Banner 468

1234453_10201664080105694_1716282793_n
Facebook

Zanzibar yakubwa na uhaba wa petroli

Zanzibar inakabiliwa na uhaba mkubwa wa mafuta ya petroli hali inayotishia kuathiri sekta za uchumi.

Uhaba huo wa petroli umekuja huku Zanzibar ikiendelea kukabiliwa na ukosefu wa umeme kwa siku 42 mfululizo.

Uhaba wa mafuta umeanza kujitokeza wiki iliyopita na kusababisha baadhi ya wananchi wanaomiliki magari kulazimika kuyafungia majumbani na kuanza kutumia usafiri wa daladala na wengine kutembea kwa miguu.

Magari yanayotoa huduma hivi sasa ya usafiri ni yale yanayotumia mafuta ya dizeli lakini idadi kubwa ya magari yanayotumia petroli yamelazimika kusitisha huduma za usafiri na kusababisha msongamano wa watu katika vituo.

Kufuatia kuadimika kwa mafuta ya petroli, kumeibuka biashara ya magendo ambapo lita moja ya petroli imekuwa ikiuzwa kwa Sh. 2,000 badala ya 1,480.

Uchunguzi wa Nipashe umegundua kuwa mafuta ya petroli yamekuwa yakiuzwa kwa bei za ulanguzi nje ya vituo vya mafuta, hasa katika maeneo ya Kijangwani, Mikunguni Gulioni.

Kampuni zinazaoingiza mafuta Zanzibar ni Zanzibar Petrolium, GAPCO, pamoja na Kampuni ya United Petroleum, lakini wateja wake wamekuwa wakifika katika vituo na kuondoka bila ya kupata huduma hiyo.

Mafuta ya petroli yamechukua nafasi kubwa katika shughuli za kiuchumi baada ya Zanzibar kukosa huduma ya umeme kuanzia Desemba, mwaka jana, baada ya kifaa aina ya spliter kulipuka katika kituo cha Fumba.

Kiongozi mmoja mwandamizi kutoka Kampuni ya United Petroleum, alisema uhaba huo wa mafuta umejitokeza baada ya nishati hiyo kuadimika katika bandari ya Mombasa, Kenya kufuatia nishati hiyo kuchelewa kuwasili kutoka nje ya nchi.

Alisema uhaba huo wa mafuta katika bandari ya Mombasa, unatarajia kumalizika kuanzia Januari 30, mwaka huu kwa vile meli zenye mafuta zinatarajiwa kuwasili katika bandari hiyo.

Hata hivyo, alisema baada ya kujitokeza upungufu huo wa mafuta, waliamua kutafuta mafuta kutoka katika meli moja iliyofunga gati, katika Bandari ya Dar es Salaam, lakini hawakufanikiwa kutokana na meli hiyo kuwa katika foleni kubwa ya kusubiri kuteremsha mafuta Tanzania Bara.

[ Read More ]

NECTA lawamani kwa kushusha ufaulu wa wanafunzi


WAZIRI wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Jumanne Maghembe ameeleza sababu kubwa iliyosababisha kushuka kwa ufaulu wa elimu ya msingi katika matokeo ya mtihani wa darasa la saba mwaka jana kuwa ni pamoja na Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA), kudhibiti uvujaji wa mitihani na uchache wa walimu uliopo nchini.

Profesa Maghembe alitaja sababu nyingine iliyosababisha wanafunzi kufanya vibaya katika mtihani wa darasa la saba mwaka jana kuwa ni kutokuwepo uwiano sawa wa matumizi ya vitabu katika shule za msingi kote nchini.

Akifungua mkutano wa siku tatu wa wadau wa elimu nchini mjini hapa juzi, Profesa Maghembe alisema kitendo cha Baraza la Mitihani la Taifa kudhibiti uvujaji wa mitihani, umesababisha kushuka kwa ufaulu kutokana na wanafunzi wengi kutegemea kupewa mitihani.

Alisema licha ya NECTA kudhibiti hali hiyo, bado wapo baadhi ya watu ambao wamekuwa wakichukua mitihani iliyopita na kuichapa upya na baadaye kuiuza mitaani kwa madai kuwa hiyo ndiyo mitihani yenyewe.

