Banner 468

1234453_10201664080105694_1716282793_n
Facebook

Umeme waua mume, mke taabani Muhimbili

-
Rehema Mwinyi.

Baba mmoja amefariki dunia na mkewe kujeruhiwa vibaya baada ya kuangukiwa na waya wa umeme.

Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi wa Ilala, Faustine Shilogile amemtaja marehemu kuwa ni Masari Abdulhussein, 27, na aliyejeruhiwa kuwa ni Bi. Najma Swalehe, 24, wote wakazi wa Kigamboni.

Akisimulia tukio hilo, Kamanda Shilogile amesema watu hao wamekutwa na mkasa huo wakati wakiwa wamebebana kwenye pikipiki.

Amesema tukio hilo la kusikitisha limetokea katika eneo la makutano ya barabara za Uhuru na Nyamwezi, Kariakoo Jijini.

Akasema Bw. Masari ndiye aliyekuwa akiendesha pikipiki hiyo yenye namba za usajili T 311 AMS aina ya Sangly huku akiwa amembeba mkewe na kuwa walipofika eneo hilo, waliangukiwa na waya wa umeme wenye moto na kusababisha wajeruhiwe vibaya.

Kamanda Shilogile amesema wataalam wa Shirika la Umeme nchini, Tanesco waliitwa mara moja na walipofika wakawatoa na kuwakimbiza katika Hospitali ya Taifa Muhimbili.

Akasema hata hivyo mwanaume, alifariki dunia wakiwa njiani na mwili wake umehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti cha Hospitali ya Taifa, Muhimbili.

Amesema mkewe Bi. Najma naye amelazwa hospitalini hapo ambapo anaendelea kupewa matibabu.

Leave a Reply