Banner 468

1234453_10201664080105694_1716282793_n
Facebook

Milango ya Zanzibar : Mji mkongwe.



gari linaloonekana ndio lilikuwa gari la Prez wa kwanza wa Zanzibar Marehemu A.Karume.


Milango ya Zanzibar ilianza kutumika katika miaka ya 1870 na kupata umaarufu mkubwa hadi sasa.Milango hii ilibuniwa na kuchongwa kufuatana na tamaduni za kihindi na kiarabu.

Katika miaka hiyo ya 18' jumla ya milango 806 ilitengenezwa. Hiki kilikuwa ni kipindi cha Sultan Bargash.
Sifa kubwa ya milango hii ni mapambo yake ambayo yalitokana na dhana ya kujikinga na madhara ya kishetani kuingia ndani ya nyumba. Mapambo mengine yaliyomo kwenye milango hiyo ni maua, matawi ya minazi, aya za Koran, jina la mwenye nyumba na mwaka uliotengenezwa mlango huo.

Zaidi baadhi ya milango hiyo imetiwa vyuma umbo la koni nyenye ncha kali ikiwa ni kama silaha ya kujikinga na uvamizi wa Tembo.


Kuna aina mbili za milango hii, moja ni umbo la mstatiri katika sehemu yake ya juu na ya pili ni umbo la nusu duara katika sehemu yake ya juu. Mlango mmoja uchukua muda wa miezi mitatu kutengenezwa na hutumia mbao ngumu aina ya Mninga. Hadi sasa milango hii hutengenezwa kwa kutumia mkono. Hata hivyo katika karakana ya Ofisi ya Hifadhi na Uendelezaji Mji Mkongwe, baadhi ya maandalizi ya utengenezaji wa milango hiyo hutumia mashine.


Mamlaka ya Hifadhi na Uendelezaji wa Mji Mkongwe, inastahili kupongezwa kwa kuhakikisha kuwa aina hii ya milango inaendelea kutumika katika Mji Mkongwe. Hii ni kutokana na kuwepo na wimbi kubwa la kung'olewa kwa milango hiyo katika miaka ya 80 kwa lengo la kuuzwa. Adhia kuwepo kwa ubadilishaji wa milango hiyo kutokana na kufanyiwa matengenezo ya nyumba.


picha na habari kutoka:kibunango.blogspot.com
[ Read More ]

Maiti ya mtoto yakutwa juu ya kaburi!!!


MAITI ya mtoto mdogo wa kike anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka miwili hadi mitatu, imekutwa juu ya kaburi katika eneo la Buguruni Madenge, Wilaya ya Ilala, Dar es Salaam.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Faustine Shilogile alisema maiti huyo ambaye hajatambuliwa, aliokotwa juzi saa 5 asubuhi.
Alisema mwili wa mtoto huyo uliokotwa ukiwa hauna jeraha lolote, ingawa alikuwa anatokwa na povu mdomoni na kwamba mpaka sasa haijajulikana maiti huyo alifikaje juu ya kaburi hilo na kwa madhumuni gani.
Aidha, Kamanda Shilogile alisema sababu na chanzo cha kifo cha mtoto huyo hakijafahamika na maiti amehifadhiwa Hospitali ya Amana kwa uchunguzi zaidi huku Polisi ikiendelea na msako dhidi ya watuhumiwa.
Akizungumza kwa simu jana kufafanua tukio hilo, Kamanda Shilogile alisema hawajamkamata mtu yeyote kuhusiana na tukio hilo ambalo lina utata. “Mtoto alikuwa amefunikwa kwa nguo.
Hakuwa na jeraha lolote. Lakini unaweza kujiuliza maswali mengi kuhusu tukio zima. Je, alitupwa hapo? Alikuwa anaumwa, au ilikuwaje,” alisema Kamanda Shilogile na kuongeza kwamba hata mazingira ya kulihusisha na ushirikina, pia inawezekana.
[ Read More ]

