A tourist asked a boat Guy do u know biology,physiology,geology,psychology and criminology?The boat guy said No........The tourist then said damn, what the hell do u know on the face of this earth you will die illiteracy!!
After a while a boat started sinking' then a boat guy asked the tourist Do you know swimology and escapology from crocodology? The tourist answer No........the boat guy said well you will drownology and crocodilogy will eat your assology and you will dieology because of your badmouthlogy!
have a nice weekend
WANUNUZI watano wa mahindi wamekufa na wengine watatu kujeruhiwa baada ya tairi la gari walilokuwa wakisafiria, kupasuka na kusababisha gari hilo kupinduka, katika eneo la Magubike katika Barabara ya Dodoma- Morogoro.Kamanda wa Polisi mkoani Morogoro, Adolphina Chialo, aliwataja waliokufa katika ajali hiyo juzi usiku kuwa ni Mwarami Abdallah, mkazi wa Mzense jijini Dar es Salaam, Selemani Ngula (30), Kasimu Mwitago (30).
Kwa mujibu wa kamanda huyo, maiti mwingine ametambuliwa kwa jina moja la Kiejo (30) wakati mwingine hajatambuliwa. Chialo pia aliwataja waliojeruhiwa kuwa ni, Timoth Paul, Elisafi Mkumbwa na Hamisi Selemani, wote wakazi wa Kibaigwa na kwamba majeruhi hao wamelazwa katika Hospitali ya Mkoa wa Morogoro kwa matibabu.
Alisema gari hilo lilikuwa linatokea katika Kijiji cha Kibaigwa, wilayani Kilosa kwenda jijini Dar es Salaam na kwamba chanzo cha ajali ni mwendo mkali.Alisema watu hao walikuwa wanasafiri kwa kutumia gari aina ya Mistubish Fuso iliyokuwa ikiendeshwa na Jackson Bezaleli Senyegwa (27) mkazi wa Kibaigwa ambaye alitoroka mara baada ya ajali hiyo.
Akizungumza na Mwandishi wa habari hizi katika wodi namba moja,mmoja wa majeruhi Hamisi Selemani, alisema gari hilo lilikuwa limebeba gunia 100 za mahindi, jambo lililosababisha moja ya matairi kuelemewa na kupasuka.
Alisema abiria wote waliokuwa nyuma ya gari hilo walifariki papo hapo baada ajali na kwamba walifunikwa na mahindi.Kamanda huyo alisema miili ya watu hao imehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti cha Hospitali ya Mkoa wa Morogoro, na kuomba wananchi kujitokeza ili kutambua miili ambayo haujatambuliwa.
[ Read More ]
Kwa mujibu wa kamanda huyo, maiti mwingine ametambuliwa kwa jina moja la Kiejo (30) wakati mwingine hajatambuliwa. Chialo pia aliwataja waliojeruhiwa kuwa ni, Timoth Paul, Elisafi Mkumbwa na Hamisi Selemani, wote wakazi wa Kibaigwa na kwamba majeruhi hao wamelazwa katika Hospitali ya Mkoa wa Morogoro kwa matibabu.
Alisema gari hilo lilikuwa linatokea katika Kijiji cha Kibaigwa, wilayani Kilosa kwenda jijini Dar es Salaam na kwamba chanzo cha ajali ni mwendo mkali.Alisema watu hao walikuwa wanasafiri kwa kutumia gari aina ya Mistubish Fuso iliyokuwa ikiendeshwa na Jackson Bezaleli Senyegwa (27) mkazi wa Kibaigwa ambaye alitoroka mara baada ya ajali hiyo.
Akizungumza na Mwandishi wa habari hizi katika wodi namba moja,mmoja wa majeruhi Hamisi Selemani, alisema gari hilo lilikuwa limebeba gunia 100 za mahindi, jambo lililosababisha moja ya matairi kuelemewa na kupasuka.
Alisema abiria wote waliokuwa nyuma ya gari hilo walifariki papo hapo baada ajali na kwamba walifunikwa na mahindi.Kamanda huyo alisema miili ya watu hao imehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti cha Hospitali ya Mkoa wa Morogoro, na kuomba wananchi kujitokeza ili kutambua miili ambayo haujatambuliwa.
VIJANA wanaomaliza vyuo vikuu vya Zanzibar wataanza kunufaika na utaratibu wa kupatiwa mafunzo maalumu ya biashara pamoja ufundi yatakayowawezesha kufungua miradi kujiajiri na kuwaajiri vijana wengine na kukuza hali zao za maisha.
