Banner 468

1234453_10201664080105694_1716282793_n
Facebook

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AFUNGUA MKUTANO WA SIKU TATU WA MWAKA KUHUSU TAFITI ZA SERA NA MAENDELEO WA REPOA DAR



 
  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwahutubia washiriki wa mkutano wakati akifungua ramsi mkutano wa siku tatu wa mwaka kuhusu Tafiti za sera na Maendeleo wa Repoa, ulioanza leo April 3, 2013 katika Hoteli ya Kunduchi Beach jijini Dar es Salaam
 Baadhi ya washiriki wa mkutano huo wakiwa ukumbini humo wakimsikiliza Makamu wa Rais Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akifungua ramsi mkutano wa siku tatu wa mwaka kuhusu Tafiti za sera na Maendeleo wa Repoa, ulioanza leo April 3, 2013 katika Hoteli ya Kunduchi Beach jijini Dar es Salaam
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na baadhi ya viongozi wakati akiwasili kwenye Ukumbi wa Hoteli ya Kunduchi Beach, kufungua ramsi mkutano wa siku tatu wa mwaka kuhusu Tafiti za sera na Maendeleo wa Repoa, ulioanza leo April 3, 2013 katika Hoteli ya Kunduchi Beach jijini Dar es Salaam
 Mwenyekiti wa CUF Prof. Ibrahim Lipumba, akichangia wakati wa mkutano mkutano wa siku tatu wa mwaka kuhusu Tafiti za sera na Maendeleo wa Repoa, ulioanza leo April 3, 2013 katika Hoteli ya Kunduchi Beach jijini Dar es Salaam. Mkutano huo umefunguliwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa mkutano wa siku tatu wa mwaka kuhusu Tafiti za sera na Maendeleo wa Repoa, baada ya kuufungua mkutano hio, ulioanza leo April 3, 2013 katika Hoteli ya Kunduchi Beach jijini Dar es Salaam. Picha na OMR

Kikao cha Baraza la Wawakilishi Zanzibar.

 Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar Pandu Ameir Kificho akitoka katika Ukumbi wa Baraza baada ya kuahirisha Kikao cha asubuhi, kwa ajili ya mapumziko na kurudi jioni kuendelea na kuchangia miswada iliowakilisha katika Kikao hicho.  
 Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi, akibadilisha mawazo na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Fedha Omar Yussuf Mzee, wakitoka ukumbi wa mkutano baada ya kuahirishwa kikao cha asubuhi.
 Mwakilishi wa Donge na Waziri wa Ardhi Maji Nishati na Makaazi Juma Ali Shamuhuna, akimsikiliza Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Fatma Ferej,  
 Wajumbe wakibadilisha mawazo nje ya Ukumbi wa Baraza.
 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi Maji Nishati na Makaazi Mustafa Aboud Jumbe akizungumza na Wajumbe wa Baraza baada ya kikao cha asubuhi kuahirishwa wakiwa katika viwanja vya Baraza, kushoto Mwanasheria wa Mkuu Zanzibar Othman Masoud na Mwakilishi wa MjiMkongwe Ismail Jussa.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Ikulu na Mwakilishi wa Dimani Dk. Mwinyihaji Makame na Mwakilishi wa Bububu kulia Hussein Ibrahim Makungu (BHAA) wakitoka katika ukumbi wa baraza baada ya kuahirrishwa kwa kikoa cha asubuhi cha maswali na majibu na kujadili mswada wa Sheria ya Uundwaji wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma ya Maji na Nishati. Zanzibar
[ Read More ]

