Mtoto aliyenusurika kimiujiza kwenye ajali ya ndege ya Yemen Airways iliyodondoka kwenye bahari ya Hindi karibu na visiwa vya Komoro na kuua watu 152 ameelezea jinsi alivyonusurika kimiujiza kwenye ajali hiyo.Bahia Bakari mwenye umri wa miaka 14 ndiye abiria pekee aliyenusurika kwenye ajali ya ndege ya Yemenia, Airbus A310 iliyotokea alfajiri ya jumanne wiki hii.
Bahia aling'ang'ania mabaki ya ndege na kuelea juu yake kwa masaa 12 katika hali ya hewa mbaya na bahari ambayo imejaa papa wengi kabla ya waokoaji kufika na kumuopoa.
Mtoto huyo ambaye hali yake inaendelea vizuri baada ya kupewa matibabu nchini Komoro amerudi kwao Ufaransa kuungana na baba yake.
Kassim Bakari, baba wa msichana huyo, akiongea na vyombo vya habari vya Ufaransa alisema kuwa nilipoongea naye kwa simu aliniambia "Tuliona ndege ikiangukia kwenye maji, nilijikuta kwenye maji, niliwasikia watu wakiongea lakini sikuweza kumuona hata mtu mmoja. Nilikuwa kwenye kiza sikuona chochote".
"Baba sikuweza kuogelea vizuri, niling'ang'ania juu ya kitu, sijui ni kitu gani" alisema Bahia akimwambia baba yake.
Bakari ambaye ana watoto wengine watatu alisema kuwa aliposikia habari za ajali ya ndege hiyo, moja kwa moja alifikiria kuwa hatamwona tena mkewe na mtoto wake wa kwanza.
"Ni msichana mwenye aibu sana, sikufikiria kama angenusurika namna hii, Siwezi kusema hii ni miujiza bali ni matakwa ya mwenyezimungu" alisema Bakari.
Bakari alisema kuwa Bahia hadi sasa hajaambiwa kuwa mama yake amefariki.
"Walimwambia kuwa mama yako yupo chumba cha jirani ili kutomshtua lakini ukweli ni kwamba mama yake amefariki na sijui nani ataweza kumwambia" alisema baba wa mtoto huyo.
Waokoaji walimuokoa Bahia kwenye bahari ya Hindi kilomita 16 toka kwenye pwani ya Visiwa vya Komoro.
Waokoaji hao walisema kuwa Bahia alikuwa dhaifu sana wakati anaokolewa, hakuweza hata kulishika boya alilorushiwa na hivyo kumfanya mzamiaji kupiga mbizi na kumpandisha kwenye boti ambako alifunikwa na blanket na kupewa maji ya moto yenye sukari anywe wakati anawahishwa hospitali.
Watu wengi wamestaajabu jinsi mtoto huyo alivyonusurika ajali hiyo na kuelea kwa jumla ya masaa 12 kwenye bahari ambayo imejaa papa wengi tena akiwa hana hata life jacket.
Mwanamuziki mashuhuri wa Marekani, Diana Ross ametajwa katika wosia wa Michael Jackson kama mlezi wa watoto watatu wa Michael inapotokea mama yake Michael Jackson mwenye miaka 80 atakaposhindwa kuwaangalia.
Hayo yapo katoka Wosia wa Michael Jackson ulioandikwa mwaka 2002 ambao ulikuwa ukisubiriwa kwa hamu, ambapo ulitolewa jana katika mahakama kuu ya Los Angeles, katika wosia huo Michael Jackson hakumtaja mke wake wa zamani Debbie Rowe kuchukua nafasi yoyote ya kuwalea watoto hao.
Katika wosia huo Michael Jackson amesema ndoa yake na Debbie Rowe iliishavunjika na kiuhakika hali hiyo inamzuia Debbie kupata chochote kutoka kwa Michael Jackson.
Michael Jackson ameacha mali yenye thamani ya jumla ya dola za kimarekani zaidi ya milioni 500 kwa familia yake.
Michael Jackson amemtaja mama yake kuwa msimamizi mkuu na mlezi wa watoto wake watatu.
Wosia huo ulipelekwa mahakamani na mwanasheria wa zamani wa Michael Jackson aitwaye John Blanca na kiongozi wa wanamuziki wa zamani John Mclain ambao walikuwa marafiki wa Michael kibiashara, wote wawili katika wosia wa Michael wametajwa kuwa wasimamizi wa mirathi.
Hata hivyo, wosia huo umeshindwa kutoa mwongozo wa masuala kadhaa likiwemo la maziko ya Michael Jackson kwamba atazikwa vipi na wapi au kuhusu utajiri wake utagawanywa vipi.