Utaratibu huo unatarajiwa kutekelezwa kufuatia mazungumzo yaliyofanyika kati ya ujumbe wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar unaoongozwa na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad na Idara ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (IT&C) ya Andhara Pradesh yaliyofanyika Hoteli ya Grand Kakatiya mjini Hyderabad.
Mbali na hatua hiyo Serikali ya Andhra Pradesh imemwomba Balozi wa Tanzania nchini India, John Kijazi kuandaa utaratibu utakaowezesha Zanzibar kunufaika na makubaliano yaliyofikiwa katika ziara ya Makamu wa Kwanza wa Rais kukuza mashirikiano katika nyanja za kiuchumi, biashara, kilimo na elimu kwa faida ya nchi mbili hizo.
Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari na Mawasiliano wa Serikali ya Andhra Pradesh, Pannola Lakshmaiah alisema utaratibu huo unapaswa kuandaliwa mikakati ya ya utekelezaji mapema ili Serikali mbili hizo hasa Zanzibar iweze kunufaika mapema na kuchangia harakati zake za kuinua hali yake ya kiuchumi.
Alisema Jimbo la Andhra Pradesh limepata heshima kubwa duniani kote kwa Teknolojia ya Mawasiliano na Habari (IT), ambapo pia katika eneo hilo kunapatikana mji maalum wa Teknolojia ya Mawasiliano (Hyderabad Technology City) unaotoa mchango mkubwa katika kukuza uchumi wa eneo hilo na India kwa ujumla.
“Jambo muhimu tutiliane saini makubaliano ya mashirikiano leo hii jioni (jana) na kitakachofuata Balozi aandae utaratibu wa utekelezaji kwa vile hakuna muda wa kusubiri, teknolojia ya habari na mawasiliano hivi sasa ni ajira ni uchumi ni kila kitu”, alisema Waziri wa IT& C.
Katika mazungumzo hayo, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, Ramadhan Abdallah Shaaban alisema bado Zanzibar iko nyuma katika elimu ya IT&C, licha ya juhudi kubwa zinazoendelea kuchukulia kuinua elimu hiyo, ukiwamo mpango mahsusi ulioanzishwa na Serikali ya Zanzibar uitwao E -government.
Waziri Shaaban alisema kuna haja Serikali ya Andhra Pradesh ambapo inafanana kiutawala na Zanzibar ndani ya Jamhuri ya Muungano kushirikiana kuandaa utaratibu wa masomo kwa vijana wa Zanzibar.
Alisema kazi hiyo inaweza kufanikishwa chini ya utaratibu wa kupeleka wataalamu Zanzibar kutoa mafunzo hayo au vijana wa Zanzibar kwenda India kujifunza na baadaye kurudi nyumbani kutumia ujuzi huo kwa maslahi yao na nchi.
Waziri wa Biashara, Viwanda na Masoko, Nassor Ahmed Mazrui alisema Zanzibar kuna vijana wengi wanaomaliza vyuo vikuu na kukaa muda mrefu bila ya kupata ajira na utaratibu huo utawasaidia kupunguza tatizo la uhaba wa ajira na kuwapa mafunzo ya kazi maalumu za amali zitakazosaidia kuimarisha maendeleo.
Waziri Mazrui alisema maeneo mengine ambayo Zanzibar inaweza kunufaika katika mashirikiano na Andhra Pradesh ni usindikaji wa bidhaa kama vile za matunda, viungo pamoja na mazao ya baharini.
Waziri Mazrui alisema Zanzibar imejaaliwa kuna rasilimali za viungo kama vile karafuu zao ambao linasafirishwa kwa wingi kwenda India na kama kutakuwa na utaratibu wa kufanyiwa ‘branding’ na baadaye kusafirishwa litaweza kupata soko kubwa zaidi ya sasa katika soko la dunia.
Aliyekuwa rais wa Afghanistan Burhanuddin Rabbani ameuliwa baada ya mtu aliyelificha bomu kwenye kilemba chake kulilipua bomu hilo wakati wakisalimiana.