Kutokana na hali hiyo, Profesa Maghembe alisema imekuwa ikichangia kwa kiasi kikubwa kwa wanafunzi kufanya vibaya kwa kuwa wamekuwa wakitarajia kuwa mitihani waliyonunua ndiyo watakayoifanya.

Profesa Maghembe alisema hakuna utaratibu wa shule zote nchini kuwa na kitabu kimoja kinachotumika katika kufundishia na badala yake kila shule imekuwa ikinunua kitabu ambacho inaona ni kizuri na kinafaa kufundishia.

Alisema kitendo cha biashara kuingia katika shule za msingi, kimechangia kuharibu elimu ya Tanzania ambapo aliwataka maofisa elimu wa mikoa na wilaya, maofisa elimu taaluma na taasisi za elimu kuangalia na kukubaliana kuchagua vitabu vinavyowiana ambavyo vitatumika kufundishia katika shule zote nchini.

Kutokana na wanafunzi kufanya vibaya katika mtihani wa darasa la saba mwaka jana, wadau wa elimu wakiwemo maofisa elimu wa mikoa na wilaya, maofisa taaluma wa mikoa na wilaya, wakuu wa vyuo vya ualimu na wakurugenzi wa halmashauri, wanakutana mjini hapa chini ya uenyekiti wa Waziri Maghembe kujadili kwa kina sababu nyingine zilizosababisha wanafunzi kufanya vibaya katika mtihani huo.

 
[ Read More ]

Mwanajeshi aliyeshambulia polisi afungwa miaka 12

MAHAKAMA ya Wilaya ya Bukoba imemhukumu askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Koplo Katarama, kifungo cha miaka 12 jela, baada ya kupatikana na hatia ya makosa matatu likiwamo la kumchania sare za kazi askari Polisi wa kike, kuharibu simu ya upepo na kumchania nguo ya ndani.

Hukumu hiyo ilitolewa Januari 5 mwaka huu katika Mahakama hiyo na Hakimu Richard Maganga ikielezwa kuwa mtuhumiwa ambaye hakuwa mahakamani hapo siku hiyo, alitenda makosa hayo Desemba 7, 2007 saa mbili asubuhi, eneo la Rwamishenye mjini hapa wakati polisi huyo akiwa kazini.

Awali Mahakama hiyo ilielezwa na Mwendesha Mashtaka wa Polisi, Ibrahimu Jumanne, kuwa Koplo Katarama siku hiyo alisimamishwa Rwamishenye akiwa katika gari la kiraia na wanajeshi wengine na baada ya gari kusimama, aliteremka na kumshambulia Sajini Wigesa aliyesimamisha gari hilo.

Ilidaiwa kuwa mshtakiwa alimkaba polisi huyo na kumwangusha katika barabara ya lami na kumsababishia michubuko magotini na maumivu makali kichwani, huku akimchania mavazi yake, kuharibu simu, kofia ya Polisi na kumchania nguo ya ndani.

Jumanne alidai kuwa mshtakiwa alimzuia polisi huyo kufanya kazi yake na baada ya upande wa mashtaka kuwasilisha mashahidi watatu, mtuhumiwa alitiwa hatiani na kuhukumiwa kifungo hicho.

Katika kosa la kwanza la kumzuia polisi kufanya kazi yake na la kumjeruhi askari huyo, alihukumiwa kifungo cha miaka mitano huku kwa la kumchania nguo, kuharibu simu na kofia alihukumiwa miaka miwili.

[ Read More ]

Mwanamke Amuua Mpenzi Wake Kwa Kumkalia


Mwanamke mmoja nchini Marekani mwenye uzito wa kilo 136 amepandishwa kizimbani kwa kosa la kumuua mpenzi wake aliyezaa naye watoto watatu kwa kumkalia hadi alipofariki.

Taarifa ya polisi wa Cleveland nchini Marekani ilisema kuwa mwanamke huyo aliyejulikana kwa jina la Mia Landigham na mpenzi wake Mikal Middleston-Bey walikuwa kwenye mzozo wa ndani ya nyumba mnamo mwezi wa nane mwaka jana.

