Banner 468

1234453_10201664080105694_1716282793_n
Facebook

AU yatofautiana na The Hague



Umoja wa Afrika umesema unasitisha ushirikiano na mahakama ya kimataifa inayoshughulikia uhalifu wa kivita, kuhusiana na uamuzi wa mahakama hiyo wa kumshtaki Rais wa Sudan Omar Al- Bashir.

Rais Omar Al- Bashir alishtakiwa kwa madai ya ukatili dhidi ya raia katika eneo la Darfur, magharibi mwa Sudan mwezi wa tatu.

Lakini wajumbe katika mkutano wa AU uliofanyika nchini Libya walikubaliana kuhusu azimio linalosema hawatatoa ushirikiano katika kukamatwa kwa Rais Bashir.

Wadadisi wanasema hatua hiyo ina maana kwamba rais Bashir anaweza kusafiri popote barani Afrika ya hofu ya kukamatwa.

Serikali ya Sudan imekuwa ikipigana na waasi katika jimbo la Darfur tangu mwaka 2003.

Mahakama ya ICC inamshtaki Rais Bashir kwa makosa mawili ya uhalifu wa kivita ; kuagiza kushambuliwa kwa raia na uporaji , pamoja na mashtaka mengine matano ya uhalifu dhidi ya binadamu , mkiwemo mauaji , ubakaji na utesaji , yote hayo yakihusishwa na mzozo huo.

Ameyakanusha mashtaka hayo yote , akisema serikali inao wajibu wa kupambana na makundi ya waasi.

Kwenye taarifa , AU imeeleza kwamba ombi lake la kuitaka mahakama ya ICC iliyoko mjini The Hague isimamishe kwa muda hoja hiyo ya kukamatwa kwa Rais Bashir limepuuzwa.

Taarifa jiyo inasema : '' Umoja wa Afrika hautatoa ushirikiano kuhusiana na hoja ya kukamatwa au kujisalimisha kwa Rais wa Sudan Omar Al- Bashir kwa mahakama ya ICC.''

Mwandishi wa BBC anasema ingawa taarifa hiyo imeungwa mkono na viongozi wengi wa Afrika , bado kuna nchi kadhaa , zikiwemo Chad na Benin ambazo zinaonekana kutoridhishwa na kauli hiyo.

Pia kumekuwa na maswali kuhusu taarifa hiyo, kwa sababu haijazitaka nchi 30 zilizotia sahihi ya kuundwa kwa mahakama ya ICC kusitisha uhusiano na mahakama hiyo.

Uamuzi huo ulifanyika katika siku ambapo Kenya imekubali kuendelea kushirikiana na mahakama hiyo ya ICC , kuwashtaki wale wanaotuhumiwa kwa kuchochea ghasia zilizofuatia uchaguzi wa mwezi Disemba mwaka 2007.

[ Read More ]

Ajali zaua watatu Jijini

Watu wa watatu wamefariki dunia na mmoja kujeruhiwa vibaya katika ajali za barabarani zilizotokea katika maeneo tofauti Jijini Dar es Salaam jana.

Akizungumzia kuhusiana na tukio la kwanza, Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni, Mark Kalunguyeye amesema lilitokea saa 9:30 usiku wa kuamkia jana katika barabara ya Haile Selasi, maeneo ya Oysterbay na kulihusisha gari aina saloon lenye namba za usajili T 555 AJV.

Amewataja waliofariki kuwa ni dereva wa gari hilo na mkazi wa Upanga, Jalvad Gama , 32 na abiria mmoja mkazi wa Masaki aliyetambuliwa kwa jina la Sailen Gilan, 50. Amesema katika ajali hiyo mtu mmoja aitwaye Gurminber Jandu , 30 alijeruhiwa.

Kamanda Kalunguyeye amesema ajali hiyo ilitokea baada ya dereva aliyekuwa akitokea Masaki kwenda barabara ya Ali Hassan Mwinyi, kushindwa kulimudu gari na kugonga mti.