Rais Burhanuddin Rabbani ambaye pia alikuwa ndiye mkuu wa baraza kuu la kutafuta amani nchini Afghanistan, alifariki dunia baada ya mtu aliyekuwa akimuamini kumgeuka na kujilipua kwa bomu alilolificha kwenye kilemba chake. Wasaidizi wanne wa Rabbani nao walifariki dunia baada ya bomu hilo kulipuka wakati Rabanni aliposimama kumsalimia kwa kumkumbatia mwakilishi wa Talibani baada ya kumalizika kwa mazungumzo marefu baina yao ya kutafuta suluhisho la amani nchini Afghanistan. Fazel Karim Aymaq ambaye ni mjumbe wa baraza la amani la Afghanistan alisema kuwa watu wawili wanaoaminika sana walifika nyumbani kwa Rabbani mjini Kabul ili kuleta ujumbe wa amani toka kwa Talibani. "Mmoja wao alisalimiana na Rabbani kwa kuweka kichwa chake kwenye mabega ya Rabbani na kulilipua bomu alilokuwa amelificha kwenye kilemba chake", alisema Aymaq. Taarifa zaidi zilisema kuwa mjumbe huyo wa Talibani alikuwa akijulikana kama Mohammad Masoom na alikuwa akifahamiana vizuri sana na Rabbani akiaminika kuwa anatafuta suluhisho la amani. Masoom aliluwa akienda mara kwa mara nyumbani kwa Rabbani na aliwahi kumkaribisha Rabbani nyumbani kwake na alimpa ulinzi wa kutosha hali iliyomjengea uaminifu wa kutosha kwa rais huyo wa zamani. Masoom aliteuliwa na Talibani kuwa mwakilishi wa Talibani katika mazungumzo ya kutafuta suluhisho la amani kati ya Talibani na serikali ya Afghanistan. Kuuliwa kwa Rabbani ni pigo kubwa sana kwa rais wa Afghanistan, Hamid Karzai ambaye aliamua kukatisha ziara yake nchini Marekani na kurudi Afghanistan. Mamia ya watu waliandamana leo kwenye mitaa ya mjini Kage.bul kulaani kuuliwa kwa rais huyo mstaafu aliyekuwa akiheshimika kwa jitihada zake za kuleta amani kwenye nchi hiyo ambayo imeharibiwa kwa vita. "Alitaka amani nchini Afghanistan na alijitolea maisha yake kupigania njia ya kuleta amani", alisema mmoja wa waandamanaji hao. source nifahamis | ||
KESI ya ajali ya meli ya MV Spice Islanders iliyofunguliwa dhidi ya manahodha wa meli hiyo na mmiliki wake, imesitishwa.Kesi hiyo ambayo jana ilitajwa kwa mara ya pili katika Mahakama Kuu ya Zanzibar, imesitishwa kupisha uchunguzi wa kamati iliyoundwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk Ali Mohamed Shein.
Hatua hiyo imefikiwa na Mrajisi wa Mahakama hiyo, George Kazi baada ya wakili wa utetezi, Hamidi Mbwezeleni, kuiomba Mahakama iiahirishe kwa sababu Katiba ya Zanzibar inapinga kesi moja kusikilizwa na vyombo viwili vinavyofanya kazi kwa mujibu wa katiba hiyo.
“Kama kuna haja ya watu hawa kushtakiwa kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar, basi tume hiyo ikae pembeni mpaka Mahakama itakapomaliza kazi yake na kama kuna haja ya tume hiyo kufanya kazi yake, basi Mahakama inabidi ikae pembeni mpaka tume hiyo itakapomaliza kazi yake,” alisema.
Bila kufanya hivyo alisema: "Hukumu ya watu hawa itakuwa na utata kwa sababu endapo Mahakama ikisema kuwa wana makosa na wanastahili adhabu halafu tume hiyo ikasema kuwa hawana makosa na hawastahili adhabu, Wazanzibari hawatatuelewa,” alisema Mbwezeleni na kusisitiza:
“Upande mwingine ni kwamba kama Mahakama ikisema kuwa watu hawa hawana makosa na wanastahili kuwa huru halafu tume hiyo ikasema kuwa watu hawa wana makosa na wanastahili kuchukuliwa hatua za kisheria, hali itakuwa tete kwa wananchi dhidi ya Serikali yao na Mahakama kwa ujumla.”
Awali, maelezo hayo ya upande wa utetezi yalipingwa na Wakili wa mashtaka, Ramadhan Nasibu ambaye alisema kama Serikali, haina shaka yoyote juu ya kamati hiyo kwa sababu inafahamu kwamba uamuzi wake hauwezi kuingilia wala kuharibu uamuzi wa Mahakama, kwa kuwa Mahakama ni chombo huru kinachosimamia haki.