Utata wagubika kwa anayedaiwa kumuuwa Padri



omar-musa
Utata umegubika suala la mtu anayedaiwa kumuua kwa kumpiga risasi Padre Evarist Mushi wa Kanisa Katoliki baada ya ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP) Zanzibar kuinyima Polisi kibali cha kumfikisha mahakamani.
Mtu huyo, Omar Mussa Makame wa Zanzibar alitarajiwa kupandishwa kizimbani juzi, lakini ofisi ya DPP ilikataa hiyo hiyo juzi kutoa kibali kwa Polisi kufanya hivyo. Omar aliwahi kugombea ujumbe wa Baraza la Wawakilishi kupitia Chama cha Wananchi (CUF) jimbo la Rahaleo mwaka 2010.
Awali Kamishna wa Polisi Zanzibar, Mussa Ali Mussa alisema jana kuwa wameshindwa kumfikisha mahakamani mtuhumiwa huyo kwa vile DPP hakuwapa kibali.
Alipulizwa sababu ambazo zimemfanya DPP asitoe kibali hicho, alisema ni vyema akaulizwa yeye mwenyewe kwani ndiye aliyetoa sababu hizo.
Mkurugenzi wa Mashitaka Zanzibar, Ibrahim Mzee Ibrahim alipofuatwa ofisini kwake jana ilielezwa kuwa yuko kwenye mkutano na mwandishi wa habari hizi akalazimika kumuandikia juu ya suala hilo kupitia kwa Katibu Muhtasi wake.
Alijibu kwa njia ya maandishi majibu yake yakiwa na maneno matatu tu: “Kamuone Kamishna Mussa”.
Alipoandikiwa tena kuwa Kamishna Mussa ndiye aliyesema uulizwe wewe kwani ndiye uliyetoa sababu alijibu kupitia kwa Katibu Muhtasi wake: “Yeye (Kamishna) anazijua sababu kwanini hataki kuzisema? Nendeni kwake mukamuulize”.
Alipoulizwa mara ya pili juu ya majibu hayo ya DPP Ibrahim, Kamishna Mussa alisema kwamba yeye hawezi kujibu mambo ya mtu mwingine.
“Ndio majibu yake ninayo, lakini yeye (DPP) ndiye aliyetoa sababu kwa hiyo ndiyo yeye anayetakiwa kuzisema sio mimi, nadhani hii ndiyo haki, aseme mwenyewe,” alisema Kamishana Mussa.
Mtuhumiwa huyo yuko mikononi mwa Polisi tangu Machi 17 mwaka huu alipokamatwa kuhusiana na mauaji hayo ya Padre Mushi aliyeuawa Februari 17 mwaka huu wakati akienda kuongoza ibada katika Kanisa la Mtakatifu Teresia liliopo Beit el Raas nje kidogo ya mji wa Zanzibar.
Katika hatua nyengine Mahakama Kuu Zanzibar imeamuru kuletwa mahakamani kwa mtuhumiwa wa mauaji ya Padri Evaristus Mushi, jumatatu ijayo ili kuweza kusikiliza shauli lililofunguliwa juzi na mawakili wa upande wa mlalamikiwa la kutofishwa mahakamani kwa mteja wao ndani ya saa 24 baada ya kukamatwa.
Mtuhumiwa huyo Omar Mussa Makame (37)aliyekuwa mgombea uwakilishi wa Jimbo la Rahaleo katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010 kupitia tiketi ya Chama cha Wananchi (CUF) bado anashikiliwa na polisi Zanzibar, anatetewa na Kampuni ya Uwakili ya AJM Solicitors and Advocate.
Juzi mchana wakili wa Kampuni hiyo Abdalah Juma Mohamed aliwakilisha mahakama kuu ya Zanzibar maombi ya Habeas Corpus application chini ya kifungu cha 390 cha Sheria ya Makosa Jinai sura ya 7 ya mwaka 2007 inayomtaka mtu anayemshikila mtu mwingine au chombo chochote bila kumfikisha mahakamani kwa saa 24 aeleze mahamaka sababu za kushikilia mtu bila kumfikisha mahakamani au amwachie huru.
Mawakili hao walimtumia summons Mkurugenzi wa Mkosa ya Jinai Zanzibar (DCI) na jana Naibu wake Kamishina Msaidizi wa Polisi Yusuf Ilembo alifika mbele ya Jaji Isack Mkusa, kusikiliza shauli hilo.
Mawakili wa Kujitegemea upande wa mlalamikiwa waliokwakilishwa na Shabani Juma Shabani pamoja na Shaibu Ibrahim waliiomba mahakani hiyo iamuru kuachiwa kwa mteteja wao .
Hata hivyo jaji Mkusa alisema, kutokana na maombi hayo kuletwa chini ya kiapo vi vema pia Upande wa serikali nao ukapewa muda wa kujiandaa kuweza kujibu hoja hizo chini ya kiapo.
Baada ya kusikilza pande zote mbili Jaji Mkusa chini ya kifungu cha sheria section 8 ya mwaka 2006 inatoa nafasi kwa mtu kupewa dhamana lakini kwa jinsi mahakama itakanyoona inafaa.
Lakini wakati huo huo muhusika naye aletwe mahakamani wakati wa kusikiliza shauri lake ‘application’ kulingana na section 8.
Padre Mushi aliyekuwa Paroko wa Parokia ya Kanisa la Minara Miwili Zanzibar aliuawa asubuhi ya February 17 mwaka huu kwa kupigwa risasi wakati akijiandaa kuendesha ibada katika kanisa la Mtakatifu Theresia nje kidogo ya Mji wa Zanzibar.
Kuuawa kwa risasi kwa Pandri Mushi, kulitanguliwa pia na shambulizi kama nilo kwa Padri Padri Ambrose Mkenda pia wa Kanisa Katokiki Zanzibar mwezi desemba mwaka jana ambaye alijeruhiwa taya ya kulazwa kwa siku kadhaa katika hospitali ya Taifa Muhimbili.
Wakati huo huo Ofisi ya DCI Zanzibar, imesema bado inasumbiri pia majarada mawili ya kesi ya kumwagiwa tindikali kwa 6 Nov 2012 kwa Katibu wa Mufti wa Zanzibar, Sheikh Fadhil Soraga, pia lile la Padri Ambrose Mkenda ambayo bado yapo kwa DPP ili kuwafikisha mahakamani watu wanaotunumiwa na makosa hayo mbao kwa sasa wako nje kwa dhamana.
Chanzo: Mwananchi
[ Read More ]