Amesema miili ya watu hao imehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti cha Hospitali ya Aghakhan.

Amesema majeruhi huyo ambaye ni mkazi wa Masaki na fundi magari, anaendelea na matibabu katika hospitali ya Aghakhan.

Katika tukio la pili, Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi wa Ilala, Faustine Shilogile amesema mwenda kwa miguu mmoja amefariki dunia baada ya kugongwa na gari lisilofahamika.

Amesema ajali hiyo ilitokea jana saa 12:15 asubuhi katika eneo la Tazara wakati mwenda kwa mguu huyo ambaye ni mwanamke anayekadiriwa kuwa na umri wa kati ya miaka 30-35, alipokuwa akivuka barabara ya Nyerere.

Amesema gari wala dereva aliyemgonga hakufahamika na kwamba mwili wa marehemu umehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti cha Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.

[ Read More ]

Michael Jackson: Mazishi yake dili



Mazishi ya Mfalme wa Pop Duniani Michael Jackson yamegeuka kuwa 'dili' la aina yake baada ya watu kibao kugombea nafasi ya kuhudhuria shughuli hiyo.

Taarifa zinaeleza kuwa hadi sasa, zaidi ya watu 500,000 wamejisajili kwa ajili ya kucheza bahati nasibu ya kuwania tiketi kiduchu, zinazotajwa kuwa ni 17,500 pekee ili kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa Michael Jackson.

Uwanja wa mpira wa kikapu wa Staples Center Jijini Los Angeles ndio utakaotumika Jumanne ijayo kwa shughuli za kumuaga mwanamuziki huyo aliyefariki ghafla Alhamisi iliyopita.

Hata hivyo, wakati watu kibao wakiwania kushiriki mazishi ya mfalme huyo wa pop duniani, familia yake bado haijaeleza ni siku gani hasa atazikwa.

[ Read More ]

Aliyedaiwa kufa aibuka msibani,

KIJANA Frank Mboma (19) aliyedaiwa kufa katika mji wa Mbalizi kwa kupigwa na wananchi wenye hasira na kuzikwa eneo hilo juzi alizua tafrani baada ya kuibuka msibani akitokea Tunduma.

Sakataka hilo lilitokea Jumatano wiki hii katika kijiji cha DDC mji mdogo wa Mbalizi Wilaya ya Mbeya Vijijini baada ya kijana huyo kufika nyumbani kwao na kukuta watu wameweka tanga.

Kitendo hicho kilizua tafrani na waombolezaji hao kutimua mbio wakidhani muzimu umeibuka.

Majira baada ya kusikia taarifa hizo, lilifuatilia hadi kijijini hapo, umbali wa kilomita 15 kutoka Mbeya mjini kujionea kulikoni.

Akithibitisha kutokea tukio hilo Mwenyekiti wa kijiji hicho, Bw. Joines Mwalusanya, alisema kifo hicho kilitokea June 27 mwaka.

Alisema walipelekewa taarifa ofisi ya kijiji kuwa kuna kijana amepigwa na wananchi wenye hasira na amefia Hospitali ya Rufaa Mbeya.

Alisema waliambatana na ndugu wa kijana huyo kwenda kutambua maiti Hospitali ya Rufaa Mbeya na kubaini kuwa marehemu huyo alikuwa ni Frank.

Hata hivyo, alisema babu wa kijana huyo Mzee Joyasi Mboma alikataa kuwa kijana huyo si mjukuu wake Frank kutokana na kuonesha tofauti za sehemu fulani mwilini japo alionekana kufanana naye kwa sehemu kubwa.


Baadaye alisema bibi wa kijana huyo na kinyozi aliyekuwa amemnyoa, walithibitisha kuwa ndiye na kuamua kuchukua kibali Polisi na kuzika Juni 29 jioni na kuendelea na matanga nyumbani kwa Mzee Mboma eneo hilo la DDC.