“Upande wa mashtaka unajizuia kuhoji uhalali wa tume hiyo kwa sababu ushahidi wao hauwezi kuizuia Mahakama isifanye kazi yake wala haitakuwa mwisho wa mashtaka ya watu hao. Tume hiyo haina meno kwa sababu ushahidi wao utakaopatikana hauwezi kuwatia watuhumiwa hao hatiani,” alisema.
Baada ya malumbano hayo, Mrajisi wa Mahakama alikubaliana na hoja za upande wa utetezi na kuahirisha kesi hiyo.
Akisoma uamuzi huo Mrajisi Kazi alisema: “Siko tayari kusema kuwa tume hiyo ni halali ama si halali, ila kwa pointi iliyotolewa na upande wa utetezi, nami ninaona kwamba ni ya msingi, hivyo ninalazimika kuiahirisha kesi hii mpaka tume hiyo itakapomaliza kazi yake na kutoa mapendekezo.”
“Siwezi kuwa katika mtizamo tofauti na upande wa utetezi kuhusu suala hilo, kwa sababu kuna hatari ya uamuzi wa tume na mahakama, kupingana. Hivyo ninaahirisha kesi hii mpaka tume hiyo itakapomaliza kazi yake.”
Mrajisi Kazi pia alisema kuwa dhamana ya watuhumiwa hao iko wazi hivyo wanatakiwa kudhaminiwa kwa hati ya Sh1milioni kila mmoja na watahitajika Mahakamani hapo mara tu baada ya tume hiyo kukamilisha kazi yake na kutoa uamuzi.”
Septemba 10, mwaka huu meli ya MV Spice Islanders iliyokuwa ikitokea Unguja kwenda Pemba ilizama katika Kisiwa cha Nungwi, kilometa 20 kutoka Unguja na kusababisha vifo vya zaidi ya watu 200 na majeruhi zaidi ya 600, huku ikiaminika kwamba mamia ya abiria wengine hawakuolewa baharini.
Siku tatu baada ya ajali hiyo, watu wanne akiwamo
Nahodha wa meli hiyo, Saidi Abdala Kinyanyite (58), mkazi wa Mbagala, Dar es Salaam na Nahodha Msaidizi, Abdallah Mohamed Ali (30), mkazi wa Bububu, Zanzibar walifikishwa mahakamani na kushtakiwa kwa uzembe na kusababisha vifo vya watu.
Watuhumiwa wengine katika kesi hiyo ni Simai Nyange Simai (27), Mkazi wa Mkele, Zanzibar ambaye ni Ofisa Usalama wa Bandarini na vyombo vyote vya usafiri wa majini na Yussuf Suleiman Jussa (47), Mkazi wa Kikwajuni Zanzibar ambaye ni Ofisa wa meli hiyo na mwanahisa.
Zaidi ya watu 36 wamefariki dunia nchini Burundi baada ya watu waliokuwa na silaha kuvamia baa na kuwapiga risasi watu wote waliokuwemo kwenye baa hiyo Watu 36 wameiaga dunia huku wengine wakiwa wamelazwa hospitali hali zao zikiwa mbaya baada ya watu waliokuwa na silaha kuvamia baada moja iliyopo nje kidogo ya mji mkuu wa Burundi, Bunjumbura na kuwamiminia risasi watu wote waliokuwemo kwenye baa hiyo.
Tukio hilo lilitokea jana wakati kundi la watu wanaoaminika kuwa ni waasi wa Burundi wanaoishi nchini Kongo kuvuka mpaka na kuivamia baa hiyo iliyopo kwenye mji wa Gatumba.
Gavana wa Bunjumbura, Jacques Minani alisema kuwa watu waliofanya shambulio hilo waliingia Gatumba baada ya kuvuka mto wakitokea nchini Jamhuri ya Kongo.
Mmoja wa watu waliojeruhiwa kwenye shambulio ambaye alipigwa risasi ya tumbo, alisema kuwa watu waliofanya shambulio hilo walikuwa wamevaa nguo za kijeshi.
"Mmoja wao alisema Waue wote waue wote hakikisha hakuna atakayenusurika", alisema majeruhi huyo aliyejulikana kwa jina la Jackson Kabura.
Kundi kubwa la watu waliokuwa na silaha nzito za kivita waliivamia baa inayojulikana kwa jina la 'Chez les Amis' na kuwalazimisha watu wote walale chini.
Mwanaume mmoja ambaye alinusurika maisha yake ingawa ndugu zake wawili waliuawa kwenye shambulio hilo alisema kuwa "Walimwambia kila mtu alale chini na ndipo walipoanza kupiga risasi."