MCHUMBA WA PREZZO, GOLDIE WAFARIKI DUNIA




Goldie Harvey enzi za uhai wake.
Goldie akiwa na mchumba wake Prezzo.
MWANAMUZIKI kutoka nchini Nigeria, Goldie Harvey ambaye pia ni mchumba wa msanii Prezzo amefariki dunia.

Kwa mujibu wa vyanzo vya habari vya nchini Nigeria, Goldie amefariki dunia akiwa hopitalini nchini humo muda mfupi baada ya kutoka nchini Marekani alipohudhuria tuzo za Grammys. Prezzo hakupatikana kudhibitisha tukio hilo,…
Goldie Harvey enzi za uhai wake.
Goldie akiwa na mchumba wake Prezzo.
MWANAMUZIKI kutoka nchini Nigeria, Goldie Harvey ambaye pia ni mchumba wa msanii Prezzo amefariki dunia.
Kwa mujibu wa vyanzo vya habari vya nchini Nigeria, Goldie amefariki dunia akiwa hopitalini nchini humo muda mfupi baada ya kutoka nchini Marekani alipohudhuria tuzo za Grammys. Prezzo hakupatikana kudhibitisha tukio hilo, lakini mtu anayesimamia uwekaji habari katika ukurasa wa Facebook wa msanii huyo alidhibitisha kuwa msanii huyo amefariki dunia usiku wa kuamkia leo na kuandikia hivi “Kwa masikitiko makubwa napenda kuwataarifu wote kuwa Goldie amefariki dunia muda mfupi baada ya kuwasili jijini Lagos akitokea Marekani. Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi,” Alisema mwekaji habari huyo.
Sababu zilizopelekea kifo cha msanii huyo mpaka sasa bado hazijafahamika.
[ Read More ]