Vyombo vya habari mbalimbali vilikuwa vikidai leo mwili wa marehemu Michael utaagwa na mazishi yatafanyika siku ya Jumapili taarifa ambazo familia ya marehemu imezikanusha, lakini hawajasema lini nguli huyo wa muziki atazikwa.
Diana Ross mwenye miaka 65 ambaye alikuwa rafiki wa Michael Jackson amesema ," Moyo wangu unauma sana kusikia kifo cha Michael, hivi sasa nipo katika sara kuwaombea watoto wa Michael na familia ya Jackson."
Mwanasheria wa Michael alisema alichelewa kupeleka wosia huo mahakamani kwa sababu alitaka familia ya Jackson kuupitia kwanza.
"Suala la msingi katika wosia huo ni kwamba Michael amemwandika mama yake kuwa msimamizi mkuu wa watoto wake kisheria,"alisema mwanasheria huyo aitwaye Blanca.
Wakati huo huo mtengeneza muziki mkongwe Quincy Jones amesema anaweza asihudhurie mazishi ya Michael Jackson.
Jones ambaye alimtengenezea Michael albamu tatu ambazo ni Thriller, Off the Wall na Bad, bado yupo katika huzuni kubwa kutokana na kifo hicho cha ghafla cha rafiki yake Michael Jackson.
Serikali ya Marekani imeingia katika zoezi la uchunguzi wa kifo cha Michael Jackson ambapo itawachunguza madaktari waliohusika na Michael, jinsi wanavyofanya kazi na vyanzo vyao vya kupata madawa.
Gregory McCalium kabla na baada ya kupewa kichapo na babu ambaye ni bondia mstaafu
Kibaka aliyezamia kwenye nyumba ya babu mmoja nchini Uingereza mwenye umri wa miaka 72 na kuanza kumtishia kwa kisu bila kujua kwamba babu huyo alikuwa ni bondia mstaafu, aliambulia kipigo kilichoichakaza sura yake.
Kibaka huyo Gregory McCalium mwenye umri wa miaka 24 mkazi wa wa Oxford nchini Uingereza, alivamia kwenye nyumba ya jirani yake ambayo babu huyo alikuwa akiishi na mke na kujaribu kuwapora mali zao bila kujua kwamba babu huyo alikuwa bondia mstaafu.
Babu Frank Corti mwenye umri wa miaka 72 alikuwa ni bondia maarufu enzi za ujana wake akiwa amejikusanyia vikombe kadhaa katika mashindano mbali mbali ya ndondi nchini Uingereza.
Picha iliyotolewa na polisi wa Uingereza ilionyesha jinsi sura ya kibaka huyo aliyekuwa na kisu ilivyoharibiwa vibaya na ngumi nzito za babu huyo.
Babu Corti baada ya kumwangushia kipondo McCalium alimlaza chini na kumlalia mpaka polisi walioitwa na mkewe walipokuja kumchukua.
Jumanne wiki hii McCalium alihukumiwa kwenda jela miaka minne na nusu kwa kosa hilo la jinai.
"Mwanzo nilishtuka aliporusha kisu chake, lakini kama watu wengine jinsi ambavyo wangejihami na mimi niliamua kufanya hivyo" alisema Corti.
"Umepata ulichostahili" alisema mwendesha mashtaka Angela Morris akimwambia McCalium wakati akisomewa mashtaka yake mahakamani hapo.
Tukio hilo lililotokea mida ya asubuhi lilimwacha kibaka McCallium akiwa amepasuliwa chini ya jicho lake na amechanika mdomo wake.
ZOEZI la kusajili simu za mkononi kwa wananchi linaanza leo rasmi ili kudhibiti wimbi la wizi la bidhaa hizo nchini.
Zoezi hilo liliazimiwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania [|TCRA] ili kuondoa kero zote zinazohusiana na zinazotokana na simu hizo za mkononi nchini.
Akitoa tamko hilo rasmi Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania, John Nkoma amesema kuwa zoezi hilo litaanza leo Julai Mosi, la kusajili kadi za simu za mkononi kwa wananchi.
Amesema kuwa lengo la kusajili kadi hizo ni kudhibiti matumizi mabaya ya simu yanayofanywa na wananchi vilevile ikiwemo na kupunguza wimbi la simu hizo ili kulinda maslahi ya mtumiaji.
Amesema ili kudhibiti matumizi mabaya ya simu sasa kila mwenye simu ya mkononi lazima ajiandikishe.