Naye Mzee Mboma ambaye amemlea kijana huyo akitoa maelezo yake kwa waandishi wa habari alisema mjukuu wake aliondoka wiki moja kwenda Tunduma kutafuta maisha hadi aliposikia habari kwamba kuna maiti inayofanana naye na baada ya utata alikubali kuzika mwili huo.


Alisema kuwa alishangaa Jumatano kufuatwa na watu na kuambiwa mjukuu wake amefika eneo jirani na kwake na anaogopa kuingia ndani baada ya kuambiwa alikuwa amekufa na kuzikwa na watu wamekusanyika kwa ajili ya msiba wake.


"Nilikwenda ingawa ilikuwa usiku wa manane, nilishangaa kumkuta Frank akiwa hai. Nilimchukua na kuingia naye ndani, baada
ya kumhoji tuligundua kuwa ni mjukuu wangu na tuliyemzika siye,"alisema Mzee Mboma.

Alisema kuwa kesho yake walikwenda Polisi kutoa taarifa na kuambia waende na Frank kwa ajili ya mahojiano zaidi ili kuondoa utata.

Akiwa Polisi Frank alieleza kuwa baada ya kwenda Tunduma kutafuta maisha alijisikia roho ikiuma na kuamua kurudi kwao mara moja ndipo alipokuta msiba wake bandia.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Bw.Advocate Nyombi hakupatikana kuzungumzia sakata hilo lakini ofisa mmoja katika ofisi yake ambaye hakutaka kutajwa jina lake kwa kuwa si msemaji, alisema wamepata taarifa za tukio hilo na walikuwa wanasubiri maelezo kamili kutoka kwa maafisa wa Jeshi hilo waliokuwa wakifuatilia tukio hilo.
[ Read More ]

AMUUWA MDOGO WAKE KWA KUMCHOMA KISU.

SIMON JOHN [29] mkazi wa Jaluo anashikiliwa na Polisi kwa tuhuma za kumuua mdogo wake kwa kumchoma na kisu huko Arusha.
Kamanda wa polisi mkoa wa Arusha, Basilio Matei amesema kuwa mtuhumiwa alikamatwa baada ya kutokea kifo hicho na kukutwa na kisu kikiwa kimetapakaa damu.

Kamanda Matei alisema kuwa mtuhumiwa alimuuwa mdogo wake aliyetambulika kwa jina la George wakati wakiwa katika ugomvi wa kifamilia kati yao.

Amasema mtuhumiwa katika ugomvi huo alichukua kisu na kumchoma nacho sehemu za kifua na kumsababishia kifo hicho.

Hata hivyo Kamanda Matei alisema kuwa hadi anatoa taarifa hizi chanzo cha kutokea kwa ugomvi huo hadi mtuhumiwa huyo kuchukua uamuzi wa kumchoma na kisu ndugu yake huyo kilikuwa bado hakijajulikana.

Amesema mtuhumiwa atafikishwa Mahakamani wakati wowote baada ya upelelezi wa tukio hilo kukamilika.

source;nifahamishe.com
[ Read More ]

KAZI NGUMU KUZUIA HOMA YA NGURUWE


Zaidi ya nchi 100 duniani, miongoni mwao Kenya na Uganda, zinakabiliana na shambulio la homa ya nguruwe na sasa Mkuu wa Shirika la Afya Duniani, WHO, Dr Margaret Chan aonya kwamba itakuwa vigumu kujaribu kudhibiti ugonjwa huo..

Alikuwa akihutubia mkutano wa maafisa wa afya ulioandaliwa na Umoja wa Mataifa mjini Cancun, nchini Mexico.

Dr Chan alisema hatua ya kufanyika kwa mkutano huo nchini Mexico ambako homa hiyo ilianzia, ni ishara kubwa ya kuwa na imani katika nchi hiyo.

“Mexico ni salama, inavutia na ni pahali penye ukarimu mkubwa.”