Drunk millionaire 'lost' £130,000 car


A wealthy property tycoon lost his £130,000 Lamborghini Gallardo supercar after a night out because he was too drunk to remember where he had parked it.
Glenn Knowles, 35, was accused of fraud when the car disappeared and has not been found since, even though it was fitted with a satellite tracking device.
Mr Knowles appeared at Guildford Crown Court with the Lamborghini's co-owner, Richard Mant.
Both were cleared of fraud when the jury accepted Mr Knowles' claim that he had been so drunk he could not recollect where he had left the Italian sports car.
When he realised the car was missing, Mr Knowles tried to cover his embarrassment by lying to his friend Mr Mant and the police, saying he didn't know what had happened to the car.
Knowles only later admitted he'd taken the car from his friend's house when the police showed him video images of the car being driven from Mr Mant's home in Epsom towards Gillingham, Kent where Mr Knowles' parents live.
After drinking heavily that night, Mr Knowles and Mr Mant then reported the car stolen and informed their insurance company of the car's theft.
Mr Knowles, who earns £160,000 per year from his property empire, said both he and Mr Mant had "no motive to commit fraud" and that they had intended to keep the Lamborghini.
The two men have shared several high performance cars since their early 20s, including a Mercedes convertible that Mr Knowles had also previously forgotten where it was parked after a night out. The Mercedes was subsequently found parked behind a nightclub in Kingston, Surrey.
Summing up, Judge Neil Stewart said: "As time went on, Mr Knowles found it harder and harder to confess and took the view that either way the car was stolen, but he said he realises it was the wrong thing to do."
[ Read More ]

WANAFUNZI WA KITANZANIA NUSURA KUUWAWA KWA MOTO BANGALORE -INDIA


TANZANIA STUDENTS ASSOCIATION BANGALORE
(TASABA)
WANAFUNZI WA KITANZANIA NUSURA
KUUWAWA KWA MOTO BANGALORE -INDIA
-----------
Tarehe 11/03/2010 majira ya saa 11:30 wanafunzi wawili ,Hamis Mbelwa Fintan mwenye na Olais Alexendra Siarra waliokuwa wanakaa No.1093/1.11th Cross,Swarnanagar,Robertsonpet,KGF-563 122. Walinusurika kuuwawa kwa moto baada ya fujo iliyofanywa na wahindi wakidai kuwachukia waAfrika.
Wahindi hao waliamua kuchukua mafuta ya petrol na kumwaga dirishani na mlangoni, walifanikiwa kuwasha moto kupitia malangoni na moto kuanza kuingia ndani wakati vijana hao wakiwa ndani. Kwa bahati nzuri walifanikiwa kuuzima moto uliokuwa unaingia ndani na ule wa nje wasamalia wema waliuzima, bahati nzuri petrol ilikuwa chache hivyo hakuna madhara makubwa yaliyotokea.

Nilipopata taarifa hii nilitoka na kufika kituo cha Police cha Hennur Cross, nilitoa taarifa hiyo wakatoka maafisa wa police na kufika sehemu ya tukio wakati huo mimi nikiwa nimebaki kituoni. Baada ya dakika 30 police walirudi bila watuhumiwa, nilipouliza walinijibu nirudi nyumbani wameshawatuliza na hawatarudia tena nilibishana sana na police juu ya hilo maana walipofika waliwakuta watuhumiwa na kuwaachia waende huru.
Nilizidi kupigania haki lakini walinijibu “This is India not Tanzania and we have to cop with them like it or not” niliwauliza kama huo ndio utamaduni wao wa kumwagia watu petrol na kuchoma moto kutaka kuwaua? Wakasema kama naona hawajanisaidia niende kutafuta msaada mahali pengine.
Nilisikitika sana kwa kauli za police hasa ukizingatia kuwa toka kifo cha mwenzetu Imran Mtui ni mwezi tu na siku 7 mpaka sasa na hatujapata taarifa ya kuridhisha kutoka kwa police halafu linatokea jaribio lingine la kuua kwa kutumia petrol.
Hali hii inatisha hasa nikiwa kama mwenyekiti wa jumuiya ya wanafunzi kuona raia wenzangu wanatishiwa kutolewa maisha yao kwa moto na bila hatia huku police wakiona jambo hilo ni la kawaida kwao na kuwaachia watuhumiwa waende huru. Watu hawa wanaishi nchini kwetu kwa amani na kufaidi matunda ya uhuru na uchumi wa nchi yetu bila bugudha.


