yale kwenye plasta hiyo yameandikwa na nani katika hospitali gani, hivyo polisi wakaanzia uchunguzi wao hapo.
Uchunguzi wa gazeti hili eneo la tukio ulibaini kuwa shuka lililotumika kuviringishia maiti za watoto hao lilikuwa imeandikwa Mwananyamala.

DAKTARI AKACHA WANAHABARI
Daktari mmoja wa Hospitali ya Mwananyamala aliyefahamika kwa jina moja la Karamahia, alipohojiwa kuhusiana na shuka hilo pamoja na maiti za watoto hao wachanga, alikataa kusema chochote kwa madai kuwa tayari sakata hilo lipo mikononi mwa polisi.

Polisi waliondoka na miili hiyo kuelekea Hospitali ya Mwananyamala, ilikoenda kuhifadhiwa wakati uchunguzi wa kina ukiendelea. 
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni, Charles Kenyela alipohojiwa na gazeti hili jana, alisema taarifa hizo amezipata na anazifanyia kazi hivyo apewe muda.

WANANCHI WALIVYOSIKITISHWA
Hata hivyo, baadhi ya wananchi walioshuhudia tukio hilo waliliambia Uwazi kwa masikitiko kuwa kitendo hicho siyo cha kibinadamu na ni tukio la kwanza la kutisha kugundulika hapa nchini.
“Haya mambo ya binadamu kuzikwa kaburi moja tulikuwa tukiyasikia kwa wenzetu lakini sasa tumeyashuhudia hapa leo. Haya ni mambo ya kutisha,” alisema shuhuda mmoja aliyejitambulisha kwa jina moja la Zuwena.

Uchunguzi zaidi umebaini kuwa watoto hao  hawakuzikwa siku nyingi zilizopita kwa sababu walikuwa bado hawajaharibika sana.



source-global publisher
[ Read More ]

WASHIRIKI WA SHINDANO LA KISURA WA TANZANIA 2011 WAANZA KAMBI.



Pichani kati Mwenyekiti na Mwanzilishi wa mradi wa Kisura wa Tanzania (BTA), Juliana Urio,akizumgumza na baadhi ya waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusina kuanza kambi wa warembo wa shindano la Kisura wa Tanzania 20110.kushoto ni Meneja masoko wa SBC,Bwa.George Michael,Afisa Mipango Ujana wa FHI Bwa.Aziz Itaka,Mwisho kabisa ni Meneja Masoko wa ATCL,Bwa. Musyangi Kajeri
WAREMBO wanaowania taji la Kisura wa Tanzania 2010/11, wameingia kambini mapmea jana katika Hoteli ya Kiromo View Resort, iliyopo nje kidogo ya Mji wa Bagamoyo,Pwani, tayari kwa fainali zitakazofanyika Machi 12, mwaka huu. Kambi hiyo itahusisha wasichana 25 kutoka mikoa mbalimbali nchini, waliofanikiwakutinga katika hatua ya fainali za shindano hilo, baada ya mchujo uliofanyika kwa miezi miwili.

Mchakato wa kuwapata wasichana
hao, ulianza Desemba 11, mwaka jana, na kumalizika mapema mwezi wa kwanza, ukihusisha warembo kutoka mikoa ya Mwanza,Mara, Kagera, Shinyanga, Tabora, Dar es Salaam, Arusha, Manyara, Dodoma, Iringa,Mbeya na Ruvuma.

Akizungumza wakati wa kuwatambulisha warembo hao katika Hoteli ya Kiromo ViewResort, Mwenyekiti na Mwanzilishi wa mradi wa Kisura wa Tanzania, Juliana Urio kutoka kampuni ya Beautiful Tanzanie Agency (BTA), alisema kuwa warembo walioingia kambini, ni wale waliopita katika mchujo baada ya kukidhi vigezovinavyotakiwa.

Vigezo hivyo urefu wa sentimita174, mapaja 36, kiuno 25, kifua 36 na umri ni kati ya miaka 18-27, bila kujali kama mshiriki ameolewa, kuzaa au la.“Mwaka huu idadi ya warembo walioingia kambini imeongezeka, kutoka 20 kama ilivyokuwa awali hadi 25, hii ikitokana na mdhamini wetu Kiromo View Resort kutupa nafasi ya pekee ya kuongeza wasichana watano zaidi,” alisema.Urio aliwataja warembo walioingia kambini kuwa ni Neema Methew na Silipa Swai kutoka Mwanza, Lilian Bussa na Gaudencia Joseph (Mara), Beatrice James (Kagera),

Monica Fikiri na Angella Mombeki (Tabora).Wengine ni Suzana Manoko, Winnfrida Sabega, Rita Swai, Lethina Christoper, Joyce Joseph, Happiness Salimenya, Grace David (Dar es salaam), Dotinata Soro, Neema Kilango, Neema Seley (Arusha), Kipoyane Laibon (Manyara), Mariam-Kissa Isaack, Asha Hamisi, Flavian Makungwa, Lucy John (Dodoma) na Queen Kabisama (Ruvuma).