Amesema kila mwenye simu ya mkononi ni lazima ajiandikishe kwa kutumia vitambulisho maalumu vya kupigia kura, Passport ya kusafiria, kitambulisho cha mfuko wa pensheni, leseni za udereva.
Pia kwa wenye vitambulisho vya Saccos, Benki, ajira, kitambulisho cha chuo cha elimu ya juu, barua ya mwajiri na kama hivyo vyote hana unatakiwa uwe na barua ya serikali za mitaaa.
Amesema zoezi hilo linatarajiwa kufanyika kwa kipindi cha miezi sita na lengo la kusajili kadi hizo wananchi watakuja kutambua faida yake kwa wale ambao wanaona ni haisaidii.
Amesema kuwa wananchi wamekuwa wakitukanana kwa maneno mabovu kwa kununua namba na kuitupa pia kupeana maneno ya kutishana na kumekuwa kumeshamiri sana wizi wa simu hizo.
Amesema namba ya kadi ikishasajiliwa basi hata kama mtu akiiba simu hiyo hataweza kuitumia na matokeo yake ataitupa.
Mtoto wa miaka 14 ndiyo mtu pekee aliyenusurika kwenye ajali ya ndege ya Yemen Airways (Yemenia) ambayo ilidondoka jana kwenye bahari ya hindi ikiwa na jumla ya watu 153.
Waokoaji walisema kwamba msichana mwenye umri wa miaka 14 alikutwa akielea kwenye bahari ya Hindi kilomita 16 kutoka kwenye pwani ya visiwa vya Komoro.
Taarifa zilisema kwamba binti huyo aliyejulikana kwa jina lake la kwanza Bahia alikuwa akisafiri pamoja na mama yake.
Hali ya mtoto huyo inaendelea vizuri kwenye hospitali aliyolazwa kwenye visiwa hivyo.
"Anaendelea vizuri na aliweza kuongea na mamlaka husika na kuwaelezea kilichotokea" alisema msemaji wa timu ya waokoaji.
Taarifa za awali zilisema kwamba msichana huyo alikuwa na umri wa miaka mitano lakini msemaji huyo alikanusha taarifa hizo.
Ndege ya Yemen Airways (Yemenia) ilidondoka na kuzama kwenye bahari ya Hindi jana karibu na visiwa vya Komoro wakati ikitokea Ufaransa kuelekea Moroni, mji mkuu wa Komoro kwa kupitia Yemen ikiwa na abiria 153.
Watu wengi waliofariki ni raia wa Ufaransa na Umoja wa Ulaya ulisema ulikuwa na mpango wa kuzipiga marufuku kwenye anga ya ulaya ndege za Yemenia ambazo zimekosolewa sana kwa kuvunja taratibu za usalama.
Hii ni ajali ya pili ya ndege ambayo imepoteza maisha ya raia wengi wa Ufaransa ikiwa ni wiki chache baada ya ndege ya Ufaransa, Air France iliyokuwa ikitokea Brazili kuelekea Ufaransa ikiwa na abiria 228 kudondoka kwenye bahari ya Atlantic na kuua watu wote waliokuwemo kwenye ndege hiyo.
Yemenia kutokana na baadhi ya ndege zake kupigwa marufuku nchini Ufaransa ilikuwa ikitumia ndege zake mpya kwaajili ya nchi za ulaya na ndege zake za zamani kwaajili ya safari zake katika nchi za Afrika na kwingineko ambako hawakupewa masharti ya usalama wa ndege zao.
Ndege iliyotoka Ufaransa ilikuwa ni mojawapo ya ndege mpya za Yemenia na ndege hiyo ilipofika Yemen, abiria walibadilisha ndege na kupandishwa ndege hiyo ya zamani iliyokuwa inakuja Afrika ambayo ilipigwa marufuku nchini Ufaransa kutokana na matatizo yake mbali mbali.
AT the tender age of 12, Vicky Jaggers cradled her newborn daughter Kirsty for the very first time.
Becoming a mother at such a young age life was always going to be difficult - but Vicky was also burdened by a horrific secret.
Her 17-year-old brother David was Kirsty's father - having RAPED Vicky several times in a matter of months.
Vicky vowed to keep the devastating truth to herself to protect her family.
Pain ... Vicky at 14 with Kirsty
Eastnews Press
But after 18 harrowing years, she bravely decided in 2004 to reveal the sickening secret to the police after monster David Jaggers, now 39, was arrested for the rape and kidnap of his then girlfriend.
DNA tests proved that David was Kirsty's father and, with Vicky courageously testifying against her sadistic brother, he is now serving a life sentence for his crimes.
Determined to give other rape survivors a voice, Vicky has now written about her ordeal in an autobiography called Silenced.