Baada ya kuona hakuna masaada kutoka police niliwashauri Hamis Mbelwa Fintan na Olais Alexendra Siarra wahame mahali pale kwani hapana usalama tena. Tunaomba sana msaada toka nyumabani na ofisi zetu za ubalozi zilizopo New-Delhi India kutafuta jinsi ya kufanya waTanzania waishio Bangalore –India na kwingine kote kuishi kwa amani, imezoeleka kuwa mara zote wanafunzi ni wakorofi lakini kwa tukio hili nakataa kabisa kama chanzo ni wahanga hawa bali ni chuki binafsi iliyoko dhidi ya wa Afrika ambayo inatufanya tuishi kwa uoga na wasiwasi mkubwa sana. Leo hii petrol ilikuwa chache siku nyingine itakuaje? Je wangefanikiwa kutoa roho za vijana hawa majibu kutoka vyombo vya dola vya India ingekuwa ni nini? Au wangesema wamejiua tena vijana hawa kwa moto? Haya ni maswali machache ya kujiuliza.


“Mungu ibariki Tanzania, Mungu tubariki wanafunzi wa kiTanzania tuishio Bangalore India”


Fidelis Msomekela


Mwenyekiti – TASABA

+919742176980

[ Read More ]

Meli ya m.v serengeti yawaka moto.

Meli ya MV Serengeti ilivyowaka jana ikiwa nangani.kwenye bandari ya zanzibar.
[ Read More ]

Sheikh Mkuu Wa Misri Dr Muhammad Sayyed Tantawyi Afariki Dunia


Sheikh Mkuu wa Tanzania Sheikh I ssa Shaabani Simba (shoto) akiwa katika picha ya pamoja na Sheikh Mkuu wa Misri (Sheikhul-Azhar v-GRAND SHEIKH OF AL-AZHAR - Pr,) Dr Muhammad Sayyed Tantawyi katika Ofisi zake za Masheikhatul-Azhar zilizopo mji wa Darassa mwezi jana.
Habari zinasema Dr. Tantawyi amefariki dunia huko Misri.
Sheikh Mkuu wa Tanzania alikuwa nchini Misri kuhudhuria Mkutano Mkuu wa 22 (The 22nd General Conference. Under the Title The Objectives of Shariah(Islamic Law)And Issues of the Contemporary Age.



Marehemu amefariki leo saa 12:00 asubuhi katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mjini Riadh Nchini Saudi Arabia akijiaanda kwa safari ya kurudi Nchini Misri.
Sheikh alikuwa Nchini Saudia Arabia Kuhudhulia Hafla ya ugawaji wa tunzo ya Mfalme Faisal iliyokuwa ikigaiwa kwa baadhi ya viongozi kutoka Nchi mbalimbali akiwemo Waziri Mkuu wa Uturuki.

Sababu za kifo chake ni Presha(Mshtuko wa Moyo) uliomtokea Ghafla akiwa kwenye ngazi ya Ndege,Taarifa zinasema hali hiyo imetokana na Uchovu aliopata kutokana na Shughuli hiyo ya jana.      


source:michuzi                                               




[ Read More ]

MAALIM SEIF YU HAI NA ANAENDELEA VIZURI

Uvumi ulioenea nchini ya kwamba Maalim Seif emefariki dunia unaonekana hauna ukweli wowote baada ya kuthibitika kwamba Maalim anaendela vizuri katika Hospitali ya Hindu Mandal.
Uvumi huo uliokua ukisambazwa leo hii kwa njia ya simu (SMS)unaeleza kua Maalim Seif amefariki dunia leo katika Hospitali ya Hindu Mandal ambapo alikua amelazwa tokea jana baada ya kuanguka jana Uwanja wa Ndege Jijini Dar-es-salaam alipokua akisubiri ndege kuelekea nchini Oman.
Maalim alikua anasumbuliwa na tatizo la Presha pamoja sukari, lakini kwa sasa anaendelea vizuri na anatarajia kuruhsiwa kwenda nyumbani hii leo.
InshaaAllah Mungu ampe afya njema......Amiin
[ Read More ]

UMEME ZANZIBAR KUREJEA JUMANNE IJAYO

Huduma ya umeme visiwani Zanzibar inatarajiwa kurudi Jumanne ijayo baada ya kukamilika kazi za utengenezaji wa kituo cha kupokea umeme kilichopo Fumba, Mkoa wa Mjini Magharibi, Unguja.