Alisema kwamba aina ya ugonjwa huo ya H1N1 si hatari mno kwa kuwa ni rahisi kwa mgonjwa kupata nafuu bila ya matatizo.

“Na hapo ndipo tunakumbana na changamoto; kuwapa watu nasaha ya kuelewa wakati wa kupata huduma za matibabu na wakati wa kutokuwa na hofu,” alisema Dr Chan.

Kenya imeripoti visa tisa vya watu ambao wana virusi hivyo. Wote ni wageni kutoka Uingereza ambako inakisiwa maambukizo yatakuwa mengi.

Uganda nayo pia imetangaza kisa kimoja cha ugonjwa huo.

Viongozi na wataalamu kutoka nchi 50 wanakutana mjini Cancun kwa siku mbili ili kujadili mikakati ya kudhibiti kusambaa kwa virusi vinavyosababisha ugonjwa huo.

Tangu ugonjwa huo kuzuka karibu miezi miwili iliyopita, zaidi ya watu elfu 70 wameambukizwa na zaidi ya mia tatu kufariki dunia.

[ Read More ]

Aliyemzushia Mumewe Amembaka Atupwa Jela

Mwanamke mmoja wa nchini Uingereza ambaye alimshtaki mumewe akidai mumewe amembaka ili aweze kuvunja uhusiano wao na kisha ajirushe na mwanaume mwingine amehukumiwa kwenda jela miezi minne.
Michaela Lodge, alifanya mapenzi na mumewe Martin katika nyumba waliyokuwa wakikaa pamoja mwezi novemba mwaka jana halafu baadae aliwapigia simu polisi akidai mumewe amemshambulia na amembaka.

Kwa mujibu wa gazeti la Daily Mail la Uingereza, polisi walimhoji mwanamke huyo kwa masaa 62 wakati mumewe alitupwa selo kwa masaa 12 na baadae kuachiwa kwa dhamana baada ya kusisitiza kuwa alifanya mapenzi na mkewe kwa hiari yake bila kumlazimisha.

Mwanamke huyo mwenye umri wa miaka 45 na mkazi wa mji wa Essex alitengeneza barua ya ushahidi miezi miwili baadae akisisitiza kuwa amebakwa na mumewe lakini hataki mumewe ashtakiwe.

Mwezi februari mwaka huu mwanamke huyo alimwandikia barua mumewe akikiri kuwa aliongopa madai ya kubaka.

"Siwezi kuendelea na kesi hii tena, wakati tulipopanda kitandani sote tulikuwa na hamu ya kufanya mapenzi, niliwaongopea polisi kuwa umenibaka" ilisema barua hiyo.

Bwana Lodge aliwaonyesha polisi barua hiyo ya mkewe na haukupita muda polisi walimkamata mkewe.

Akitoa hukumu, jaji Rodger Hayward Smith alisema "Yalikuwa ni madai ya kutisha uliyokuwa umeyapangilia mapema ili kumtoa maishani mwako".

Michaela, mama wa watoto watatu alihukumiwa jana kwenda jela miezi minne pamoja na maombi ya mumewe kuwa asamehewe adhabu ya kifungo jela.

source:nifahamishe.com
[ Read More ]

MTOTO PEKEE ALIYEOKOKA KATIKA AJALI YA NDEGE YA YEMENIA


Mtoto aliyenusurika kimiujiza kwenye ajali ya ndege ya Yemen Airways iliyodondoka kwenye bahari ya Hindi karibu na visiwa vya Komoro na kuua watu 152 ameelezea jinsi alivyonusurika kimiujiza kwenye ajali hiyo. Bahia Bakari mwenye umri wa miaka 14 ndiye abiria pekee aliyenusurika kwenye ajali ya ndege ya Yemenia, Airbus A310 iliyotokea alfajiri ya jumanne wiki hii.

Bahia aling'ang'ania mabaki ya ndege na kuelea juu yake kwa masaa 12 katika hali ya hewa mbaya na bahari ambayo imejaa papa wengi kabla ya waokoaji kufika na kumuopoa.

