Banner 468

1234453_10201664080105694_1716282793_n
Facebook

Wahasibu watakiwa kuwania CPA

-
Rehema Mwinyi.

Wahitimu wa Uhasibu na Fedha wa Chuo Kikuu Mzumbe (MU), wameshauriwa kujiendeleza kwa kufanya mitihani ya juu ya Uhasibu (CPA) na baadaye kusajiliwa katika Bodi ya Uhasibu (NBAA) ili watambulike wanataaluma.

Changamoto hiyo ilitolewa na Meneja wa Mfuko wa Pensheni wa Mashirika ya Umma (PPF), Kanda ya Mashariki na Kati, Meshack Bandawe, wakati wa hafla maalumu ya wanafunzi wanaotarajia kumaliza masomo yao ya Stashahada na Shahada.

Alisema taaluma ya uhasibu ni moja ya taaluma zinazohitaji kuwa na uaminifu na uadilifu wa kiwango cha juu kutokana na mazingira ya kazi yaliyojaa vishawishi vingi zaidi ukilinganisha na kazi nyinginezo.

Kwa mujibu wa Meneja huyo wa PPF Kanda ya Mashariki na Kati, wapo watu wenye taaluma ya uhasibu ambao wamekuwa wakiharibu sifa ya taaluma hiyo na kusababisha wananchi kupoteza imani.

Hivyo alisema ni wajibu wa wanafunzi wa chuo kikuu hicho kuheshimu sheria za kazi kwa kuwa waadilifu ili kuepukana na sifa mbaya katika utendaji wao kwa siku za usoni pindi watakapopata ajira.

Alisema watakapoingia kwenye ajira iwe ya sekta binafsi ama ya umma, wana wajibu wa kusimamia na kuhakikisha michango ya wanachama wa mifuko ya jamii ukiwamo wa PPF inawasilishwa kwa wakati ili kuepukana usumbufu baada ya watumishi kustaafu kazi ama kuondoka kwa sababu yoyote.

Leave a Reply