Kaimu Meneja wa Shirika la Umeme Zanzibar (ZECO), Hassan Ali Mbarouk, aliwaambia waandishi wa habari waliotembelea katika kituo chenye kufanyiwa matengenezo cha Fumba kwamba ikiwa kazi ya kurejesha huduma hiyo itafanyika kama ilivyopangwa basi huduma hiyo itarejea siku hiyo.

Alisema kazi hiyo iliyobakia ni kuunganisha waya za umeme kutoka nchi kavu na baharini na kazi hiyo ya kuunganishwa kwa waya kutoka katika vituo vya Fumba hadi Ras Kiromoni Tanzania Bara itachukua muda wa siku tatu.

Akitaja hatua zitakazochukuliwa za kurejesha huduma hiyo, Kaimu Meneja huyo alisema hadi Jumapili ijayo kazi ya matengenezo itakuwa imemalizika na matarajio Machi 8 kutafanyika vipimo vya majaribio na Machi 9 ndiyo huduma hiyo inatarajiwa kuwashwa.

Aliwaeleza waandishi wa habari kuwa kuchelewa kwa huduma hiyo kumesababishwa na mafuta yaliyokuwemo ndani ya waya zinazoleta umeme kutokuwa safi na kulazimika kusafishwa kwa muda wa siku tatu.

Wakazi wa visiwa hivyo wamekosa huduma ya umeme tangu Desemba mwaka jana, baada ya kutokea hitilafu katika kituo cha kupokea umeme huo kutoka Ras Kiromoni hadi Funmba mjini Unguja.
[ Read More ]

300 dead in massive quake in Chile, search on for survivors.


SANTIAGO: Rescue teams hunted for survivors on Sunday after one of the largest earthquakes on record killed at least 300 people in Chile and sent giant waves roaring across the Pacific Ocean.

In an address to the nation on Saturday, President Michelle Bachelet said two million Chileans had been affected but, after touring the worst-hit areas by plane, she found it hard to spell out the magnitude of the disaster.

In Pics: Massive quake in Chile

"The power of nature has again struck our country," Bachelet said, declaring six of Chile's 15 regions "catastrophe zones" in the aftermath of the 8.8-magnitude quake.

Highways in the South American nation of 16 million were sliced to pieces, bridges imploded and buildings collapsed as the earthquake struck at pre-dawn hours Saturday some 325 kilometers (200 miles) southwest of the capital Santiago.

"This is a catastrophe of immense proportions, so it will be very difficult to give precise figures," Interior Minister Edmundo Perez Yoma said. Officials later said at least 300 people had been killed.

Waves well over two meters (seven feet) high crashed into the Chilean coast after the quake struck at 3:34 am (0634 GMT) and tore out into the Pacific, killing at least five people in the remote Robinson Crusoe islands.

In the Chilean port of Talcahuano, trawlers were sent shooting inland to the town square where they lay oddly marooned next to abandoned cars.

About 50 countries and territories along an arc stretching from New Zealand to Japan braced for giant waves, five years after the Indian Ocean tsunami disaster that killed more than 220,000 people.

More than 70,000 people fled vulnerable coastal areas of Japan Sunday as a tsunami slammed into the country's long Pacific coastline.

"Please do not approach the coast at any cost," Prime Minister Yukio Hatoyama said in nationally televised comments as Japan, one of the world's most quake-prone nations, went on its first major tsunami alert in 15 years.

The first tsunami wave, 30 centimetres (one foot) high, hit Nemuro on the northern island of Hokkaido in the early afternoon, the Meteorological Agency said.