UTOAJI WA VITAMBULISHO VYA TAIFA KWA UPANDE WA ZANZIBAR AWAMU YA KWANZA


06246Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akipokea Kitambulisho cha Taifa kutoka
kwa Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Perera Ame Silima,wakati wa
  Utoaji wa vitambulisho vya Taifa,awamu ya  kwanza kwa upande wa
Zanzibar,katika  hafla iliyofanyika jana  viwanja vya Baraza la
Wawakilishi Chukwani, Nje ya Mji wa Zanzibar,[Picha na Ramadhan
Othman,Ikulu.]
IMG_0018Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraz la Mapinduzi
Dk.Ali Mohamed Shein,akikaribishwa na Mkurugenzi Mkuu wa vitambulisho
vya Taifa,Dicson Maimu,alipowasili katika viwanja vya Baraza la
Wawakilishi Chukwani, Nje ya Mji wa Zanzibar,katika Utoaji wa
vitambulisho vya Taifa,awamu ya  kwanza kwa upande wa Zanzibar.[Picha
na Ramadhan Othman,Ikulu.]
IMG_9473Kadhi Mkuu wa Zanzibar Sheikh Khamis Haji,akiweka
kidole Gumba kufanya uhakiki katika mashine maalum,wakati wa Utoaji wa
vitambulisho vya Taifa,awamu ya  kwanza kwa upande wa Zanzibar,katika
hafla iliyofanyika jana katika  viwanja vya Baraza la Wawakilishi
Chukwani, Nje ya Mji wa Zanzibar,[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.]
IMG_9486Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar Pandu Ameir
Kificho,akiweka kidole Gumba kufanya uhakiki katika mashine
maalum,wakati wa Utoaji wa vitambulisho vya Taifa,awamu ya  kwanza kwa
upande wa Zanzibar,katika hafla iliyofanyika jana katika  viwanja vya
Baraza la Wawakilishi Chukwani, Nje ya Mji wa Zanzibar,[Picha na
Ramadhan Othman,Ikulu.]
IMG_9496Baadhi ya Viongozi na Wananchi,na Wafanyakazi wa
Mamlaka ya vita mbulisho wakiwa katika hafla ya  Utoaji wa
vitambulisho vya Taifa,awamu ya  kwanza kwa upande wa Zanzibar,katika
hafla iliyofanyika jana katika  viwanja vya Baraza la Wawakilishi
Chukwani, Nje ya Mji wa Zanzibar,[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.]
IMG_9511Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania,Jenerali Devis
Mwamunyange, akiweka kidole Gumba kufanya uhakiki katika mashine
maalum,wakati wa Utoaji wa vitambulisho vya Taifa,awamu ya  kwanza kwa
upande wa Zanzibar,katika hafla iliyofanyika jana katika  viwanja vya
Baraza la Wawakilishi Chukwani, Nje ya Mji wa Zanzibar,[Picha na
Ramadhan Othman,Ikulu.]
IMG_9735Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi,Dk.Ali Mohamed Shein,(kushoto) akimkabidhi kitambulisho
Makamo wa Pili wa Rais Balozi Seif Ali Iddi,wakati wa   Utoaji wa
vitambulisho vya Taifa,awamu ya  kwanza kwa upande wa Zanzibar,  hafla
ilifanyika jana katika  viwanja vya Baraza la Wawakilishi Chukwani, Nje
ya Mji wa Zanzibar,[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.]
IMG_9741Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi,Dk.Ali Mohamed Shein,(kushoto) akimkabidhi kitambulisho Jaji
Mkuu wa Tanzania,Mohamed Chande Othman, wakati wa   Utoaji wa
vitambulisho vya Taifa,awamu ya  kwanza kwa upande wa Zanzibar,katika
hafla iliyofanyika jana  viwanja vya Baraza la Wawakilishi Chukwani,
Nje ya Mji wa Zanzibar,(kushoto) Naibu waziri wa Mambo ya Ndani ya
Nchi Perera Ame Silima,[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.] 
IMG_9753Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi,Dk.Ali Mohamed Shein,(kushoto) akimkabidhi kitambulisho Jaji
Mkuu wa Zanzibar,Omar Othman Makungu,wakati wa   Utoaji wa
vitambulisho vya Taifa,awamu ya  kwanza kwa upande wa Zanzibar,katika
hafla iliyofanyika jana katika  viwanja vya Baraza la Wawakilishi
Chukwani, Nje ya Mji wa Zanzibar,[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.]
IMG_9779Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi,Dk.Ali Mohamed Shein,(kushoto) akimkabidhi kitambulisho Mama
Maria Nyerere,wakati wa   Utoaji wa vitambulisho vya Taifa,awamu ya
kwanza kwa upande wa Zanzibar,  hafla ilifanyika jana katika  viwanja
vya Baraza la Wawakilishi Chukwani, Nje ya Mji wa Zanzibar,[Picha na
Ramadhan Othman,Ikulu.]
[ Read More ]

Just in:

Inna lillahi waina ilaihi rajiun.