Mtoto huyo ambaye hali yake inaendelea vizuri baada ya kupewa matibabu nchini Komoro amerudi kwao Ufaransa kuungana na baba yake.

Kassim Bakari, baba wa msichana huyo, akiongea na vyombo vya habari vya Ufaransa alisema kuwa nilipoongea naye kwa simu aliniambia "Tuliona ndege ikiangukia kwenye maji, nilijikuta kwenye maji, niliwasikia watu wakiongea lakini sikuweza kumuona hata mtu mmoja. Nilikuwa kwenye kiza sikuona chochote".

"Baba sikuweza kuogelea vizuri, niling'ang'ania juu ya kitu, sijui ni kitu gani" alisema Bahia akimwambia baba yake.

Bakari ambaye ana watoto wengine watatu alisema kuwa aliposikia habari za ajali ya ndege hiyo, moja kwa moja alifikiria kuwa hatamwona tena mkewe na mtoto wake wa kwanza.

"Ni msichana mwenye aibu sana, sikufikiria kama angenusurika namna hii, Siwezi kusema hii ni miujiza bali ni matakwa ya mwenyezimungu" alisema Bakari.

Bakari alisema kuwa Bahia hadi sasa hajaambiwa kuwa mama yake amefariki.

"Walimwambia kuwa mama yako yupo chumba cha jirani ili kutomshtua lakini ukweli ni kwamba mama yake amefariki na sijui nani ataweza kumwambia" alisema baba wa mtoto huyo.

Waokoaji walimuokoa Bahia kwenye bahari ya Hindi kilomita 16 toka kwenye pwani ya Visiwa vya Komoro.

Waokoaji hao walisema kuwa Bahia alikuwa dhaifu sana wakati anaokolewa, hakuweza hata kulishika boya alilorushiwa na hivyo kumfanya mzamiaji kupiga mbizi na kumpandisha kwenye boti ambako alifunikwa na blanket na kupewa maji ya moto yenye sukari anywe wakati anawahishwa hospitali.

Watu wengi wamestaajabu jinsi mtoto huyo alivyonusurika ajali hiyo na kuelea kwa jumla ya masaa 12 kwenye bahari ambayo imejaa papa wengi tena akiwa hana hata life jacket.


source:nifahamishe.com
[ Read More ]

Mwanamuziki Diana Ross kupewa watoto Michael Jakson

Mwanamuziki mashuhuri wa Marekani, Diana Ross ametajwa katika wosia wa Michael Jackson kama mlezi wa watoto watatu wa Michael inapotokea mama yake Michael Jackson mwenye miaka 80 atakaposhindwa kuwaangalia.

Hayo yapo katoka Wosia wa Michael Jackson ulioandikwa mwaka 2002 ambao ulikuwa ukisubiriwa kwa hamu, ambapo ulitolewa jana katika mahakama kuu ya Los Angeles, katika wosia huo Michael Jackson hakumtaja mke wake wa zamani Debbie Rowe kuchukua nafasi yoyote ya kuwalea watoto hao.

Katika wosia huo Michael Jackson amesema ndoa yake na Debbie Rowe iliishavunjika na kiuhakika hali hiyo inamzuia Debbie kupata chochote kutoka kwa Michael Jackson.

Michael Jackson ameacha mali yenye thamani ya jumla ya dola za kimarekani zaidi ya milioni 500 kwa familia yake.

Michael Jackson amemtaja mama yake kuwa msimamizi mkuu na mlezi wa watoto wake watatu.

Wosia huo ulipelekwa mahakamani na mwanasheria wa zamani wa Michael Jackson aitwaye John Blanca na kiongozi wa wanamuziki wa zamani John Mclain ambao walikuwa marafiki wa Michael kibiashara, wote wawili katika wosia wa Michael wametajwa kuwa wasimamizi wa mirathi.