The 34-year-old says: "The evil abuse David inflicted on me ruined my young life. I had to lie to my family for 18 years about Kirsty's father, as I thought telling my parents would destroy them.
"However, there is one good thing to come out of my horrific story - Kirsty."
Vile David brutally snatched away Vicky's innocence when she was just 12.
As she slept in her room above the pub owned by their mum Avril, now 63, and dad Len, who passed away in 1994, David climbed into Vicky's bed and raped her.
Vicky says: "I had no idea what he was doing - it seemed so unreal.
"Obviously I was a virgin and knew hardly anything about sex - but I knew what David was doing was very wrong.
"I can remember being in agony, but also too terrified to scream out.
Terrible
"It seemed to go on for ever and when the attack was finally over David simply got out of bed and left - shutting my bedroom door like nothing had happened.
"I cried all night and pushed my cupboard in front of my door in case he came back. The next morning I was desperate to say something to Mum and Dad.
"But when I saw David, his expression told me that if I said a word, he would kill me. So my parents had no idea about the horror that had occurred."
Over the following months, David raped Vicky twice more - on both occasions sneaking into her bedroom while she slept.
Vicky, from Tilbury, Essex, says: "I felt dirty and useless. The next day, I would sit in the bath for hours and try to scrub myself clean. But nothing could wash away the memories of those terrible attacks."
Shortly after his last attack, David left the family home to move in with friends.
Vicky explains: "It was a relief to have him out of the house. I hoped to be rid of him for ever. At that point, I had no idea I was carrying his child."
In fact, Vicky did not know she was pregnant until three months before the birth. After she suffered stomach pains, a doctor found she was six months pregnant.
Vicky says: "I was big as a child and always wore baggy jumpers, so no one had noticed my growing stomach.
"Hearing I was six months pregnant was devastating and knowing it was David's baby made me feel physically sick."
Hope ... Vicky is looking to the future with new man Kelly
Eastnews Press
Even then, Vicky did not tell her parents who the real father was - claiming it was a boy she had met the previous summer at a caravan park.
She says: "It was heartbreaking to see their disappointment. I was desperate to tell them the truth but thought they might think badly of me.
"I was 12, terrified and about to be a mother to my brother's child."
In July 1987, Vicky gave birth to Kirsty and decided not to put her up for adoption.
She says: "I was lucky enough to have my parents' support and even though I knew the terrible secret of Kirsty's real father, my heart filled with love for her."
A year after the birth, Vicky saw David again, when he moved closer to the family home. She says: "It made my stomach turn. He looked sleazy and had a constant lazy grin on his face which twitched.
"He made my skin crawl. When he looked at Kirsty, he didn't show any interest. He must have known she was his, but thankfully he didn't want to go near her."
In 1989, David was arrested for strangling his girlfriend, 23-year-old Helen Mitchell, to death after an argument.
He propped up her body on the sofa and sat with her all night, before leaving in the morning without reporting the crime.
He denied murder but was convicted of manslaughter and jailed for six years.
Over the following years, Vicky had a number of destructive relationships with other men and gave birth to four more children - Alicia, now 17, Sam, 16, Jamie, ten, and eight-year-old Kirk.
But Vicky's life finally changed for the better seven years ago when she met the man she calls her "knight in shining armour" - Kelly, 39, currently unemployed.
She says: "For the first time, I was with a man who truly cared for me and wanted to be a father to my children."
The couple married in August 2002 but however close she got to Kelly, Vicky still felt she could not tell him about the abuse she endured at the hands of her brother. But in December 2004, another shocking twist made Vicky realise she had to open up to her loved ones - and the police.
A nationwide hunt had been launched for David after he kidnapped and raped another girlfriend. Holding her prisoner in his van for three days, he repeatedly raped and beat her.
Evil
Vicky recalls: "This was the breaking point. I knew David would be punished, but the court needed to know the true extent of his evil. I had to come forward."
Rapist ... David in 2004
Vicky decided she first had to tell Kelly, mum Avril and daughter Kirsty.
She says: "I was terrified about their reaction and sobbed hysterically while I spoke. Through the tears, I could only say the words 'rape, David' and 'Kirsty's dad'.
"It was awful to see the hurt on their faces but it was also such a relief - 18 years after David raped me I could finally speak the truth. Mum was devastated and apologised for not looking after me but there was nothing she could have done. Kirsty was in shock and was speechless that her killer uncle was also her father."
After telling the family, Vicky went to the police, who took DNA samples that proved David was Kirsty's dad.