Alisema kuwa wakiwa kambini, warembo hao watapewa mafunzo mbalimbali kuhusiana na maisha yao binafsi na jinsi ya kukabiliana na changamoto zinazowazunguka katika maisha yao ya kila siku, ikiwa ni pamoja na kutembelea maeneo tofauti. Urio aliwapongeza warembo waliopata bahati ya kutinga fainali za shindano hilo,ikiwa ni pamoja na kuwashukuru wazazi waliowaruhusu watoto wao kujiunga shindano hilo, akiwaahidi ‘kuwapika’ vilivyo warembo hao ili waweze kuwa mfano wa kuigwa kwa jamii ya kitanzania kutokana na matendo yao.

Mdhamini mkuu wa shindano hilo ambalo linafanyika kwa mara ya tatu sasa, ni Family Health International (FHI), wakati wadhamini wengine ni TBC1, Kiromo View Resort, TanFoam (Arusha), SBC Limited, Flare Magazine, Hugo Domingo, BASATA, GRM Production, Clouds FM, ATCL na MJ Records

[ Read More ]

ZAIDI YA WAGONJWA 263 WA FESTULA NA MDOMO WA SUNGURA WAMENUFAIKA NA HUDUMA YA M PESA


Mkurugenzi msaidizi wa hospitali ya CCBRT Haika Mawala akimkaribisha Mkurugenzi wa mahusiano na Vodacom Foundation Mwamvita Makamba wa pili toka kushoto akiambatana na Mkuu wa kitengo cha Safaricom Foundation-Kenya Sanda Ojiambo walipotembelea hospitali ya CCBRT kwa lengo la kujionea jinsi gani huduma ya Vodafone M pesa inavyosaidia wagonjwa wa fistula na mdomo wa sungura kwa kutumiwa fedha za nauli na matumizi ya njiani kwenye mikoa mbalimbali hapa nchini na kuja kutibiwa hospitalini hapo zaidi ya wagonjwa 263 wamenufaika na huduma hiyo.
Mkurugenzi msaidizi wa hospitali ya CCBRT Haika Mawala akimkaribisha
Mkurugenzi wa mahusiano na Vodacom Foundation Mwamvita Makamba
Mkurugenzi wa Vodafone Foundation wa Egypt Noha Saad kushoto akisaini kitabu cha wageni katika hospitali ya CCBRT mara baada ya kutembelea hospitalini hapo na wakurugenzi wenzake Mwamvita Makamba,Mkuu wa kitengo cha Safaricom Foundation-Kenya Sanda Ojiambo wakiwa na lengo la kujionea jinsi gani huduma ya Vodafone M pesa inavyosaidia wagonjwa wa mdomo wa sungura na fistula kwa kutumiwa fedha za nauli na matumizi ya njiani kwenye mikoa mbalimbali hapa nchini na kuja kutibiwa hospitalini hapo zaidi ya wagonjwa 263 wamenufaika na huduma hiyo.
Mkuu wa kitengo cha Safaricom Foundation-Kenya Sanda Ojiambo(kushoto)akizungumza na waandishi wa habari katika hospitali ya CCBRT walipotembelea hospitalini hapo kwa lengo la kujionea ni jinsi gani huduma ya M pesa inavyosaidia wagonjwa wa fetula na wa mdomo wa sungura kwa kutumiwa fedha za nauli na matumizi ya njiani kwenye mikoa mbalimbali hapa nchini na kuja kutibiwa hospitalini hapo zaidi ya wagonjwa 263 wamenufaika na huduma hiyo,katikati Mkurugenzi wa Vodafone Foundation Uingereza Andrew Dunnet,Mkurugenzi wa Vodafone Foundation Tanzania Mwamvita Makamba.
Mkurugenzi wa hospitali ya CCBRT Tom Vanneste akifafanua jambo kuhusu ugonjwa wa mdomo kisungura na fistula kwa maafisa wa Vodafone M pesa Afrika walipotembelea hospitalini hapo hawapo pichani kujionea jinsi gani huduma ya M pesa inavyosaidia wagonjwa kutoka mikoa mbalimbali hapa nchini na kuja kutibiwa hospitalini hapo zaidi ya wagonjwa 263 wamenufaika na huduma hiyo.

[ Read More ]

NIZAR KHALFANI AENDELEA KUNG'ARA NYUMBANI NA CANADA


Mchezaji nyota wa Vancouver Whitecaps ya jijini Vancouver huko British Columbia, Canada, akiwa anafundisha watoto kuliskata kabumbu maeneo ya Tabata jijini Dar alipokuja kuchezea Taifa Stars. Nizar amekuwa lulu kwa timu hiyo ya kulipwa na Taifa Stars, yote hii ikitokana na kujituma, nidhamu na kupenda kazi yake. Ni mfano wa kuigwa
Nizar ana mashabiki wengi watoto kwa wakubwa 
na anapeperusha vilivyo bendera yetu
Nizar akinyanyasa ngome ya adui
Nizar akiwakilisha wakati Taifa Stars ilipocheza na Brazil Dar
Nizar huwa haachwi peke yake. akiachwa tu nyavu hizi...
Nizar na kikosi cha kwanza cha Vancouver Whitecaps. 
Kwa habari kamili ya timu hiyo
BOFYA HAPA
[ Read More ]