Taarifa zaidi zilisema kuwa mzozo huo ulikuwa mkubwa sana na kupelekea Mia aliyekuwa na uzito wa kilo 136 wakati huo kurushiana makonde na Mikal.

Mia alifanikiwa kumwangusha chini Mikal ambaye alikuwa mwembamba sana mwenye mwenye uzito wa kilo 54.4 tu. Mia alimkalia Mikal kwa dakika kadhaa aliponyanyuka Mikal alikuwa hapumui tena na alifariki dakika chache baadae.

Kufuatia tukio Mia alipandishwa mahakamani juzi jumatano na kuhukumiwa kwenda jela miaka mitatu na kufanya kazi za kuitumikia jamii kwa masaa 100.

Mia alikiri kosa lake la kumuua bila kukusudia mpenzi wake huyo ambaye amezaa naye watoto watatu. Mia pia aliiomba radhi familia ya marehemu kwa kusababisha kifo chake.

Wakili wa Mia aliiambia mahakama kuwa uhusiano wa Mia na Mikal ulikuwa na historia ya migogoro mingi na alimuomba jaji ampunguzie adhabu Mia kwa kuwa hana historia ya makosa ya jinai.

"Napenda kusema kuwa naomba radhi na nimehuzishwa na yaliyotokea natamani ningekuwa na uwezo wa kuurudisha uhai wake", alisema Mia.

source nifahamishe.com
[ Read More ]

Maiti za watoto 4 zaokotwa ufukweni

WATOTO wanne wa mtaa mmoja wamekufa kutokana na kifo cha maji baada ya watoto hao kutoroka majumbani mwao na kwenda bichi kuogelea na kifo kuwakuta huko.
Watoto hao majirani wameacha simanzi na vilio kutawala katika eneo la Jangwani Mchikichini jijini Dar es Salaam kutokana na watoto hao wanne majirani kufa maji ka pamoja wakati walipokwenda kuogelea.

Akitoa taarifa hiyo kwa wanahabari jijini jana, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Temeke, Bw.Liberatus Sabasi, alisema kuwa maiti za watoto hao ziliokotwa juzi majira ya saa 11 jioni, ufukweni mwa Bahari ya Hindi, eneo la Bomba la Maji Machafu, Feri Temeke.

Alisema watoto hao wote kwa pamoja walitoweka nyumbani kwa wazazi wao Januari 16 na kupatana waende kuogelea baharini.

Alisema kuwa baada ya kuogelea watoto hao walizidiwa na maji kisha kufariki dunia ambapo miili yao ilikutwa jana karibu na bomba la maji machafu.

Watoto hao ni Seleman Abdalah (11), Muhsin Salim (9), Abeid Salum (8- 9) na Abubakar Mohamed (8-9), wote wakazi wa Jangwani Mchikichini
Alisema uchunguzi wa kina utafanyika na baada ya hapo watoto hao watazikwa pamoja makaburi ya Ilala Kota jijini.

Katika tukio jingine Mwanamke aliyetamabulika kwa jina la Zaitun Waziri (28), mkazi wa Vijibweni CCM, amekutwa amekufa baada ya kujinyonga kwa kutumia mtandio wake alioutundika kwenye mti.
Kamanda Sabasi alisema kuwa tukio hilo lilitokea jana saa 3 usiku, huko Vijibweni karibu na Shule ya Msingi Vijibweni.

Alisema kiwiliwili cha mwanamke huyo kilikutwa kikining'inia juu ya mti ambapo mwanamke huyo hakuweza kuacha ujumbe wowote uliomsababisha afanye hivyo.

Maiti imehifadhiwa chumba cha maiti Hospitali ya Temeke na polisi wanaendelea na uchunguzi zaidi.



source.nifahamishe.
[ Read More ]

Majambazi wacharuka, waua watu 14 Ukerewe, waliteka kisiwa

WIMBI la ujambazi linazidi kutikisa nchi baada ya watu 14 kuuawa na wengine 17 kujeruhiwa kwa risasi katika shambulio lililofanywa na kundi la majambazi kwenye kisiwa kidogo cha Izinga kilicho wilayani Ukerewe na wengine 17 kujeruhiwa kwa risasi.