Ajali ya boti iliyokuwa ikitokea Pangani Tanga imezama watu wanane wamefariki wakiwemo watoto watatu. Na watu kumi na moja wamepotea baharini. Wengine wameokolewa na boti ilikuwa na jumla ya watu 35. Chombo hicho kimezama kutokana na hali ya hewa ya upepo,Mammlaka ya hali ya hewa jana mwanzoni mwa week hii imetoa tahadhari ya kuwepo kwa mvua kubwa na upepo.
[ Read More ]

Gas City: Hospitali ya Apollo kujengwa Kilwa


Wananchi wa Halmashauri ya wilaya ya Kilwa, mkoani Lindi na wakaazi wa mikoa ya kusini kwa ujumla, wanatarajia kunufaika na ugunduzi wa gesi katika visiwa vya Zafaran na Lavan vilivyopo wilayani huo. Kampuni ya Statoil kutoka nchini Norway ikishirikiana na Exxon Mobil imegundua gesi katika Visiwa vya Zafaran na Lavan vilivyopo Kitalu namba 2, Ukanda wa Pwani ya Tanzania, hususan Pwani ya Kilwa mkoani Lindi. Kutokana na ujio wa wageni hao, Watanzania hususan wakazi wa Kilwa, Lindi na Mtwara kwa jumla hawana budi kupata faida za moja kwa moja na zingine zisizo za moja kwa moja ikiwemo gesi hiyo kutumika kutengeneza umeme utakaopatikana kwa uhakika na kuuzwa kwa wananchi wote. 
Akizungumza mjini Kilwa Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya Kilwa, Adoh Mapunda amesema kuwa, madiwani, watendaji na mkuu wa wilaya wamekaa na kutafakari kwa kina juu ya faida ya kudumu itakayoonekana wilayani humo kutokana na ujio wa mradi wa gesi. Amefafanua zaidi kuwa mradi huo ni ujenzi wa hospitali ya kimataifa itakayolingana na ile ya Apollo nchini India ambayo viongozi mbalimbali duniani hukimbilia kwenda kutibiwa ambayo itajengwa na mwekezaji na itaendeshwa na taasisi nyingine ya kimataifa huku halmashauri ikiwa na hisa za kupata gawiwo la kila mwaka kutokana na faida. Mpango huo unatekelezwa kupitia utaratibu uliopo katika mikataba kwa wawekezaji kuhusu uwajibikaji na ushiriki katika masuala ya kijamii. Amesema kuwa, tayari Statoil imetenga Sh18 bilioni kuanza ujenzi wa hospitali hiyo mjini Kilwa wakati wowote kuanzia mwaka huu ambapo michoro ya hospitali hiyo ipo tayari huku ikitarajia madaktari bingwa kutoka ndani na nje ya nchi na itakuwa na wafanyakazi wataalamu, pamoja na wahudumu ambao wengi watatoka Halmashauri ya Kilwa.

[ Read More ]

Dr Shein swears in permanent secretaries for national unity government


Zanzibar President Dr Ali Mohammed Shein swears in Dr Abdulhamid Yahya Mzee at a ceremony at Zanzibar State House yesterday after appointing him Isles’ Revolutionary Council Permanent Secretary. (Photo: Ramadhan Othman)
 