Hata hivyo, wosia huo umeshindwa kutoa mwongozo wa masuala kadhaa likiwemo la maziko ya Michael Jackson kwamba atazikwa vipi na wapi au kuhusu utajiri wake utagawanywa vipi.

Vyombo vya habari mbalimbali vilikuwa vikidai leo mwili wa marehemu Michael utaagwa na mazishi yatafanyika siku ya Jumapili taarifa ambazo familia ya marehemu imezikanusha, lakini hawajasema lini nguli huyo wa muziki atazikwa.

Diana Ross mwenye miaka 65 ambaye alikuwa rafiki wa Michael Jackson amesema ," Moyo wangu unauma sana kusikia kifo cha Michael, hivi sasa nipo katika sara kuwaombea watoto wa Michael na familia ya Jackson."

Mwanasheria wa Michael alisema alichelewa kupeleka wosia huo mahakamani kwa sababu alitaka familia ya Jackson kuupitia kwanza.

"Suala la msingi katika wosia huo ni kwamba Michael amemwandika mama yake kuwa msimamizi mkuu wa watoto wake kisheria,"alisema mwanasheria huyo aitwaye Blanca.

Wakati huo huo mtengeneza muziki mkongwe Quincy Jones amesema anaweza asihudhurie mazishi ya Michael Jackson.

Jones ambaye alimtengenezea Michael albamu tatu ambazo ni Thriller, Off the Wall na Bad, bado yupo katika huzuni kubwa kutokana na kifo hicho cha ghafla cha rafiki yake Michael Jackson.

Serikali ya Marekani imeingia katika zoezi la uchunguzi wa kifo cha Michael Jackson ambapo itawachunguza madaktari waliohusika na Michael, jinsi wanavyofanya kazi na vyanzo vyao vya kupata madawa.

[ Read More ]

KIBAKA AHARIBIWA SURA KATIKA NYUMBA YA BONDIA.


Gregory McCalium kabla na baada ya kupewa kichapo na babu ambaye ni bondia mstaafu

Kibaka aliyezamia kwenye nyumba ya babu mmoja nchini Uingereza mwenye umri wa miaka 72 na kuanza kumtishia kwa kisu bila kujua kwamba babu huyo alikuwa ni bondia mstaafu, aliambulia kipigo kilichoichakaza sura yake.
Kibaka huyo Gregory McCalium mwenye umri wa miaka 24 mkazi wa wa Oxford nchini Uingereza, alivamia kwenye nyumba ya jirani yake ambayo babu huyo alikuwa akiishi na mke na kujaribu kuwapora mali zao bila kujua kwamba babu huyo alikuwa bondia mstaafu.

Babu Frank Corti mwenye umri wa miaka 72 alikuwa ni bondia maarufu enzi za ujana wake akiwa amejikusanyia vikombe kadhaa katika mashindano mbali mbali ya ndondi nchini Uingereza.

Picha iliyotolewa na polisi wa Uingereza ilionyesha jinsi sura ya kibaka huyo aliyekuwa na kisu ilivyoharibiwa vibaya na ngumi nzito za babu huyo.

Babu Corti baada ya kumwangushia kipondo McCalium alimlaza chini na kumlalia mpaka polisi walioitwa na mkewe walipokuja kumchukua.

Jumanne wiki hii McCalium alihukumiwa kwenda jela miaka minne na nusu kwa kosa hilo la jinai.

"Mwanzo nilishtuka aliporusha kisu chake, lakini kama watu wengine jinsi ambavyo wangejihami na mimi niliamua kufanya hivyo" alisema Corti.

"Umepata ulichostahili" alisema mwendesha mashtaka Angela Morris akimwambia McCalium wakati akisomewa mashtaka yake mahakamani hapo.

Tukio hilo lililotokea mida ya asubuhi lilimwacha kibaka McCallium akiwa amepasuliwa chini ya jicho lake na amechanika mdomo wake.

source:nifahamishe.com
[ Read More ]