Katika salamu zake za Mwaka Mpya, Rais Jakaya Kikwete alilipongeza Jeshi la Polisi kwa kufanikiwa kupunguza wimbi la ujambazi, lakini siku chache baadaye kuliripotiwa matukio makubwa ya ujambazi, likiwemo la mkoani Ruvuma ambako askari polisi walinusurika kuuawa baada ya kushambuliwa na majambazi na kuporwa bunduki mbili.

Tukio jingine lilitokea mkoani Mwanza ambako jambazi mmoja aliuawa wakati polisi wakirushiana risasi na kundi la majambazi katika jaribio la uporaji kwenye mgahawa wa UTurn.

Hali imekuwa mbaya zaidi kwenye kisiwa cha Izinga kilicho Ziwa Victoria ambako majambazi hao walivamia majira ya saa 9:25 usiku.

Watu walioshuhudia tukio hilo waliiambia Mwananchi kuwa umati wa watu ulijitokeza kujaribu kupambana na majambazi hao baada ya kusikia kelele za kuomba msaada.

Mashuhuda hao walisema baada ya wananchi kujitokeza, mmoja wa majambazi hao aliwafyutulia risasi na kasababisha majeruhi na vifo vya watu hao.

Waliongeza kuwa awali waliposikia mlio wa bunduki, walidhani ni baruti, lakini baada ya kelele hizo walijikusanya kwa ajili ya kuwakabili na wananchi wengine walienda kujaribu kuharibu mtumbwi wao ili wasiutumie kutoroka, ndipo majambazi hao wakamimina risasi na kuua watu zaidi.

Walidai kuwa kundi la majambazi hao lilivamia kisiwa hicho usiku likitumia mitumbwi miwili ya injini, lakini wananchi walibaini kuingia kwao na kuwazingira. Baada ya kubaini kuwa wamezingira, walianza kufyatua risasi na kusababisha vifo vya wananchi saba.

Katika mashambulizi hayo wavamizi hao waliweza kujeruhi watu wengine 17 na wao wananchi kufanikiwa kuwaua wavamizi hao wawili.

Akizungumzia tukio hilo, mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya ya Ukerewe, Queen Mwashinga Mlozi alisema kati ya watu hao waliokufa wawili wanasadikiwa kuwa ni majambazi.

Mlozi ambaye pia ni mkuu wa wilaya ya Ukerewe alisema tayari taarifa ya tukio hilo ameifikisha kwa uongozi wa mkoa na kuongeza kuwa mkuu wa mkoa wa Mwanza, Abbas Kandoro akiongozana na kamati ya ulinzi na usalama walifika eneo la tukio ili kupata taarifa zaidi za tukio hilo.

Kaimu Mganga Mkuu wa wilaya ya Ukerewe, Dk Faustine Nkinga alisema hali za majeruhi bado ni mbaya na kwamba wanaendelea na kazi ya kunusuru maisha yao kwa sababu kati yao wanne walipoteza damu nyingi na wengine walifanyiwa upasuaji ili kuwaondoa risasi kwenye miili yao na wengine wamehamishiwa Hospitali ya Bugando.

Mkuu wa mkoa, Abbas Kandoro, ofisa usalama wa mkoa, Jason Mutashongerwa na kamanda wa polisi mkoa, Jamal Rwambow waliondoka asubuhi jana kwenda eneo la tukio kujionea hali halisi ya uvamizi huo.

Kandoro alisema kuwa majeruhi wote 17 walihamishiwa Hospitali ya Rufaa ya Bugando kwa ajili ya matibabu zaidi kutokana na hospitali ya Ukerewe kutomudu kuwahudumia wagonjwa hao.

Naye Kamanda Rwambow alisema kuwa watu waliothibitika kuuawa eneo la tukio kisiwani humo ni saba na watu wengine watano ambao walipelekwa wakiwa majeruhi kutibiwa walifariki wakati wakitibiwa. Habari zilizofika baadaye zilieleza kuwa watu wengine watatu walipoteza maisha.

"Mpaka sasa niko na viongozi wengine wa kamati ya ulinzi na usalama wa mkoa tukielekea eneo la tukio, lakini ninachoweza kukueleza ni kuwa tukio lipo na watu wamekufa na kati ya hao waliokufa wawili ni majambazi ambao waliuawa na wananchi.