Employment History

  • President
    Zanzibar

Board Memberships and Affiliations

  • Chief Secretary
    Zanzibar
  • Chief Secretary
    Zanzibar Revolutionary Council
  • Permanent Secretary
    Revolutionary Council
Zanzibar President Dr Ali Mohammed Shein yesterday sworn in the newly appointed permanent secretaries for the government of national unity.
The new permanent secretaries were appointed on Thursday evening, whereby he re-appointed all the permanent secretaries, who had saved in the sixth phase government.
According to a press statement availed to the media, Abdulhamid Yahya Mzee was appointed Chief Secretary and Secretary of the Zanzibar Revolutionary Council, while Salum Maulid Salum was appointed as Permanent Secretary in the President’s Office and Chairman for the Revolutionary Council, State House.
Others are Abdalla Juma Abdalla, Deputy Permanent Secretary (Special Government Departments), Said Abdalla Natepe, Deputy Permanent Secretary (International Cooperation and Coordination of activities of Zanzibaris living abroad), Mwinyiusi Abdalla Hassan, Deputy Permanent Secretary (Regional Administration and Local Governments).
Other permanent secretaries include Khami Mussa Omra, who has been re-appointed as Permanent Secretary in the Ministry of Finance, Economy and Development Plans and Abdi Khamis Faki Deputy Secretary in the Ministry of Finance.
Dr Shein also appointed Amina Khamis as Executive Secretary for Zanzibar Planning Commission and Joseph Abdalla Meza as Permanent Secretary in the President’s Office Civil Servant and Good Governance and his Deputy is Yakout H Yakout, Dr Omar Dadi Shajak, Permanent Secretary in First Vice President Office and Dr Ismal Seif Salum as his deputy.
Dr Khalid Said Mohammed has been appointed as Permanent Secretary in the Second Vice President Office and his deputy is Said Shaaban Said.
Dr Shein also has appointed Asaa Ahmada Rashid as Permanent Secretary in the Ministry of Constitution and Justice and his deputy is Abdughani Msoma, while Mwanaidi Saleh Abdalla has been appointed Permanent Secretary in the Ministry of Education and Vocational Training and his deputy is Mzee Abdalla Mzee Abdalla.
Mohammed Saleh Jidawi has been re-appointed in the Ministry of Health, while Dr Malik Abdalla Juma as Director General in the Ministry.
Others appointed are Vuai Idd Lila, the Ministry of Infrastructure and Communication and his deputy is Msanif Haji Mussa.
Rahma Mohammed Mshangama had been appointed to the Ministry of Social Welfare, Youth Development, Women and Children and her deputy is Msham Abadalla Khamis.
Other permanent secretaries are Ali Saleh Mwinyikai in the Ministry of Information, Culture, Tourism and Sports and his deputy is Issa Mlingoti Ali.
Other appointed permanent secretaries and their deputies are Mwalimu Ali Mwalimu (Ministry of Land, Housing, Water, and Energy), his deputy is Tahir M. Abdalla, Julian Raphael (Ministry of Trade, Industries, and Marketing), his deputy is Rashid
Ali Salum, Asha Ali Abdalla (Ministry of Labour, Peoples Economic Empowerment and Cooperatives), his deputy is Ali Khamis Juma, Othman Maalim (Ministry of Agriculture and Natural Resources), his deputies are Juma Ali Juma and Dr Bakar Asseid (Natural Resources).
The president also appointed Dr Kassim Gharib as permanent secretary in the Ministry Livestock and Fisheries, his deputy is Dr Omar Ali Ameir.
The newly appointed permanent secretaries and their deputies come from the main political CCM and CUF that form the national unity government.
Isles Constitution as amended also allows the new power-sharing government to distribute ministerial positions to the respective parties in accordance with percentage of votes scored by the parties in the general elections.
[ Read More ]

Two die in helicopter crane crash in Vauxhall, London

 
Two people have died after a helicopter crashed into a crane at a building site in central London in misty conditions, police have said.
read more http://www.bbc.co.uk/news/uk-england-21040410
[ Read More ]

Saikolojia: Namna ya kutambua tabia ya mtu


Hakuna anayependa kusahihishwa, kugombana au kukemewa mbele za watu, hii ndiyo tabia ya watu wajeuri na walio na tabia za kitukutu. Mara nyingine hudhani wanapata sifa. Wako watu wa jinsi hii ambao hawawezi kukugombeza au (kukupa vidonge vyako) mkiwa wawili peke yenu, watangoja watu wengine wawepo ndiyo waanze kubwabwaja, cha kufanya jiepushe nao.


Kwa kule kukimbiwa na marafiki, na kuwa mpweke, huongeza tabia za kitukutu na kijeuri na hii huwafanya watu hawa kutambulika haraka na kiurahisi zaidi.

Zifuatazo ni alama zitakazokutambulisha mtu jeuri na mtukutu:

a) Alama za kimaneno
Mara kwa mara hupendelea kusema maneno haya vinywani mwao.
Nakwambia bora unge…”
Wewe sichochote, silolote…”
Nakwambia, lazima u...”
Fanya vile ninavyokuambia mimi…”
Nataka u...”
Wewe endelea tu tutaona...”

b) Alama za kimwili
Hupendelea kusimama wima
Huwa wenye pozi kavu, ngumu (still and rigid pause)
Hupenda kukunja mikono
Hupenda kupayuka au kupigia wengine kelele
Hupenda kuwanyooshea wengine vidole.
Hupenda kuwazodoa wengine na vidole (hawezi kukuelekeza hadi kidole chake kikusukume)
Hupenda kupiga au kugonga meza na viti akizungumza



2. Watu wapole, waliotayari kukubali kushuka (Submissive)
Hawa ni watu wanaopenda kujitoa sadaka kwa ajili ya manufaa ya wengine. Kwa hali hii ni rahisi watu hawa kujikuta wanatumiwa vibaya na watu wengine hasa wale wajeuri na watukutu tulio waangalia awali.