Because of Vicky's brave decision, David admitted two charges of raping her when he appeared at Basildon Crown Court, Essex, in 2005.
Shockingly, he was given just a one-year jail sentence on each count.
He also admitted raping his girlfriend, making threats to kill, false imprisonment and kidnap and was given a life sentence but with a minimum term of just six years.
Vicky says: "When he does come out, I know I will always be protected by my amazing, loving family - something David will never have."
Kirsty, now 21, who has luckily not suffered any health problems despite having parents who are blood relatives, says: "I'm so proud of Mum. She has been through a horrific time, but has always done her best to be a great mum.
"Her brave decision hopefully means David will not be able to hurt any other women."
Binti mmoja wa nchini Pakistan ambaye alitoroka nyumbani kwao na kwenda kuolewa bila ya idhini ya wazazi wake ameuliwa yeye na mumewe kwa kupigwa risasi na ndugu zake ambao walidai wanasafisha aibu iliyowekwa na binti huyo.Ndugu wa binti huyo wakiwa wamevalia unifomu za polisi walivamia nyumba aliyokimbilia binti huyo baada ya kuolewa kisiri na kuwaua watu wote waliokuwemo ndani ya nyumba hiyo.
Polisi wa Pakistan walisema kwamba kundi kubwa la ndugu wa binti huyo walivamia nyumba ambayo binti huyo na mumewe walikuwa wakikaa kwenye kitongoji cha Charsadda, kilichopo kaskazini magharibi mwa Pakistani.
"Kundi hilo lilimchukua bwana harusi na kumtoa nje ya nyumba hiyo kabla ya kumuua kwa kumpiga risasi, wakati baadhi yao wakiingia ndani na kumuua bi harusi, mama na dada wa bwana harusi" alisema afisa wa polisi wa eneo hilo.
"Waliwapiga kwanza kisha wakawaua kwa kuwapiga risasi" alisema afisa huyo.
"Baba wa bwana harusi naye aliuliwa" alisema afisa mwingine wa polisi alipohojiwa na shirika la habari la AFP.
Bi harusi alikuwa na umri wa miaka 19 wakati bwana harusi alikuwa na umri wa miaka 29.
Polisi walisema kwamba binti huyo wa kitongoji cha jirani alikimbia nyumbani kwao na kwenda kuolewa kwenye kitongoji hicho bila ya ruhusa ya wazazi wake.
"Walikuwa wameoana wiki chache tu zilizopita" alisema mjomba wa bwana harusi Misal Khan wakati akihojiwa kwenye eneo la tukio.
Kundi la ndugu wa bi harusi inasemekana liliongozwa na wajomba na binamu zake ambao walifanya mauaji hayo kwa madai ya kusafisha heshima ya ukoo wao.
Polisi walisema kwamba wamewakamata ndugu wa binti huyo na watu walioambatana nao kuwasaidia kufanya mauaji hayo.
Shirika la kutetea haki za binadamu limekuwa likipinga mauji yanayofanywa nchini humo kwa madai ya kulinda heshima ya familia.
Wanawake wanaobakwa au wanaopata mimba kabla ya ndoa wamekuwa wakiuliwa nchini humo kwa madai kwamba wanaitia aibu familia.
Mwaka 2005 rais wa wakati huo wa Pakistan, Pervez Musharaf aliamuru adhabu ya kifo kwa watu watakaofanya mauaji kwa madai ya kurudisha heshima ya familia zao.
Msichana mmoja wa nchini Tunisia amejiua kwa kumeza vidonge kutokana na huzuni ya kifo cha Michael Jackson huku ikikadiriwa kuwa jumla ya washabiki 12 wa Michael Jackson kutoka sehemu mbali mbali duniani wameishajiua tangia kutangazwa kwa kifo chake.Msichana huyo wa mji wa El Manar uliopo kaskazini mwa Tunia alijiua kwa kunywa vidonge vingi sana baada ya kugubikwa na huzuni kubwa tangia habari za kifo cha Michael Jackson zilipotangazwa.
Taarifa zilizema kwamba msichana huyo alitumia siku nzima akiwa amejifungia chumbani kwake akiangalia video za Michael Jackson kabla ya kuamua kunywa vidonge hivyo na kufariki.
Michael Jackson alifanya shoo yake ya kwanza kabisa barani Afrika nchini Tunisia mwaka 1996 iliyohudhuriwa na washabiki wake 65,000.
Jumla ya watu 12 washabiki wakereketwa wa Michael Jackson kutoka sehemu mbali mbali duniani inasemekana wamejiua baada ya kutangazwa habari za kifo cha Michael Jackson.