The massive quake plunged much of Santiago into darkness, snapping power lines, severing communications. The international airport was closed after sustaining significant damage to the terminal.

Many Chileans were still in nightclubs partying at the start of the weekend when the quake struck before dawn, ripping up roads, bringing roofs crashing down and toppling power lines.

"It was the worst experience of my life," said 22-year-old Sebastian, standing outside his house in eastern Santiago.

"Friends who were at clubs said it was pandemonium," said Santiago resident Maren Andrea Jimenez, an American expert working for the United Nations. "It was scary! Plaster began falling from the ceiling."

President Barack Obama said the United States "stands ready to assist in the rescue and recovery efforts, and we have resources that are positioned to deploy should the Chilean government ask for our help."

"Early indications are that hundreds of lives have been lost in Chile and damage is severe. On behalf of the American people, Michelle and I send our deepest condolences to the Chilean people," he said at the White House.

The total value of economic damage caused by the quake is likely to range between 15 billion and 30 billion dollars, a US risk modeling firm predicted.

Despite officials saying up to 1.5 million homes could be affected, Chile's Foreign Minister Mariano Fernandez asked countries that had offered aid to hold off until local authorities could assess the emergency needs.

Chile does not want "aid from anywhere to be a distraction" from disaster relief, Fernandez said, adding: "Any aid that arrives without having been determined to be needed really helps very little."

The European Union said it would provide three million euros (four million dollars) in immediate assistance. Unlike Haiti, struck by a devastating earthquake last month, Chile is one of Latin America's wealthiest countries.

The US Geological Survey said it had recorded more than 51 aftershocks ranging from 4.9 to 6.9 since the quake.

Earthquake-prone Chile lies along the Pacific rim of fire and is regularly rocked by quakes, but damage is often limited as they mostly hit in remote desert regions.

It was the second major earthquake to hit the Western hemisphere in seven weeks after more than 200,000 people were killed in Haiti last month by a 7.0-magnitude quake.

The epicentre was just a few hundred miles north of the biggest earthquake on record, a 9.5-magnitude monster in May 1960 that killed between 2,200 and 5,700 people and triggered a huge tsunami that reached as far as eastern New Zealand.
[ Read More ]

Joti wa ze comedy alazwa moi....


[t.JPG]
Msanii maarufu wa kundi la vichekesho la Orijino Komedi,Lukac Mhavile a.k.a Joti (pichani) anahofiwa kuvunjika shingo,baada ya kupata ajali alipokuwa akirekodi kipindi pamoja na wenzake eneo la daraja la Salender,jijini Dar.




Joti aligongwa na lori aina ya Scania malai ya Ubalaozi wa Ubelgiji nchini,saa 5:30 jana asubuhi.Amelazwa Taasisi ya Mifupa Muhimbili (MOI) kwa matibabu,akiwa amefungwa kifaa maalum cha kuzuia shingo kukunja na kugeuka.


Akizungumzia tukio hilo,Kamanda wa Polisi mkoa wa Kinondoni,Sebastian Masinde,alisema ajali hiyo ilitokea wakati msanii huyo akiwa na wenzake wakiigiza tukio lililodaiwa kutokea eneo hilo la Mwanamke kuoata Manyoya baada ya kumpa ombaomba pesa.


Alisema walipokuwa wakiigiza wakiwemo pia wasanii wenzake Masanja na Mpoki,ombaomba waliokuwa karibu walichachamaa na kuwazuia wasiigize ambapo katika kufanya hivyo waliwavamia na Joti na wenzake wakalazimika kukimbia.


"walipokuwa wakikimbia ndipo alipogongwa na gari,wamekasirika kwa sababu sasa mwenye kila gari lake anayepita pale anafunga vioo,hivyo hawakupenda Komedi waigize tukio hilo na kuanza kuwafukuza.
kamanada Masinde alisema kuwa baada ya tukio hilo, Majeruhi walipelekwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili ambako amelazwa MOI,na dereva wa Lori hilo anashikiliwa na polisi pamoja na gari lililosababisha ajali hiyo.
source michuzi.
[ Read More ]