Mara nyingi watu walio wapole na wanaokubali kushuka hupenda kuwatia moyo wengine wawe kama wao. Katika vizazi vilivyopita, wanawake walitegemewa zaidi kuwa watu wa kundi hili. Ni mabadiliko ya maisha na ya jamii ya leo ambayo yamemfanya hata mwanamke kuwa mjeuri na mshindani tofauti na jamii za awali.

Kwa upande mwingine mfumo wa maisha wa vizazi vya nyuma ulimweka chini mwanamke na kuzuia maendeleo yake hasa katika kujiendelezea vipawa alivyonavyo kwa vigezo tu kwamba yeye ni wakukubali chochote na wakati wowote sasa tunayaona mabadiliko kwa kiasi fulani.

Mara kwa mara watu wapole, na waliotayari kushuka wamekuwa wenye hisia za kinyonge na kutengwa, wakijihisi kutokuwa salama wakati mwingi. Kujijali, kujipenda na kujithamini kwa watu hawa siyo kwa kudumu, bali kunakuwa na nyakati za kuyumbayumba kutokana na mazingira. Hawa siyo watu wenye ujasiri ndani yao wenyewe na hata katika vile wavifanyavyo.

Mara mtu wa kundi hili anapokutana na mtu mjeuri na mtukutu, hofu na ujasiri wake hupungua sana, na anaweza kukubali kupingwa hata kama alikuwa ana haki. Kwa sababu mara nyingi watu wa jinsi hii wanajua kuwa kwa upole wao watu wengi wamekuwa wakiwatumia na kuwachezea, hii imewafanya wawe ni watu wenye vihasira vya mara kwa mara.

Kwa sababu wameunganishwa na hisia zao zaidi, ni rahisi wao kuzielezea hisia zao kwa mtu mwingine, hata kama hisia zao ni za kujutia kile walicho kifanya wenyewe. Mara nyingi husikia amani kwa yale wanayofanya au kuyaamua.

Ingawa mara nyingine mambo huwaendela tofauti na walivyopanga, watu hawa hufahamu kuwa hawanabudi kukubali kosa au na kuwa tayari kujifunza kutokana na yale makosa.

Mambo yanapowaendea vema hupenda kujisifia na kujiona walio juu. Mara nyingine misimamo yao huwashawishi na kuwavutia wengine watazame kama wao, sio watu wanaopenda kuwatumia wengine vibaya (being manipulative) kama vile kuwasema au kuwasengenya wengine, hii huwafanya kuwa na wafuasi au washabiki wengi zaidi.

Kule kujiamini kwao na kuwa na ujasiri hupunguza sana msongo wa mawazo maishani mwao na hii huwasaidia kuelekeza nishati na nguvu zao zote katika kufikia malengo waliojiwekea.

Mara kwa mara sio watu wenye mabadiliko ya hisia (change of attitude) na hii hufanya mahusiano yao na wengine kuwa yasiyoyumba na mawasiliano baina yao na wengine huwa wazi, sio watu wakuficha wanachokiona, uwazi walionao kuwaweka huru.

Hujisikia vema hujipenda na kujithamini muda mwingi. Hujijengea hisia za usalama na imani kwa sababu ya mawasiliano bora walionayo na wale wanaowazunguka, hii pia husababishwa na wao kuelewa fika wajibu wao na wajibu wa wengine pia.

Ingawa wanaweza kuwa wabishi, lakini huheshimu misimamo ya wengine na kupenda ya kwao iheshimiwe pia na hii huwafanya kuwa na ushirika na wale wanaowazunguka. Mara nyingi ni wazuri katika kuwatia wengine moyo kujitahidi zaidi.

Alam za kuwatambua:
Alama za maneno
Nahisi……. Najisikia kuu……………”
Ningependa kuu…………”
Wewe unaonaje hapa/mawazo yako nini…………..”
Unadhani njia gani bora kulishuhulikia hili ………..”
Nafikiri………..”
Hembu tu……………..”