Lakini taarifa kamili nitatoa baada ya uchunguzi kamili na kufika eneo la tukio," alieleza Kamanda Rwanbow kwa njia ya simu.

Mbunge wa Ukerewe, Getrude Mongella alisema kuwa Jeshi la Polisi linastahili lawama kutokana na tukio hilo kwa sababu wananchi wa visiwa vya wilayani Ukerewe walichanga Sh3 milioni ili wajengewe kituo, lakini hadi leo jeshi hilo limeshindwa kutoa maelekezo ya kufanikisha nia hiyo.

"Nimesikitishwa na tukio hili, lakini jeshi la polisi linastahili lawama kutokana na kuzembea kutoa maelekezo kwa wananchi ambao tayari wamechanga Sh3 milioni za kujengea vituo vya polisi katika visiwa vya uvuvi," alieleza Mongella.

Tukio hili linaufanya mkoa wa Mwanza kuwa miongoni mwa mikoa inayoongoza kwa matukio ya ujambazi. Wananchi wamekuwa wakivamia kila mara na kujeruhiwa kwa mapanga, nondo na silaha za moto na kuporwa mali na fedha.

Julai mwaka jana watu wanaosadikiwa kuwa majambazi walivamia na kuteka Kisiwa cha Ziragula na kujeruhi wananchi zaidi ya 13 na kupora mali na fedha.

Januari 14 mwaka huu majambazi pia walivamia eneo la uvuvi la Igombe na kupora Sh700,000 na kujeruhi wananchi watatu.

source..mwananchi.

[ Read More ]

Kondoo Azaliwa Akiwa na Sura ya Binadamu



Kondoo aliyezaliwa nchini Uturuki akiwa na sura ya binadamu amewashangaza mamia ya watu duniani na kuwa gumzo kwenye vyombo mbali mbali vya habari duniani.
Kondoo huyo aliyezaliwa akiwa amefariki ana sura kama ya binamu lakini mwili wake ni kama wa kondoo.

Kondoo huyo alizaliwa katika zahanati ya mifugo katika kijiji kimoja katika mji wa Izmir nchini Uturuki.

Erhan Elibol, bwana mifugo aliyemzalisha kwa njia ya upasuaji kondoo aliyekuwa na mimba, alielezea mshtuko aliopata baada ya kuona kichanga cha kondoo kilichozaliwa kina sura inayofanana na binadamu.

"Nimewahi kuona maumbile mbali mbali ya ajabu ya ng'ombe na kondoo, nimewahi kuona ng'ombe mwenye jicho moja, ng'ombe mwenye vichwa viwili na ng'ombe mwenye miguu mitano, lakini kwa mara ya kwanza ndio nimekutana na kiumbe kama hiki", alisema afisa mifugo huyo mwenye umri wa miaka 29.

Kichanga hicho cha kondoo kina macho, pua na mdomo kama binadamu isipokuwa masikio ndio ya kondoo.

Wataalamu wa mifugo wanafanya uchunguzi kujua chanzo cha kondoo huyo kuzaliwa akiwa na sura kama ya binadamu.

Mwezi septemba mwaka jana, mbuzi mmoja nchini Zimbwabwe alizaa kichanga cha mbuzi kikiwa na kichwa kama cha binadamu.

Kichanga hicho cha mbuzi kilikuwa hai kwa masaa kadhaa kabla ya wanakijiji waliotishika na sura yake kuamua kukiua.

Gavana wa jimbo alilozaliwa kichanga hicho cha mbuzi alisema kuwa mbuzi huyo alizaliwa kufuatia matunda ya uhusiano usiofaa kati ya mbuzi mwanamke na binadamu.


source.nifahamishe.com
[ Read More ]

'Tens of thousands' killed in Haiti quake


Haitian President Rene Preval said estimates of the death toll in the devastating earthquake in capital Port-au- Prince could easily be in the tens of thousands, while other officials said more than 100,000 may have perished.

'Up to now I've heard 50,000, I've heard 30,000. Let's say, it's too early to give a number,' Preval told broadcaster CNN, conceding that any sort of official estimate was extremely difficult. 'I am still trying to understand myself the magnitude of the event.'