Gary Taylor, rais na mmiliki wa tovuti ya MJJcommunity.com, iliyoanzishwa miaka kumi iliyopita alisema kwamba anavyofahamu hadi sasa washabiki 12 wa Michael Jackson ambao walihuzishwa sana na kifo chake wamejiua.
"Ninavyofahamu ni kwamba watu 12 wamejiua sehemu mbali mbali duniani, mmoja wapo ni raia wa Uingereza" alisema Taylor.
"Hali imekuwa mbaya, watu wanachukua uamuzi wa haraka ambao Michael asingetaka washabiki wake wauchukue, angewataka waendelee kuishi", alisema Taylor.
Jesse Jackson, rafiki wa karibu wa Michael ametoa video kwenye YouTube akiwataka washabiki wa Michael wasijidhuru.
Wakati huo huo taarifa za kutoka nchini Urusi zilisema kwamba mwanaume mmoja aliyejulikana kwa jina la Pável Talaláyev alijaribu kujiua muda mfupi baada ya kutangazwa kwa kifo chake na baada ya jitihada kubwa za madaktari kunusuru maisha yake alipozinduka alianza kuwalaumu madaktari kwa kumuokoa na kusema "Hili ni pigo kubwa sana kwangu, sitaki kuishi tena sijui kwanini wameniokoa nataka nikawe pamoja na Michael".
TAARIFA mpya za uchunguzi wa kifo cha msanii Michael Jackson zimeonyesha matokeo ambayo yanashangaza kwa kiasi kikubwa.
Vyombo mbalimbali vya habari ulimwenguni vimefichua kuwa msanii huyo alikuwa amedhoofika kiasi cha kutisha na kubakia mifupa kutokana na kutokula na kisha kutumia kiasi kikubwa cha vidonge.
Uchunguzi huo umeonyesha kuwa baada ya kifo chake mabaki ya baadhi ya vidonge hivyo yamekutwa tumboni mwake.
Mwili wake, uchunguzi huo umebaini kuwa ulikuwa umedhoofu kiasi kwamba kiuno, mapaja na mabega yake yalikuwa na matundo ya vidonda vingi vya sindano, vinavyodhaniwa kuwa ni vya sindano za kutuliza na kuondoa maumivu ambazo alichomwa mara tatu kutwa, tena kwa miaka mngi.
Pia, amekutwa na makovu mengi yaliyotokana na upasuaji wa mara 13 ailiofanyiwa kwa ajili ya kubadili sura yake.
Wataalam hao wamegundua uchunguzi wa kusikitisha wenye kuonyesha kuwa msanii huyo, Wacko Jacko hali yake ilikuwa imedhoofu wakati mauti yakimkuta wiki iliyopita mjini Los Angeles.
Uchunguzi huo umeonyesha kuwa licha ya kuwa na urefu wa futi tano na inchi 10, lakini msanii huyo alikuwa amepungua uzito na kubakia na kilo chache ambazo hazilingani na urefu wake.
Wataalam hao wanaeleza kuwa alikuwa akila mlo mmoja kutwa, kiasi kwamba wakati akifariki tumbo lake lilikuwa tupu, mabaki ya vidonge vilivyoanza kusagika ambavyo alitumia na sindano ambazo hatimaye zilisababisha moyo wake kusimama. Sampuli zaidi zimechukuliwa kwa ajili ya uchunguzi zaidi.
Kichwani, Wacko Jacko alikuwa amepoteza nywele karibu zote. Mfalme huyo wa pop, uchunguzi umeonyesha kuwa alikuwa akivaa nywele bandia, ambazo wachunguzi hawakuwa na kazi ya kuziondoa kwa ajili ya uchunguzi wao.
Kichwani mwake, upande wa sikio la kushoto, alikuwa na jeraha kubwa ambalo liliacha upara kutokana na ajali ya mwaka 1984 wakati alipoungua moto akipiga picha ya filamu ya tangazo la Kampuni ya Pepso.
Mwili mwake, wachunguzi hao wamebaini kuwa alikuwa amevunjika mbavu kadhaa, ikiaminika kuwa zilitokana na juhudi za kujaribu kuokoa maisha yake baada ya kuzimia. Matundu manne ya sindano yamegundulika karibu na moyo wa msanii huyo.
Uchunguzi huo umeonyesha kuwa harakati za kumwokoa ndizo zilizomsababishia madhara hayo yakiwamo ya sindano tatu zilizochomwa na kupenya ukuta wa moyo wake, kumsababisha madhara.
Katika uchunguzi huo, imeonekana kuwa magoti ya Jackson na sehemu ya mbele ya ugoko wake zilikuwa na majeraha kama ilivyokuwa mgongoni mwake.