Alama za kimwili
Hupenda kuwa wima ila wenye pozi laini (relaxed stance)
Huangalia kijasiri na kuangalia usoni (kukodoa macho).
Huwa na hisia za upole, kujitawala na kujimiliki wenyewe

Kwa vyovyote vile, mara zote unapokutana na mtu mwenye tabia yeyote kati ya hizi tatu kumbuka una haki ya kufanya yafuatayo;

Jifunze kuelezea hisia zako njema (usiogopoe au kuona aibu kwakuwa hutokuwa umejitendea haki)
Jifunze kuzielezea hisia zako mbaya au za hasira, kamwe usifunike. Mfano; “Sipendi kabisa unavyokula”
Jifunze kusema hapana, Mfano; “Hapana sitaweza kufika leo”

Toa wazo la kweli, usipake watu mafuta kwa mgongo wa chupa. Mfano; “Mimi siliafiki hilo jambo hata kidogo”
Kiri kuwa umekasirika, hasa pale ambapo haunabudi kukasirika.

Mfano: “Kweli umeniudhi sana baada ya kusema hayo maneno”. Usitoe tabasamu la mamba tu, kutabasamu wakati ndani yako unahisi kuungua moto.

source: Jamii forum.
[ Read More ]

TANZANIA YASHINDA KATIKA SHINDANO LA KUTAFUTA MAAJABU SABA YA ASILI YA BARA LA AFRIKA

Bodi ya Utalii Tanzania inapenda kuwaarifu wananchi na umma kwa ujumla kuwa Tanzania itakuwa ni
miongoni mwa nchi ambazo angalau moja ya vivutio vyake kitaingia katika orodha ya Maajabu Saba ya Asili
Barani Afrika baada ya kukamilika kwa upigaji wa kura katika shindano la kutafuta Maajabu Saba ya Asili
Barani Afrika Desemba31, 2012 na Tanzania kuwa miongoni mwa washindi

Kampeni ya kutafuta Maajabu Saba ya Asili ya Bara la Afrika ilikuwa iikiendeshwa na Taasisi ya Seven
Natural Wonders yenye makao yake makuu nchini Marekani tangu mwaka 2008 ambapo upigaji wa kura
ulihusisha Taasisi za Kimataifa ikiwemo taasisi ya uhifadhi asili wa Mazingira (IUNC) na wataalamu wengine
duniani ambao walipiga kura kwa kuzingatia zaidi umuhimu wa asili, upekee na uzuri wa kivutio husika.
Taasisi hiyo ya Seven Natural Wonders imewasiliana na Mkurugenzi Mwendeshaji wa Bodi ya Utalii Tanzania,
Dr. Aloyce Nzuki na kumfahamisha kuhusu matokeo ya awali na kumthibitishia kuwa Tanzania ni kati ya nchi
zilizoshinda na kwamba vivutio vyake zaidi ya kimoja vitakuwa miongoni mwa Maajabu hayo Saba ya Asili
Barani Afrika. Tanzania itakuwa mwenyeji wa sherehe za tukio la utangazaji wa vivutio vilivyoshinda katika
shindano hili na kwamba itakuwa ni fursa kwa Watanzania na Afrika kwa ujumla kufurahia tukio hilo na
Maajbu yatakayoshinda.
Sherehe za utangazaji wa washindi zitafanyika jijini Arusha katika Hotel ya Mt Meru Februari 11, 2013 ambapo
watu mashuhuri kutoka nchi mbalimbali Barani Afrika, na wandishi kutoka vyombo vya habari vya Kimataifa
na ndani ya nchi wataalikwa kushiriki katika sherehe hizo na kushuhudia utangazaji wa vivutio vya Tanzania na
vingine vya Afrika kuwa Maajabu Saba ya Asili Barani Afrika.
Bodi ya Utalii Tanzania inapenda kuwashukuru watu wote ndani na nje ya Tanzania walioshiriki katika kupigia
kura vivutio vya Tanzania. Vivutio vya Tanzania vilivyokuwa katika shindano hili ni Mlima Kilimnajaro,
Bonde la Ngorongoro, na Hifadhi ya Taifa ya Serengeti
Imetolewa na:
Mkurugenzi Mwendeshaji
Bodi ya Utalii Tanzania
Jengo la IPS ghorofa ya tatu
Mtaa wa Samora/Azikiwe
S.L.P 2485 D’slaam, Tanzania
[ Read More ]