Earlier, he had told The Miami Herald that thousands may have been killed in the magnitude 7.0 earthquake that rocked the country Tuesday afternoon, and issued an appeal for world assistance. The damage was centred in and around the capital Port-au-Prince, home to about 1.9 million people.

Figures for the number of dead remain murky as the government tries to assess the damage.

Speaking on CNN, Prime Minister Jean-Max Bellerive said: 'I believe that we are well over 100,000' dead, based on the number of buildings that have collapsed.

The UN mission in Haiti said Wednesday that the country suffered 'massive and broad' destruction from the devastating earthquakes which may result in large number of casualties.

Fifty to 100 UN staff remained unaccounted for a day after the earthquake, said Vicznezo Pugliese, spokesman for the UN Stabilization Mission in Haiti (MINUSTAH). Separate reports say the dead included soldiers from Brazil, China and Jordan.

The end death toll could amount to the largest number of deaths ever for any UN single mission. UN officials warned that the situation remained fluid because the quake and its aftershocks had cut off communication lines between UN headquarters in New York and the mission in Haiti.

Pugliese said hotels, hospitals, schools and the national prison in Port-au-Prince all suffered extensive damage. Electricity was interrupted and water was in short supply.

'Casualties, which are vast, can only be estimated,' Pugliese said in a statement made available at UN headquarters in New York.

The missing staff had worked in the main MINUSTAH office, a six-storey concrete building which collapsed. Normally, between 200 and 250 UN staff worked in the main office building but many may have left before the quakes struck.

Ten other staff were still unaccounted for who worked for UN agencies like the UN Development Programme, some of whom were in hotels.

Hundreds of thousands of Haitians slept in the streets Tuesday night after the earthquake struck, fearful that their houses would collapse. UN soldiers and police patrolled Port-au-Prince since the earthquake to maintain order and security.

The UN Security Council held a minute of silence before it met Wednesday and issued a statement expressing 'deepest sympathy and solidarity' to Haitians killed or affected by the catastrophe.

The 15-nation council also voiced support for the government of Haiti and called on UN members to assist the country in rescuing the survivors.

John Holmes, the top UN coordinator for humanitarian emergency, said there was no 'reliable information at the moment'.

The earthquake with magnitude of 7 on the Richter scale struck the impoverished Caribbean nation Tuesday right before 5 p.m. local time.

Holmes said a Chinese search and rescue team had arrived in Port-au-Prince. There are 119 Chinese police in the UN mission in Haiti. Taiwan was sending 55 rescue workers and two search-and-rescue dogs, Taiwan officials said earlier Wednesday.

US and other country rescue teams were scheduled to reach Haiti in coming days.

[ Read More ]

Togo footballer describes team's bus ambush attack


Togo's national football team has been attacked by an armed gang, reports say several players were wounded and the driver was killed when attackers opened fire with machine guns.
The team was travelling by bus from Congo Brazzaville to Angola for the Africa Cup of Nations.
Thomas Dossevi, who was onboard the bus, said that all the windows of the bus were smashed and everyone laid flat under their seats as the attack happened.
The footballer, who plays both for Togo and FC Nantes in France, describes his experience to to the BBC's Owen Bennet Jones.
[ Read More ]

HAPPY NEW YEAR...





Namshukuru Mwenyezi mungu kwa kunijalia kuuona mwaka mpya wa kiislam na pia mwaka 2010..pia napenda kuwashkuru wale wote walionisupport kwa njia moja au nyengine ktk kuufanya mwaka 2009 kuwa so special...especial my belove mama. i love you mama.ila nawashkuru all hater kwa kunichukia na pia kunikatisha tamaa kuwa sitaweza kufanya kitu..kupitia chuki zao zimenifanya kuwa jasiri na kuwa na moyo wa kuendeleaza yale niliyopanga.....nimewasamehe wote walionikosea ktk njia 1 au nyengine ila kwa kuwa am not perfect nawaomba msamaha wote nilowakosea.....let us open another page with alot of success...amin thanks all... happy new year..





i love mama.you a so special......

[ Read More ]