Daktari wake binafsi, Conrad Murray, ambaye alikuwa karibu na msanii huyo amekamatwa na kuhojiwa huku familia ya msanii huyo ikieleza kuwa inataka uchunguzi zaidi unatakiwa kufanyika.
Dk Murray, ndiye anayeaminika kumpiga sindano msanii huyo kabla ya umauti kumkuta, akiaminika kumpa dawa iitwayo Demerol, jambo ambalo limemwingiza katika mzozo wa kitibabu.
Rafiki wa karibu wa familia, Mchungaji Jesse Jackson alieleza wasiwasi kuhusu chanzo cha kifo cha msanii huyo na kutaka uchunguzi zaidi na mtaalam, Dk Murray ambaye alikodiwa na Kampuni ya AEG Live , ambayo ilikuwa na jukumu la kuandaa matamasha 50 ya msanii huyo, katika ukumbi wa O2 Arena, London mwezi ujao, achunguzwe zaidi.
MHADHIRI mwandamizi wa Chuo Kikuu Cha Dar-es-Salaam, Professa Haroub Miraji Othman, 66, amefariki dunia usiku wa kuamkia jana katika hoteli ya Abuso Shangani mjini Zanzibar.
Kwa mujibu wa msemaji wa familia hiyo, Ali Uki alisema kifo cha Professa Othuman kilitokea ghafla akiwa usingizini. Alisema wakati mkewe akimuasha, alistuka alipoona Dk Othman haamki na ndipo alipoita watu kumsaidia.
Alisema mkewe pia aliomba msaada wa kuitiwa daktari ili aende kumpima na kuthibitisha kwamba taarifa za kuthibitisha kifo chake zilitolewa majira ya saa 1:30 asubuhi.
Professa Othman alifika mjini hapa juzi asubuhi akitokea Dar es Salaam kwa ajili ya kuhudhuria uzinduzi wa kitabu kilichotungwa na Professa Thomas Burgess, Ali Sultan Issa na Maalim Seif Sharif Hamad kiitwacho ‘Race Revolution and the Struggle for Human Rights in Zanzibar".
Hafla hiyo ilifanyika kwenye ukumbi mpya wa Al- Yamin Funguni mjini hapa na baadaye kuhudhuria uzinduzi wa Tamasha la Nchi za Jahazi (ZIFF) hadi majira ya saa 6:00 usiku baadaye kwenda hoteli ya Abuso iliyo Mji Mkongwe akiwa na mkewe Professa Saida Yahya Othman.
“Professa hakuwa anaumwa jana... si mlimuona alivyokuwa katika usinduzi wa kitabu asubuhi na usiku alikuwa katika uzinduzi wa tamasha la ZIFF. Amefariki alfajiri; kwa hakika kila mtu yatamfika mauti yeye ametangulia na sisi tupo nyuma yake ndio ameshatutoka, tunachofanya sasa ni kuwasiliana na jamaa kwa ajili ya matayarisho ya mazishi,” alisema msemaji huyo.
Makamu mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Professa Rwekaza Mukandala alisema Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kimestushwa na kifo cha mhadhiri huyo na kumuelezea kuwa ni mtu asiyechoka na mchapakazi mzuri.
Profesa Othman atazikwa leo jioni na mipango ya mazishi inafanyika nyumbani kwake eneo la Baraste - Michenzani. Habari zinasema atazikwa pembeni kwa kaburi la mama yake mkoa wa Mjini Zanzibar.
Mhadhiri huyo atakumbukwa kwa msimamo wake na heshima aliyokuwa amejijengea kitaaluma katika sheria za kimataifa, masuala ya maendeleo na diplomasia.
Hakusita kuwakosoa viongozi wa serikali ya Jamhuri ya Muungano na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) wakati zilipokuwa zikienda kombo.
Mkuu wa Taasisi ya Mawasiliano ya Umma, Dk Bernadetta Killian alisema kuwa amestushwa na kifo cha mhadhiri mwenzake katika chuo kikuu cha Dar es Salaam.
Mgeni rasmi katika uzinduzi wa tamasha hilo la ZIFF alikuwa Waziri Kiongozi wa SMZ, Shamsi Vuai Nahodha na tamasha hilo lilikuwa likirushwa moja kwa moja na kituo cha televisheni cha serikali, TVZ.
Hadi mauti yanamfika, Professa Othman alikuwa mwenyekiti na muanzilishi wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ambacho kilianzishwa kwa ajili ya kutoa msaada wa kisheria kwa watu wenye kipato cha chini.