Miili ya watu iliachwa kwenye maegesho ya magari katika hospitali moja mjini Gatumba huku taarifa zaidi zikisema kuwa idadi ya majeruhi imekuwa kubwa kuliko uwezo wa hospitali.
Rais Pierre Nkurunziza wa Burundi aliahirisha safari yake ya kwenda New York, Marekani na kutembelea eneo lilipofanyika shambulio hilo na kuahidi kuwachukulia hatua kali watu wote waliohusika.
[ Read More ]
Tukio hilo lilitokea jana wakati kundi la watu wanaoaminika kuwa ni waasi wa Burundi wanaoishi nchini Kongo kuvuka mpaka na kuivamia baa hiyo iliyopo kwenye mji wa Gatumba.
Gavana wa Bunjumbura, Jacques Minani alisema kuwa watu waliofanya shambulio hilo waliingia Gatumba baada ya kuvuka mto wakitokea nchini Jamhuri ya Kongo.
Mmoja wa watu waliojeruhiwa kwenye shambulio ambaye alipigwa risasi ya tumbo, alisema kuwa watu waliofanya shambulio hilo walikuwa wamevaa nguo za kijeshi.
"Mmoja wao alisema Waue wote waue wote hakikisha hakuna atakayenusurika", alisema majeruhi huyo aliyejulikana kwa jina la Jackson Kabura.
Kundi kubwa la watu waliokuwa na silaha nzito za kivita waliivamia baa inayojulikana kwa jina la 'Chez les Amis' na kuwalazimisha watu wote walale chini.
Mwanaume mmoja ambaye alinusurika maisha yake ingawa ndugu zake wawili waliuawa kwenye shambulio hilo alisema kuwa "Walimwambia kila mtu alale chini na ndipo walipoanza kupiga risasi."
Miili ya watu iliachwa kwenye maegesho ya magari katika hospitali moja mjini Gatumba huku taarifa zaidi zikisema kuwa idadi ya majeruhi imekuwa kubwa kuliko uwezo wa hospitali.
Rais Pierre Nkurunziza wa Burundi aliahirisha safari yake ya kwenda New York, Marekani na kutembelea eneo lilipofanyika shambulio hilo na kuahidi kuwachukulia hatua kali watu wote waliohusika.
na nifahamishe.
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi ya Wilaya ya Mpanda, imemhukumu Haruna Ndayage (54), mkazi wa mtaa wa Kashaulili, kifungo cha miaka 30 jela baada ya kupatikana na hatia ya kumuingilia mkewe kinyume na maumbile.
Hukumu hiyo ilitolewa jana na Hakimu Mkazi, Desdel Magezi, baada ya kuridhika na ushahidi uliotolewa mahakamani hapo na upande wa mashtaka.
Alisema shahidi wa tano ambaye ni daktari aliithibitishia mahakama kuwa mlalamikaji baada ya kufanyiwa uchunguzi iligundulika kuwa aliingiliwa kinyume na maumbile yake.
Aidha, alisema ushahidi uliotolewa na watoto wao ulionyesha kuwa Haruna alimfayia kitendo hicho mkewe, kwani watoto wote walimtaja baba yao ndiye mhusika wa kitendo hicho.
Kabla ya kutolewa kwa hukumu hiyo, mshtakiwa aliiomba mahakama impunguzie adhabu, kwani wakati akifanya kosa hilo hakuwa na akili timamu.
Alidai kwa miaka 24 waliyoishi na mkewe hakuwa na ugomvi wowote naye isipokuwa miezi sita kabla ya tukio hili waalikuwa na ugomvi ugomvi ambao hakuweza kuueleza mahakamani hapo.
Hata hivyo, Mwendesha Mashtaka wa Polisi, Finias Mjula, alipinga utetezi huo na kuiomba mahakama itoe adhabu kali kwa mshtakiwa ili awe mfano kwa watu wengine wenye tabia ya kuwadhalilisha wake zao.
Awali katika kesi hiyo, ilidaiwa kuwa Oktoba 28, mwaka jana, majira ya saa 12 alfajiri, mshtakiwa alimwingilia kinyume cha maumbile mkewe.
Jiji la Mbeya liko kwenye taharuki hivi sasa kufuatia ajali ya moto unaoendelea kuwaka katika soko la Sido, ambako wafanyibiashara wa lililokuwa soko la Mwanjelwa walihamia baada ya soko hilo la awali kuungua.
[ Read More ]