Mara baada ya kumaliza masomo yake ya juu nchini Urusi, Prof Haroub alirejea Zanzibar lakini hakupata ajira na kufanyiwa mipango na serikali kwenda kufanya kazi Bara.
Professa Othman alikuwa akifanya kazi katika kitivo cha sheria cha UDSM kuanzia miaka ya sabini na amefariki akiwa mhadhiri mwandamizi.
Mbali na elimu yake, Professa Othman alikuwa mstari wa mbele katika kupigania haki na ameshawahi kuteuliwa katika tume mbalimbali, ikiwemo ya kufanya marekebisho ya katiba na tume ya Nyalali.
Tume ya Nyalali ilikuwa ikiangalia mfumo unaofaa kisiasa nchini wakati dunia ikiwa kwenye mageuzi ya kisiasa na kiuchumi baada ya kumalizika kwa vita baridi kati ya mataifa ya mashariki na magharibi. Aliwahi kuwa mwenyekiti wa bodi ya iliyokuwa Shirika la Habari la Tanzania (Shihata) katika mwaka 1995.
Katika kipindi cha uchaguzi mkuu wa kwanza katika mfumo wa vyama vingi, Prof Othman alikuwa mwenyekiti wa taasisi ya wangaalizi wa ndani wa uchaguzi ambayo iliingia katika lawama kubwa baada ya kusema uchaguzi mkuu wa Zanzibar wa mwaka 1995 haukuwa huru na haki jambo ambalo lilimsababishia kuwekewa chuki na baadhi ya viongozi wa Zanzibar kutokana na msimamo huo.
Waangalizi waliokuwa chini ya Professa Othman walitoa taarifa ya kwamba uchaguzi mkuu wa mwaka 1995 haukuwa huru na haki tofauti na taarifa ya Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC).
Mwezi uliopita alihudhuria semina iliyowakutanisha waandishi wa habari waandamizi kuhusu jinsi ya kuhakikisha chaguzi zinazofuata zinakuwa huru na haki bila ya kutawaliwa na fujo pamoja na kutoa mafunzo ya sheria za kimataifa na haki za binaadamu kwa makamanda na wakuu vya vyuo vya mafunzo Zanzibar, ikiwa ni hatua moja ya kuwaelimisha juu ya masuala ya ukiukwaji wa haki za binaadamu.
"Nikiwa hai inshaallah nataka kushuhudia uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 unafuata misingi yote ya demokrasia na haki za binadamu, zaidi kwa vyombo vya habari," alisema Prof Othman katika semina hiyo.
Akizungumzia kifo hicho, Mwanadiplomasia Dk. Salim Ahmed Salim na katibu mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad walieleza kupokea taarifa hizo kwa mshituko mkubwa na kwamba msomi huyo atakumbukwa kwa mengi, lakini wakasema kubwa zaidi ni utetezi wake kwa wanyonge na kupigania haki za binaadamu.
Naye Prof Abdallah Safari alisema amepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za kifo cha msomi huyo na kuelezea kifo chake kuwa ni msiba mkubwa kwa wanataaluma na jamii kwa ujumla.
"Unajua pengo la Prof Haroub ni kubwa na si kirahisi kuzibika katika Chuo kikuu cha Dar es Salaam kwa sababu kifo cha mwanataaluma siku zote pengo lake huwa kubwa sana," alisema Profesa Safari.
Alimfananisha Prof Haroub na wanafalsafa wa zamani kama Walter Rodney, aliyeandika kitabu kinachoelezea jinsi Ulaya ilivyorudisha nyuma maendeleo ya kiuchumi ya Afrika, na kwamba dunia imempoteza mwanadiplomasia mkubwa.
"Kwa Tanzania ukitaka uchambuzi mzuri wa migogoro hususan ya Mashariki ya Kati, Afrika na nchi nyingine, basi bila ya kumpata Profesa Haroub ni vigumu kupata uchambuzi uliokamilika," alisema.
Alisema hii ni wiki ya misiba mikubwa kwa sababu Tanzania imempoteza Sheikh Suleiman Mohamed Gorogosi, aliyefariki kwa ajali ya gari na mwanamuziki nyota wa miondoko ya pop, Michael Jackson wa Marekani.
Alimkumbuka Prof Othman wakati alipofundisha katika miaka ya sabini akiwa UDSM na kuelezea kuwa walikuwa na uhusiano mzuri.
Prof Othman alikuwa mstari wa mbele kuikosoa SMZdhidi ya ukandamizaji na ukiukwaji wa haki za raia.
Prof Othman ameacha mjane ambaye ni Professa Saida Othman na mtoto mmoja, Tahir Othman.